Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,400
- 465,175
- Thread starter
- #101
Sehemu ya 72.
Nilimwangalia kwa hamu kubwa yule mama kwani niliamini ujuaji wake ulikuwa na manufaa kwa yale mawazo yangu yenye utata kuhusu kauli ya yule kijana aliyedai anaishi nyumbani kwa yule mama.
"Leo umechelewa kufunga mwanangu! Wateja walikuwa wengi sana nini?" alisema yule mama jirani akiwa anafika kibandani kwangu na kusimama karibu na mimi huku akiwa anajifunga vizuri kitenge alichovaa.
"Si sana ndiyo tunajiandaa andaa sasa kufunga lakini namalizia kwanza kupaka vanishi hiki kitanda cha mteja," nilimjibu.
"Kumbe wateja wapo mpaka wa vitanda. Hongera sana," aliniambia kwa kushangaa.
"Kwani mama ukiwa na watoto si lazima utahitaji vitanda mara kwa mara," nilimwambia ili kumchokonoa kwa yale mawazo yangu.
"Sijui hao wenye watoto wanaohitaji vitanda, mimi nilimaliza siku nyingi sana," alinijibu.
"Kufanya nini?" nilimuuliza.
"Si kuzaa. Mimi nilishazaa mambo ya vitanda nilishamaliza navyo siku nyingi kama kuna wanaochonga kwa ajili ya watoto ni wale wanaozaa siku hizi."
Kauli hiyo nayo ilinishangaza pia, kwani ilipingana moja kwa moja na kauli ya yule kijana aliyeondoka.
"Kwani mama huna watoto wadogo, kama vijana hivi?" nilimuuliza huku nikimwangalia kimachalemachale.
"Aa, wapi! Wanangu wote wakubwa wanajitegemea tena wameoa na kuolewa wako makwao," alinijibu huku akitabasamu.
"Ina maana unaishi peke yako siku zote hizi?" nilimuuliza swali ambalo hata yeye mwenyewe kabla ya kunijibu, alicheka kwanza.
Najua kwanini alicheka, kwa sababu hata siku moja sijawahi kumwona mtu mwingine ndani ya nyumba yake sasa iweje nimuulize?
"Unanichekesha sana mwanangu. Kuna siku umekuja nyumbani ukamuona mtu mwingine zaidi ya mimi mama yako?" aliniuliza akiendelea kucheka lakini huku akigeukageuka kuangalia huku na kule.
Ni kweli sijawahi kumwona mtu ndani ya nyumba yake zaidi ya yeye. Hata mgenu sijawahi kumwona.
Na kama ilivyosema awali kuwa, kawaida ya yule mama ilikuwa kwamba hata akienda sokoni au popote pengine lakini mbali na nyumbani kwake, lazima funguo azilete kwangu mpaka atakaporudi. Ingawa sifahamu kwanini alikuwa akiziacha wakati anaishi peke yake. Sasa yule kijana alitokea wapi?
Je nini kitaendelea?
Nilimwangalia kwa hamu kubwa yule mama kwani niliamini ujuaji wake ulikuwa na manufaa kwa yale mawazo yangu yenye utata kuhusu kauli ya yule kijana aliyedai anaishi nyumbani kwa yule mama.
"Leo umechelewa kufunga mwanangu! Wateja walikuwa wengi sana nini?" alisema yule mama jirani akiwa anafika kibandani kwangu na kusimama karibu na mimi huku akiwa anajifunga vizuri kitenge alichovaa.
"Si sana ndiyo tunajiandaa andaa sasa kufunga lakini namalizia kwanza kupaka vanishi hiki kitanda cha mteja," nilimjibu.
"Kumbe wateja wapo mpaka wa vitanda. Hongera sana," aliniambia kwa kushangaa.
"Kwani mama ukiwa na watoto si lazima utahitaji vitanda mara kwa mara," nilimwambia ili kumchokonoa kwa yale mawazo yangu.
"Sijui hao wenye watoto wanaohitaji vitanda, mimi nilimaliza siku nyingi sana," alinijibu.
"Kufanya nini?" nilimuuliza.
"Si kuzaa. Mimi nilishazaa mambo ya vitanda nilishamaliza navyo siku nyingi kama kuna wanaochonga kwa ajili ya watoto ni wale wanaozaa siku hizi."
Kauli hiyo nayo ilinishangaza pia, kwani ilipingana moja kwa moja na kauli ya yule kijana aliyeondoka.
"Kwani mama huna watoto wadogo, kama vijana hivi?" nilimuuliza huku nikimwangalia kimachalemachale.
"Aa, wapi! Wanangu wote wakubwa wanajitegemea tena wameoa na kuolewa wako makwao," alinijibu huku akitabasamu.
"Ina maana unaishi peke yako siku zote hizi?" nilimuuliza swali ambalo hata yeye mwenyewe kabla ya kunijibu, alicheka kwanza.
Najua kwanini alicheka, kwa sababu hata siku moja sijawahi kumwona mtu mwingine ndani ya nyumba yake sasa iweje nimuulize?
"Unanichekesha sana mwanangu. Kuna siku umekuja nyumbani ukamuona mtu mwingine zaidi ya mimi mama yako?" aliniuliza akiendelea kucheka lakini huku akigeukageuka kuangalia huku na kule.
Ni kweli sijawahi kumwona mtu ndani ya nyumba yake zaidi ya yeye. Hata mgenu sijawahi kumwona.
Na kama ilivyosema awali kuwa, kawaida ya yule mama ilikuwa kwamba hata akienda sokoni au popote pengine lakini mbali na nyumbani kwake, lazima funguo azilete kwangu mpaka atakaporudi. Ingawa sifahamu kwanini alikuwa akiziacha wakati anaishi peke yake. Sasa yule kijana alitokea wapi?
Je nini kitaendelea?