Kanungila Karim
JF-Expert Member
- Apr 29, 2016
- 20,746
- 25,662
BIASHARA YA KIFO 11
Huo ndiyo ulikuwa mwanzo wa biashara ya kifo waliyokuwa wameianza, kazi kubwa ya Ethan ilikuwa ni kutafuta wanawake na suala zima la kuwachuna ngozi kwa wale waliokataa kuigiza filamu za ngono zilikuwa chini ya watu wengine kabisa.
Akaanza kupata mafanikio makubwa, hakutaka kurudi kule alipotoka, yaani kufanya starehe mpaka kuishiwa kabisa, hapo, akaanza kujipanga kwa kufanya biashara nyingine, akaanza kufungua maduka ambayo yalianza kumuingizia kiasi fulani cha fedha.
Hakuacha kuwatafuta wanawake, ilikuwa ni kazi kubwa iliyokuwa na malipo makubwa pia, alikuwa akisafiri huku na kule na kuonana na wanawake wengi na mwisho wa siku kuwalaghai kwa maneno mengi, ahadi za kufanya kazi kwa malipo makubwa na mwisho wa siku kuwatumikisha katika filamu za ngono.
Mara baada ya kutembea sana barani Ulaya, hapo ndipo alipoanza safari za kuelekea barani Afrika na nchi ya kwanza kabisa iliyokuja akilini mwake ilikuwa Nigeria. Alijua ni kwa jinsi gani Waafrika wengi walivyokuwa wakihangaika kwa ajili ya kufika nchini Marekani au hata barani Ulaya tu, alijua ni kwa jinsi gani watu wa huko walivyokuwa wakihangaika, hivyo, kwa upande wake aliona kwamba kusingekuwa na ugumu wowote ule.
Mara baada ya kuteremka katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Murtala Muhammed uliokuwa jijini Lagos moja kwa moja akaanza kuelekea hotelini ambapo huko ndipo alipopanga kukutana na wasichana kwa ajili ya kufanya nao kazi za kugiza filamu za ngono pasipo kujua.
“Samahani,” alisema Ethan, alikuwa akimwambia mwanaume mmoja mara baada ya kukaa takribani wiki moja nchini humo.
“Bila samahani.”
“Ninahitaji wasichana kama kumi hivi.”
“Wa nini?”
“Ninahitaji kuzungumza nao, ila wawe wazuri ambao wanahitaji ajira ya kweli,” alisema Ethan, alikuwa akizungumza na mwanaume mmoja hotelini hapo.
“Hakuna tatizo! Kuna maslahi?”
“Hilo si tatizo.”
Kwa kijana yule, hiyo ikaonekana kuwa kazi ndogo mno. Kulikuwa na wanawake wengi nchini Nigeria ambao hawakuwa na kazi na walikuwa radhi kufanya kazi yoyote japokuwa walisoma sana na vyumbani walikuwa na vyeti vya chuo.
Alipoanza kuwatafuta, wala hakupata kazi kubwa, akafanikiwa kuwapata na kuwaambia kila kitu kilichokuwa kikiendelea na hivyo walitakiwa kuonana na huyo mtu hotelini kitu ambacho hakikuwa tatizo lolote lile, alipowakusanya, akaanza kuelekea nao hotelini huko.
“Vipi?”
“Wapo kumi, au unataka niongeze?’ aliuliza kijana yule.
“Hapana! Haohao wanatosha.”
“Sawa!”
Alichokifanya Ethan ni kutaka kuonana nao, wakaletwa chumbani mule na kuanza kuzungumza nao. Ethan alikuwa na uwezo mkubwa wa kuzungumza, alikuwa na uwezo wa kuziteka akili za mtu na kuzifanya alivyotaka yeye.
Alizungumza kipole, kwa umakini sana na uso wake aliuweka katika hali iliyowafanya wale wasichana kuona kwamba kweli mtu huyo alikuwa akihitaji wasichana kwa ajili ya kufanya kazi, alionekana kama mtu aliyekuwa na kiu ya kumsaidia mtu fulani.
“Kazi zipo, ila hotelini, malipo yake yanaanzia dola elfu moja kwa siku,” alisema Ethan maneno yaliyowafanya wasichana wale kushtuka.
“Dola elfu moja?”
“Ndiyo! Ni nyingi?”
“Ni nyingi mno!”
“Ni nyingi unapokuwa Afrika, unapokuwa Marekani, ni kiasi kidogo sana, tena inawezekana baada ya wiki mkalilia muongezwe mshahara,” alisema Ethan huku akichia tabasamu pana, wasichana wote wakacheka.
Kwa kumwangalia usingeweza kuamini kwamba alikuwa akijihusisha na kle kilichokuwa kikiendelea nyuma yake, alionekana kuwa kijana makini na mpole sana na aliaminika kutokana na jinsi alivyokuwa tu.
Wasichana wale wakatekwa, wakamwanmini Ethan na kuamini kila kitu alichokuwa akikizungumza, wakakubaliana naye kwamba walikuwa radhi kufanya kazi hiyo wakatakiwa kuwasiliana na wazazi wao au ndugu zao wakati yeye akifanya ishu zote za safari.
“Vipi?” aliuliza bwana Cook.
“Kuna Wanaigeria nimewapata, wazuriiii...”
“Haohao njoo nao.”
“Hakuna tatizo!’
Hiyo ndiyo ilikuwa kazi yake ya kila siku, alikuwa akizunguka huku na kule kwa ajili ya kazi hiyo tu. Aliendelea kulipwa vizuri, alijipatia kiasi kikubwa cha fedha kiasi kwamba kuna kipindi alihisi kwamba anaukaribia ubilionea.
Hakupata muda wa kupumzika, kila siku aliona kama muda umemtupa mkono hivyo alitakiwa kupambana kila siku mpaka kuhakikisha kwamba anafanikiwa na kuwa tajiri mkubwa maishani mwake.
Baada ya kuzunguka nchi nyingi za Afrika hapo ndipo alipoanza safari ya kwenda nchini Tanzania. Tayari alipewa taarifa kwamba huko kulikuwa na wanawake warembo, waliovutia mno na ambao hawakuwa na maisha mazuri kama walivyokuwa wanawake wengine barani Afrika.
Akatamani kwenda huko na kuianza safari hiyo. Alipofika ndani ya ndege, huku akiwa amevalia suti yake, macho yake yakatua kwa msichana mrembo mno, alipomwangalia, akatokea kumpenda lakini kwa kuwa alikuwa na kazi ya kufanya hasa na wasichana kama alivyokuwa msichana huyo, akataka kumuingiza katika biashara hiyohiyo.
“My name is Annabel,” (Ninaitwa Annabel) alijitambulisha msichana yule.
“Oooh! Annabel...myname is Ethan,” (Oooh! Annabel...jina langu ni Ethan,” alijitambulisha Ethan kwa msichana huyo.
Huo ndiyo ulikuwa mwanzo wa kufahamiana, walizungumza mengi huku wakionekana kama watu waliokwishaonana miaka miwili iliyopita. Kila mmoja alijitahidi kujifanya mchangamfu kwa mwenzake kitu kilichowafanya kutokuchokana kabisa.
Kichwani mwa Ethan kulifikiriwa vitu viwili tu, kumchukua msichana yule na kwenda kumchezesha filamu za ngono au kama angekataa basi angemchukua na kumpeleka kwa watu waliokuwa na kazi ya kuchuna ngozi tu.
Kwa muonekano wa sura, alikuwa binti mrembo mno zaidi ya wasichana ambao aliwahi kuwachukua kwa ajili ya kwenda nchini Mareani kwa lengo la kuigiza filamu za utupu. Kila alipomwangalia, hata yeye mwenyewe alihisi kumpenda ila kitu alichokisikitikia ni kwamba alikuwa akienda kuigiza filamu za utupu.
“Annabel...”
“Beee...”
“Hivi unajua kwamba wewe ni mrembo?”
“Hapana! Nipo kawaida!”
“Hakuna! Wewe ni mrembo mno, hivi umeuchukua kutoka wapi?”
“Kwa wazazi wangu!”
“Nimefurahi sana kukaa kiti kimoja nawe, hakika najisikia faraja.”
“Usijali,” alisema Annabel pasipo kujua lengo kubwa la kijana huyo ambaye aliendelea kumuonyeshea uchangamfu zaidi huku ikiwa njia mojawapo ya kufanya kumzoea ili hata kile alichokuwa amekipanga kiweze kufanikiwa.
Je nini kitaendelea?
Huo ndiyo ulikuwa mwanzo wa biashara ya kifo waliyokuwa wameianza, kazi kubwa ya Ethan ilikuwa ni kutafuta wanawake na suala zima la kuwachuna ngozi kwa wale waliokataa kuigiza filamu za ngono zilikuwa chini ya watu wengine kabisa.
Akaanza kupata mafanikio makubwa, hakutaka kurudi kule alipotoka, yaani kufanya starehe mpaka kuishiwa kabisa, hapo, akaanza kujipanga kwa kufanya biashara nyingine, akaanza kufungua maduka ambayo yalianza kumuingizia kiasi fulani cha fedha.
Hakuacha kuwatafuta wanawake, ilikuwa ni kazi kubwa iliyokuwa na malipo makubwa pia, alikuwa akisafiri huku na kule na kuonana na wanawake wengi na mwisho wa siku kuwalaghai kwa maneno mengi, ahadi za kufanya kazi kwa malipo makubwa na mwisho wa siku kuwatumikisha katika filamu za ngono.
Mara baada ya kutembea sana barani Ulaya, hapo ndipo alipoanza safari za kuelekea barani Afrika na nchi ya kwanza kabisa iliyokuja akilini mwake ilikuwa Nigeria. Alijua ni kwa jinsi gani Waafrika wengi walivyokuwa wakihangaika kwa ajili ya kufika nchini Marekani au hata barani Ulaya tu, alijua ni kwa jinsi gani watu wa huko walivyokuwa wakihangaika, hivyo, kwa upande wake aliona kwamba kusingekuwa na ugumu wowote ule.
Mara baada ya kuteremka katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Murtala Muhammed uliokuwa jijini Lagos moja kwa moja akaanza kuelekea hotelini ambapo huko ndipo alipopanga kukutana na wasichana kwa ajili ya kufanya nao kazi za kugiza filamu za ngono pasipo kujua.
“Samahani,” alisema Ethan, alikuwa akimwambia mwanaume mmoja mara baada ya kukaa takribani wiki moja nchini humo.
“Bila samahani.”
“Ninahitaji wasichana kama kumi hivi.”
“Wa nini?”
“Ninahitaji kuzungumza nao, ila wawe wazuri ambao wanahitaji ajira ya kweli,” alisema Ethan, alikuwa akizungumza na mwanaume mmoja hotelini hapo.
“Hakuna tatizo! Kuna maslahi?”
“Hilo si tatizo.”
Kwa kijana yule, hiyo ikaonekana kuwa kazi ndogo mno. Kulikuwa na wanawake wengi nchini Nigeria ambao hawakuwa na kazi na walikuwa radhi kufanya kazi yoyote japokuwa walisoma sana na vyumbani walikuwa na vyeti vya chuo.
Alipoanza kuwatafuta, wala hakupata kazi kubwa, akafanikiwa kuwapata na kuwaambia kila kitu kilichokuwa kikiendelea na hivyo walitakiwa kuonana na huyo mtu hotelini kitu ambacho hakikuwa tatizo lolote lile, alipowakusanya, akaanza kuelekea nao hotelini huko.
“Vipi?”
“Wapo kumi, au unataka niongeze?’ aliuliza kijana yule.
“Hapana! Haohao wanatosha.”
“Sawa!”
Alichokifanya Ethan ni kutaka kuonana nao, wakaletwa chumbani mule na kuanza kuzungumza nao. Ethan alikuwa na uwezo mkubwa wa kuzungumza, alikuwa na uwezo wa kuziteka akili za mtu na kuzifanya alivyotaka yeye.
Alizungumza kipole, kwa umakini sana na uso wake aliuweka katika hali iliyowafanya wale wasichana kuona kwamba kweli mtu huyo alikuwa akihitaji wasichana kwa ajili ya kufanya kazi, alionekana kama mtu aliyekuwa na kiu ya kumsaidia mtu fulani.
“Kazi zipo, ila hotelini, malipo yake yanaanzia dola elfu moja kwa siku,” alisema Ethan maneno yaliyowafanya wasichana wale kushtuka.
“Dola elfu moja?”
“Ndiyo! Ni nyingi?”
“Ni nyingi mno!”
“Ni nyingi unapokuwa Afrika, unapokuwa Marekani, ni kiasi kidogo sana, tena inawezekana baada ya wiki mkalilia muongezwe mshahara,” alisema Ethan huku akichia tabasamu pana, wasichana wote wakacheka.
Kwa kumwangalia usingeweza kuamini kwamba alikuwa akijihusisha na kle kilichokuwa kikiendelea nyuma yake, alionekana kuwa kijana makini na mpole sana na aliaminika kutokana na jinsi alivyokuwa tu.
Wasichana wale wakatekwa, wakamwanmini Ethan na kuamini kila kitu alichokuwa akikizungumza, wakakubaliana naye kwamba walikuwa radhi kufanya kazi hiyo wakatakiwa kuwasiliana na wazazi wao au ndugu zao wakati yeye akifanya ishu zote za safari.
“Vipi?” aliuliza bwana Cook.
“Kuna Wanaigeria nimewapata, wazuriiii...”
“Haohao njoo nao.”
“Hakuna tatizo!’
Hiyo ndiyo ilikuwa kazi yake ya kila siku, alikuwa akizunguka huku na kule kwa ajili ya kazi hiyo tu. Aliendelea kulipwa vizuri, alijipatia kiasi kikubwa cha fedha kiasi kwamba kuna kipindi alihisi kwamba anaukaribia ubilionea.
Hakupata muda wa kupumzika, kila siku aliona kama muda umemtupa mkono hivyo alitakiwa kupambana kila siku mpaka kuhakikisha kwamba anafanikiwa na kuwa tajiri mkubwa maishani mwake.
Baada ya kuzunguka nchi nyingi za Afrika hapo ndipo alipoanza safari ya kwenda nchini Tanzania. Tayari alipewa taarifa kwamba huko kulikuwa na wanawake warembo, waliovutia mno na ambao hawakuwa na maisha mazuri kama walivyokuwa wanawake wengine barani Afrika.
Akatamani kwenda huko na kuianza safari hiyo. Alipofika ndani ya ndege, huku akiwa amevalia suti yake, macho yake yakatua kwa msichana mrembo mno, alipomwangalia, akatokea kumpenda lakini kwa kuwa alikuwa na kazi ya kufanya hasa na wasichana kama alivyokuwa msichana huyo, akataka kumuingiza katika biashara hiyohiyo.
“My name is Annabel,” (Ninaitwa Annabel) alijitambulisha msichana yule.
“Oooh! Annabel...myname is Ethan,” (Oooh! Annabel...jina langu ni Ethan,” alijitambulisha Ethan kwa msichana huyo.
Huo ndiyo ulikuwa mwanzo wa kufahamiana, walizungumza mengi huku wakionekana kama watu waliokwishaonana miaka miwili iliyopita. Kila mmoja alijitahidi kujifanya mchangamfu kwa mwenzake kitu kilichowafanya kutokuchokana kabisa.
Kichwani mwa Ethan kulifikiriwa vitu viwili tu, kumchukua msichana yule na kwenda kumchezesha filamu za ngono au kama angekataa basi angemchukua na kumpeleka kwa watu waliokuwa na kazi ya kuchuna ngozi tu.
Kwa muonekano wa sura, alikuwa binti mrembo mno zaidi ya wasichana ambao aliwahi kuwachukua kwa ajili ya kwenda nchini Mareani kwa lengo la kuigiza filamu za utupu. Kila alipomwangalia, hata yeye mwenyewe alihisi kumpenda ila kitu alichokisikitikia ni kwamba alikuwa akienda kuigiza filamu za utupu.
“Annabel...”
“Beee...”
“Hivi unajua kwamba wewe ni mrembo?”
“Hapana! Nipo kawaida!”
“Hakuna! Wewe ni mrembo mno, hivi umeuchukua kutoka wapi?”
“Kwa wazazi wangu!”
“Nimefurahi sana kukaa kiti kimoja nawe, hakika najisikia faraja.”
“Usijali,” alisema Annabel pasipo kujua lengo kubwa la kijana huyo ambaye aliendelea kumuonyeshea uchangamfu zaidi huku ikiwa njia mojawapo ya kufanya kumzoea ili hata kile alichokuwa amekipanga kiweze kufanikiwa.
Je nini kitaendelea?