Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 152,901
- 453,430
Mtunzi Juma hiza
Sehemu ya 01.
Naitwa Abdul Mensah, ni mzaliwa wa Mabawa, Tanga mjini. Nilipomaliza shule ya msingi mwaka 1992 sikubahatika kuendelea na masomo ya sekondari hivyo nilikuja jijini Dar kwa lengo la kutafuta kazi ya kufanya. Kikubwa kilichonileta Dar ni kutokana na familia yetu kuwa fukara.
Hapa Dar nilifikia Manzese kwa kaka wa rafiki yangu niliyekuwa nimesoma naye shule ya msingi.
Kibaraua changu cha kwanza kukipata kilikuwa cha kuwa msaidizi wa fundi wa kujenga nyumba, kule Ubungo Kibangu. Nilifanya kazi hii kwa muda wa miezi miwili nikaona hainilipi, hivyo nikaacha na kuanza kuuza karanga. Pia nikaja acha mwezi mmoja mbele. Nikajitosa kwenye kujifunza kazi ya ufundi seremala.
Aliyenipa wazo hili ni kaka wa rafiki yangu ambaye alisema afadhali nijifunze useremala kwani nikihitimu nitaweza kufanya kazi kwa uhakika na nitakuwa na ujuzi kichwani kuliko kuuza karanga ama kuhangaika kubeba zege.
Niliona ni wazo zuri sana, akanitafutia fundi mmoja maeneo ya Midizini.
Nilikuwa na kichwa chepesi cha kujifunza na kuelewa kwa haraka lakini nilichelewa kuondoka kwa yule fundi.
Kilichofanyika akaniondoa kwenye kundi la wanafunzi na kuwa fundi kama yeye, kwamba sasa niliweza kupata senti kidogo kwa ajili ya mahitaji yangu ya kimaisha.
Lakini baada ya mwaka mmoja niliamua kuachana na yule fundi na kwenda kufanya kazi zangu binafsi sehemu nyingine.
Pia, nilihama nyumbani kwa yule kaka wa rafiki yangu na kwenda kupanga chumba kimoja Magomeni.
Hapo ndipo nilipoanza kuandaa sehemu yangu ya kufanyia kazi mwenyewe.
Nikiwa na zana chache lakini nikajua muda si mrefu nitajikamilisha kila kitu.
Kazi nilizokuwa napokea zilikuwa ni za aina zote tu. Kutengeneza vitanda, makabati, meza, mpaka majeneza kwa wale waliokuwa wanahitaji.
Miezi mitano mbele bahati ilifunguka kwani niliweza kupata zana zote za kazi. Pia wateja walikuwa wanakuja kwa wingi wakitaka kutengenezewa vitu mbalimbali.
Lakini siku moja nikiwa sehemu yangu ya kazi, alinijia mzee mmoja wa jirani na sehemu hiyo na kuniambia;
Je, nini kitaendelea?
Sehemu ya 01.
Naitwa Abdul Mensah, ni mzaliwa wa Mabawa, Tanga mjini. Nilipomaliza shule ya msingi mwaka 1992 sikubahatika kuendelea na masomo ya sekondari hivyo nilikuja jijini Dar kwa lengo la kutafuta kazi ya kufanya. Kikubwa kilichonileta Dar ni kutokana na familia yetu kuwa fukara.
Hapa Dar nilifikia Manzese kwa kaka wa rafiki yangu niliyekuwa nimesoma naye shule ya msingi.
Kibaraua changu cha kwanza kukipata kilikuwa cha kuwa msaidizi wa fundi wa kujenga nyumba, kule Ubungo Kibangu. Nilifanya kazi hii kwa muda wa miezi miwili nikaona hainilipi, hivyo nikaacha na kuanza kuuza karanga. Pia nikaja acha mwezi mmoja mbele. Nikajitosa kwenye kujifunza kazi ya ufundi seremala.
Aliyenipa wazo hili ni kaka wa rafiki yangu ambaye alisema afadhali nijifunze useremala kwani nikihitimu nitaweza kufanya kazi kwa uhakika na nitakuwa na ujuzi kichwani kuliko kuuza karanga ama kuhangaika kubeba zege.
Niliona ni wazo zuri sana, akanitafutia fundi mmoja maeneo ya Midizini.
Nilikuwa na kichwa chepesi cha kujifunza na kuelewa kwa haraka lakini nilichelewa kuondoka kwa yule fundi.
Kilichofanyika akaniondoa kwenye kundi la wanafunzi na kuwa fundi kama yeye, kwamba sasa niliweza kupata senti kidogo kwa ajili ya mahitaji yangu ya kimaisha.
Lakini baada ya mwaka mmoja niliamua kuachana na yule fundi na kwenda kufanya kazi zangu binafsi sehemu nyingine.
Pia, nilihama nyumbani kwa yule kaka wa rafiki yangu na kwenda kupanga chumba kimoja Magomeni.
Hapo ndipo nilipoanza kuandaa sehemu yangu ya kufanyia kazi mwenyewe.
Nikiwa na zana chache lakini nikajua muda si mrefu nitajikamilisha kila kitu.
Kazi nilizokuwa napokea zilikuwa ni za aina zote tu. Kutengeneza vitanda, makabati, meza, mpaka majeneza kwa wale waliokuwa wanahitaji.
Miezi mitano mbele bahati ilifunguka kwani niliweza kupata zana zote za kazi. Pia wateja walikuwa wanakuja kwa wingi wakitaka kutengenezewa vitu mbalimbali.
Lakini siku moja nikiwa sehemu yangu ya kazi, alinijia mzee mmoja wa jirani na sehemu hiyo na kuniambia;
Je, nini kitaendelea?