Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 153,012
- 454,017
- Thread starter
- #81
Sehemu ya 55.
Nilitamani sana kumsimulia kila kitu mdogo wangu kuhusu mambo yaliyotokea siku hiyo japokuwa alikuwa anajua kuna mambo ya ajabu yalinitokea kwa kusimulia nilipofika nyumbani Tanga, lakini kila nilipofikiria jinsi ya kuanza ile sauti ya kunionya ilisikika akilini mwangu.
Usiku wa saa sita hivi, nikiwa bado nimelala nilishtuka ghafla lakini bila kujua ni kitu gani kilinishtua. Nilitupa macho moja kwa moja mlangoni na kukutana na maajabu mengine.
Jeneza nililolichonga kazini ambalo lilitakiwa kuchukuliwa kesho yake lilikuwa mlangoni likiwa halina mfuniko.
Nilishtuka sana na kukurupuka kutoka kitandani hadi kwenye kona ya chumba. Lakini kabla sijapiga kelele, sanduku lilitoweka machoni mwangu. Nilitupa macho kumwangalia mdogo wangu pale kitandani kama naye ameshtukia tukio lile. Ghafla nikaliona sanduku kitandani lilikuwa limelala palepale sehemu nilipokuwa nimelala mimi. Hilo nalo liliniogopesha sana.
"Hee! Hee!" nilipiga kelele bila kutarajia. Zilikuwa kelele za kuomba msaada kutoka kwa majirani. Pia kwa mdogo wangu ambaye naye licha ya kelele zangu hakuonesha hata dalili za kugeuka pale kitandani.
Ghafla niliacha kupiga kelele na kulikodolea macho jeneza. Safari hii lilikuwa na mfuniko wake juu.
Pembeni yake kulikuwa na kitu kama kamba nyeusi imelizunguka. Halafu pale pale nikaendelea kusikia ile sauti ikinionya vile vile kwamba, ili kuokoa maisha yangu sikuwa natakiwa kusema kwa mtu yeyote yule kuhusu yale mambo yaliyokuwa yakinitokea.
Nilipata wazo la kumfuata mdogo wangu pale pale kitandani ili nimwamshe na kumjulisha mambo yalivyo. Pia alione mwenyewe lile jeneza. Lakini je, ningemfikiaje wakati jeneza lilikuwa bado lipo kitandani?
Akili za haraka haraka ziliniambia nitoke nje na kwenda kumgongea jirani yangu ili aje aokoe jahazi. Nikiwa nimesimama mlangoni, sijaufungua, ile sauti, safari hii si kwamba ilinijia kwa kuhisi, bali ilisikika wazi wazi mle chumbani.
Nikasita kutoka. Nilibaki nimesimama nikiliangalia jeneza. Kwa jinsi nilivyoona mimi ilikuwa kama tunaangaliana na mtu ana kwa ana.
Je, nini kitaendelea?
Nilitamani sana kumsimulia kila kitu mdogo wangu kuhusu mambo yaliyotokea siku hiyo japokuwa alikuwa anajua kuna mambo ya ajabu yalinitokea kwa kusimulia nilipofika nyumbani Tanga, lakini kila nilipofikiria jinsi ya kuanza ile sauti ya kunionya ilisikika akilini mwangu.
Usiku wa saa sita hivi, nikiwa bado nimelala nilishtuka ghafla lakini bila kujua ni kitu gani kilinishtua. Nilitupa macho moja kwa moja mlangoni na kukutana na maajabu mengine.
Jeneza nililolichonga kazini ambalo lilitakiwa kuchukuliwa kesho yake lilikuwa mlangoni likiwa halina mfuniko.
Nilishtuka sana na kukurupuka kutoka kitandani hadi kwenye kona ya chumba. Lakini kabla sijapiga kelele, sanduku lilitoweka machoni mwangu. Nilitupa macho kumwangalia mdogo wangu pale kitandani kama naye ameshtukia tukio lile. Ghafla nikaliona sanduku kitandani lilikuwa limelala palepale sehemu nilipokuwa nimelala mimi. Hilo nalo liliniogopesha sana.
"Hee! Hee!" nilipiga kelele bila kutarajia. Zilikuwa kelele za kuomba msaada kutoka kwa majirani. Pia kwa mdogo wangu ambaye naye licha ya kelele zangu hakuonesha hata dalili za kugeuka pale kitandani.
Ghafla niliacha kupiga kelele na kulikodolea macho jeneza. Safari hii lilikuwa na mfuniko wake juu.
Pembeni yake kulikuwa na kitu kama kamba nyeusi imelizunguka. Halafu pale pale nikaendelea kusikia ile sauti ikinionya vile vile kwamba, ili kuokoa maisha yangu sikuwa natakiwa kusema kwa mtu yeyote yule kuhusu yale mambo yaliyokuwa yakinitokea.
Nilipata wazo la kumfuata mdogo wangu pale pale kitandani ili nimwamshe na kumjulisha mambo yalivyo. Pia alione mwenyewe lile jeneza. Lakini je, ningemfikiaje wakati jeneza lilikuwa bado lipo kitandani?
Akili za haraka haraka ziliniambia nitoke nje na kwenda kumgongea jirani yangu ili aje aokoe jahazi. Nikiwa nimesimama mlangoni, sijaufungua, ile sauti, safari hii si kwamba ilinijia kwa kuhisi, bali ilisikika wazi wazi mle chumbani.
Nikasita kutoka. Nilibaki nimesimama nikiliangalia jeneza. Kwa jinsi nilivyoona mimi ilikuwa kama tunaangaliana na mtu ana kwa ana.
Je, nini kitaendelea?