Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,400
- 465,165
- Thread starter
- #21
SEHEMU YA 21:
Najua nimekuhamisha kwenye mkasa wangu baada ya kuingia habari nyingine ambayo niliamini ni lazima nanyi muijue kwani sehemu ya simulizi hii ni kuelezea makosa ya kibinadamu ili ujifunze kupitia makosa yetu.
Waswahili wana usemi kuwa hasidi hana sababu. Mwaka tangu nijifungue kumbe kulikuwa na moto unawaka taratibu, sina habari. Kitendo changu cha kuzaa watoto wa kike kiiuudhi familia ya mume wangu pamoja na mume wangu.
Taratibu wifi zangu wakaanza chokochoko zao kwa kunitolea maneno ya kejeri kuwa nitawazalia watoto wa kike mpaka lini nani atakuwa mrithi wa mali za mume wangu.
Taarifa zilizonifikia kutoka katika chanzo changu makini zilisema, kama nitaendelea kumjazia mitoto ya kike basi si muda mrefu nyumba nitaiona chungu.
Kama kawaida taarifa rasmi ilinifikia kwa kunieleza. Nakumbuka vizuri siku hiyo nilikuwa namuosha mtoto baada ya kumlisha uji.
"Shoga una mpya?" Shositi wangu alianza kuniuliza swali ambalo lilifanya mapigo ya moyo yalipuke kwa kujua kwa ujio ule kuna jambo zito.
"Ipi tena hiyo mpenzi?"
" Mambo yameanza upya."
"Mambo gani?"
"Wanadamu kweli hawana shukrani yaani kila nikiwaangalia wifi zako siwamalizi."
"Kivipi mpenzi?" "Yaani wameanzisha kampeni mpya ya kukutoa tena ndani."
"Ipi hiyo mbona kila kukicha hila za wanadamu zinaongezeka Yarabi." Mapigo ya moyo ulipiga dhahili "Ni hivi baada ya kufeli mpango wao wa kukutoa ndani baada ya kupata mtoto. Sasa wamekuja na mpya eti umewajazia malaya nani atakuwa mrithi wa mali za mumeo.
“Imeanzishwa kampeni nyingine ya kutafuta mtoto wa kiume nje ya ndoa ili kukung'oa ndani."
Habari zile zilinishtua na kuninyima raha. Nilijiuliza kosa langu nini mpaka wanifuatilie maisha yangu.
"Basi ndiyo mpango wao na mumeo siku hizi kila akitoka kazini anaanzia kwa bi mdogo mwingine ndipo arudi kwako. Yamerudi ya wakati ule ulipochelewa kupata mtoto."
Nilijikuta moyo ukiniuma na kuona kila moyo ukitulia wanaanzisha mapya. Nilipanga baada ya kuondoka shoga yangu niende kwa dada kumueleza habari zile. Sikuamini wanangu kuonekana machangudoa, kosa langu nini kuzaaa watoto wa kike?
Najua nimekuhamisha kwenye mkasa wangu baada ya kuingia habari nyingine ambayo niliamini ni lazima nanyi muijue kwani sehemu ya simulizi hii ni kuelezea makosa ya kibinadamu ili ujifunze kupitia makosa yetu.
Waswahili wana usemi kuwa hasidi hana sababu. Mwaka tangu nijifungue kumbe kulikuwa na moto unawaka taratibu, sina habari. Kitendo changu cha kuzaa watoto wa kike kiiuudhi familia ya mume wangu pamoja na mume wangu.
Taratibu wifi zangu wakaanza chokochoko zao kwa kunitolea maneno ya kejeri kuwa nitawazalia watoto wa kike mpaka lini nani atakuwa mrithi wa mali za mume wangu.
Taarifa zilizonifikia kutoka katika chanzo changu makini zilisema, kama nitaendelea kumjazia mitoto ya kike basi si muda mrefu nyumba nitaiona chungu.
Kama kawaida taarifa rasmi ilinifikia kwa kunieleza. Nakumbuka vizuri siku hiyo nilikuwa namuosha mtoto baada ya kumlisha uji.
"Shoga una mpya?" Shositi wangu alianza kuniuliza swali ambalo lilifanya mapigo ya moyo yalipuke kwa kujua kwa ujio ule kuna jambo zito.
"Ipi tena hiyo mpenzi?"
" Mambo yameanza upya."
"Mambo gani?"
"Wanadamu kweli hawana shukrani yaani kila nikiwaangalia wifi zako siwamalizi."
"Kivipi mpenzi?" "Yaani wameanzisha kampeni mpya ya kukutoa tena ndani."
"Ipi hiyo mbona kila kukicha hila za wanadamu zinaongezeka Yarabi." Mapigo ya moyo ulipiga dhahili "Ni hivi baada ya kufeli mpango wao wa kukutoa ndani baada ya kupata mtoto. Sasa wamekuja na mpya eti umewajazia malaya nani atakuwa mrithi wa mali za mumeo.
“Imeanzishwa kampeni nyingine ya kutafuta mtoto wa kiume nje ya ndoa ili kukung'oa ndani."
Habari zile zilinishtua na kuninyima raha. Nilijiuliza kosa langu nini mpaka wanifuatilie maisha yangu.
"Basi ndiyo mpango wao na mumeo siku hizi kila akitoka kazini anaanzia kwa bi mdogo mwingine ndipo arudi kwako. Yamerudi ya wakati ule ulipochelewa kupata mtoto."
Nilijikuta moyo ukiniuma na kuona kila moyo ukitulia wanaanzisha mapya. Nilipanga baada ya kuondoka shoga yangu niende kwa dada kumueleza habari zile. Sikuamini wanangu kuonekana machangudoa, kosa langu nini kuzaaa watoto wa kike?