Simulizi:Biashara Ya Kifo

Simulizi:Biashara Ya Kifo

Sehemu ya 22

“Vipi?”
“Tayari! Jiandae, yafunge maboksi hayo vizuri, kuna boti itakuja upande wa huku, tutatakiwa kutoka kisha kuingia botini,” alisema Ethan.

Upande wa pili, Thorn na wenzake walikuwa wakiendelea kuimba na kupiga kelele, walikuwa wamekunywa mno na walionekana kuzidiwa na ulevi, muda wote, mizinga ya pombe kali ilikuwa mikononi mwao, nyimbo walizoimba, hazikueleweka kabisa.

Hakukuwa na wafanyakazi waliokuwa wakiwafahamu wale walikuwa wakina nani, kadiri walivyoendelea kuwa ndani ya meli ile walizidi kuwa na maswali zaidi, hawakuonekana kuwa watu wazuri hata mara moja kutokana na yale waliyokuwa wakiyafanya.

Baada ya dakika kama kumi, ghafla wakaanza kuhisi kwamba meli ile ilianza kuzama. Wafanyakazi wote wakashtuka, hawakuwa na uhakika juu ya kile walichokuwa wamekihisi, walichokifanya ni kwenda kwenye vyumba vyote kuangalia.

Walipokuwa wakielekea katika chumba kile, ghafla wakaona maji mengi yakitoka kutokea mlangoni na walipoufungua mlango tu, chumba kizima kilikuwa kimejaa maji, hivyo kitendo cha kuufungua tu, maji yakawa kama yameruhusiwa.

Kila mtu alichanganyikiwa, maji yaliendelea kuingia na kadiri muda ulivyozidi kwenda mbele na ndivyo meli ile ilivyoendelea kuzama. Kila mmoja akaanza kuhangaika huku na kule, walikuwa wamefika mbali mno na nchi kavu hakukuonekana, walikuwa wakiukaribia mpaka wa bahari mbili za Indi na Atlantiki.

“Chukueni maboya,” alisema nahodha huku akionekana kuchanganyikiwa, giza lilikuwa limetanda kila kona.

Kilichofanyika, wafanyakazi wakachukua maboya, kijana yule ambaye alikuwa amekwishafanya mipango na Ethan, akachukua boti iliyokuwa imefungwa nyuma ya meli ile, akaifungua kamba, ikaelekea baharini, hapohapo hakutaka kuchelewa, alichokifanya ni kujirusha majini na kuanza kupiga mbizi kuifuata boti ile, alipoifikia, akaipanda, akaiwasha na kuelekea katika upande ule aliokuwepo Ethan na Annabel ambapo napo chumba chao kilianza kujaa maji, maboksi yale matano yaliyojaa hela yalianza kuelea.
*****
Hawakutaka kupoteza muda, tayari meli ile ilianza kuzama hivyo ilimaanisha kwamba kama wasingefanya haraka kutoka, nao wangeweza kufa.

Alichokifanya Ethan ni kuchuka yale maboksi matano yaliyojaa hela huku akisaidiana na Annabel na kuanza kutoka nje.

Hayakuwa maboksi makubwa sana, na wala hayakuwa mazito sana. Walipotoka nje, tayari meli ililala upande mmoja, maji yalijaa na kadiri muda ulivyokuwa ukizidi kwenda mbele na ndivyo ambavyo maji yalizidi na meli kuendelea kuzama zaidi.

Hakukuwa na mwanga wa taa yoyote ile, maji yaliingia katika mtambo wa umeme uliokuwa chini na umeme kuzima. Walikuwa wakipishana na wafanyakazi ambao wote hao walikuwa kwenye harakati za kuyaokoa maisha yao.

Huku wakiwa na maboksi yao, wakaelekea katika upande ambao walikubaliana na kijana yule kwamba wangeonana, kuangalia kule baharini, wakaiona boti kwa mbali ikielea, bila wasiwasi wakajua kwamba huyo ndiye alikuwa yule kijana ambaye mpaka muda huo hawakujua aliitwa nani.

Walichokifanya, kitu cha kwanza kabisa kilikuwa ni kuyatupa mabegi yale baharini, walitaka wayatangulize hayo na ndipo nao wafuate. Walipoyatupa yote na kuyaona yakielea, Ethan akamgeukia Annabel.
“We have to jump,” (tunatakiwa turuke) alisema Ethan.

“What?” (Unasemaje?)
“We have to jump right now,” (Ni lazima turuke sasa hivi) alisema Ethan.

“I am afraid,” (Naogopa)
“What are you afraid of?” (Unaogopa nini?)
“Pleasee! I can’t jump,” (Tafadhali! Siwezi kuruka) alisema Annabel huku akionekana kuogopa.

Maji yalizidi kujaa, watu waliendelea kukimbia huku na kule kuyaokoa maisha yao, wale waliokuwa na maboya, tayari wakaanza kujirusha baharini kwani kwa namna moja au nyingine walikwishajua kwamba meli ile ilikuwa ni lazima izame.

Alichokifanya Ethan ni kuanza kumbembeleza Annabel kwamba asingeweza kufa japokuwa maji yalionekana kuwa mbali. Alizungumza naye, walipokubaliana, akamshika mkono na kumwambia sasa ulikuwa wakati wa kuruka.

“Jump.....” (Ruka...) alisema Ethan huku akimshika Annabel mikono kisha kujitupa ndani ya maji.
 
Sehemu ya 23

Meli ile iliendelea kuzama, walichokifanya mara baada ya kutumbukia majini ni kuanza kupiga mbizi kuyafuata maboksi yale. Hicho ndicho kilichokuwa kitu cha muhimu kuliko vyote, walipoyafikia, wakaanza kuyavuta na kuyapeleka katika boti iliyokuwa ikiwasubiria.

“Vipi tena? Mbona maboksi tena?” aliuliza kijana yule huku akionekana kushangaa.

“Wewe twende,” alisema Ethan.
“Ila uzito unaweza kuwa mkubwa.”
“Usijali, wewe twende kwanza, kama mzigo utakuwa mkubwa, tutapunguza,” alisema Ethan.

Hakuwa na jinsi, alichokifanya kijana yule ni kuwasha injini na kisha kuondoka mahali hapo. Ethan akatabasamu kwa mara ya kwanza tangu apate taarifa kwamba Annabel alikuwa ametekwa na watu wasiojulikana.

Uso wake ukawa na tumaini jipya, akajiona shujaa kuliko watu wote duniani. Boti ile iliendelea kwenda mbele, kila mtu alikuwa kimya. Annabel alikuwa amejikunyata, alihisi baridi kali mwilini mwake.

Alichokifanya Ethan ni kumsogelea kisha kumkumbatia vilivyo ili aweze kupunguza baridi lililokuwa likimpiga. Kijana yule bado alikuwa na maswali mengi kichwani mwake kuhusu yale maboksi yaliyokuwa mule ndani ya boti. Alitamani kuuliza lakini akabaki kimya kwa kuona kwamba angepewa jibu kama lile alilopewa mwanzo.

“Unaitwa nani rafiki yangu?’ aliuliza Ethan, kwa mbali walikuwa wakiziona taa za Mji wa Nangame.

“Naitwa Michael Johnson.”
“Sawa! Tunahitaji ututunzie siri, usimwambie mtu yeyote juu ya kilichotokea,” alisema Ethan.
“Usijali! ! Haya ni maboksi ya nini?”
“Tunataka kukufanya uwe tajiri!”
“Kivipi?”

“Tunataka kukupa dola milioni tano.”
“Unasemaje? Acha masihara.”
“Ndiyo hivyo! Upo tayari?”
“Kuna mtu anayekataa fedha? Nipo tayari,” alijibu Michael.

“Sawa! Tufike nchi kavu, kisha tunza hii siri, ikiwezekana, hakikisha bwana Cook hakuoni sehemu yoyote ile, kama akikuona, jua kwamba atakuua,” alisema Ethan.

“Ataniua?”
“Ndiyo! Ni lazima ujifiche huku ukila maisha.”
“Nitafanya hivyo!”

Ethan alimtaka Michael kuficha siri juu ya kile kilichokuwa kimetokea na ndiyo maana alimuahidi kumpa kiasi kikubwa cha fedha, kiasi ambacho hata Michael angefanya kazi mpaka anakufa asingeweza kukipata, kwa kifupi ni kwamba alitaka kumfanya milionea.

Kuhusu fedha, mpaka muda huo hakuwa na tatizo lolote lile, kila boksi moja katika maboksi yale matano kulikuwa na dola milioni tano kwa maana hiyo maboksi yote yalikuwa na dola milioni ishirini na tano, zaidi ya bilioni hamsini kwa fedha za Kitanzania.

Walizidi kwenda mbele mpaka walipofika nchi kavu ambapo wakaegesha ile boti na kisha kuanza kuangalia huku na kule.

Hawakujiona kama walikuwa salama, waliifahamu Afrika Kusini, haikuwa nchi ya amani, kulikuwa na vijana wengi wa kihuni ambao kazi zao zilikuwa ni kuwaibia wageni waliokuwa wakija nchini humo.
Walichokifanya ni kubeba maboksi yale na kisha kuanza kuondoka nayo.

Mpaka muda huo bado Michael hakujua ndani ya maboksi yale kulikuwa na nini na hakujua kwa nini alipewa boksi moja abebe maboksi manne yaliyobakia waliyabeba wao wenyewe.

Walipofika barabarani tena huku wakiwa salama, wakasimamisha teksi na kutaka kupelekwa katika hoteli moja kubwa na ya kifahari, hawakuhofia kuhusu gharama.

Hawakuchukua muda mrefu wakafika katika Hoteli ya Crystal Palace iliyokuwa katikati ya jiji hilo ambapo wakateremka na maboksi yao na kuanza kuelekea ndani.

“Can we help you sir?” (Tunaweza kukusaidia mkuu?) aliuliza mhudumu mmoja, alikuja na mwenzake, walitaka kuwasaidia maboksi yale.

“Never mind! Thank you,” (Msijali! Asanteni) alisema Ethan na kuelekea ndani.

Kitu cha kwanza kabisa mara baada ya kufika ndani ya hoteli hiyo pale mapokezi wakataka kuonana na meneja mkuu, walikuwa na mazungumzo naye. Mhudumu mmoja akaondoka na kwenda ofisini kwa huyo meneja na kumuita.

“Niwasaidie nini?”
“Tunahitaji ulinzi kwa siku ya leo,” alisema Ethan.

“Ulinzi wa namna gani?”
“Ulinzi kotekote! Tumekuwa tukitafutwa sana, tunahitaji ulinzi wa kutosha.”
“Mshachukua vyumba?”
“Hapana!”

“Chukueni vyumba vya wafanyabiashara, vina ulinzi wa kutosha na vipo ardhini,” alisema meneja yule.
“Kiasi gani?”
“Randi laki tano.”

“Asante,” alisema Ethan na kisha kuchukua vyumba viwili huku akimtaka Michael ampe lile boksi na angemwambia mengi kuhusu maboksi hayo ifikapo asubuhi, Michael akakubaliana naye na kwenda kulala kwenye chumba cha gharama.
****
 
Sehemu ya 24

Bwana Cook alipewa taarifa kwamba kile alichokuwa amewaagiza vijana wake tayari kilifanyika na hivyo walikuwa wakijiandaa kwa afari ya kurudi nchini Marekani.

Moyo wake ulifurahi mno kusikia kwamba mntu aliyekuwa akimhitaji sana, Ethan alikuwa amekamatwa na hivyo kurudishwa nchini Marekani na kukabidhiwa mikononi mwake.

Kila wakati uso wake ulijawa na tabasamu pana, alifurahi mno na kuona vijana wake walikuwa siriazi na kazi, hivyo kuahidi kuwalipa zaidi ya kile alichokuwa amewalipa.

Alimchukia mno Ethan, hakumpenda hata mara moja, alimfanya kupata hasara, hakuingiza fedha kama ilivyotakiwa, yaani biashara yake ilidorora kabisa.

Huo ulikuwa ni muda wa kunywa mvinyo, ulikuwa ni muda wa kucheza na kurukaruka tu, kitendo cha Ethan kuwa njiani akiletwa kilimpa furaha kubwa ajabu.

Meli ya mizigo ambayo ndiyo aliyoagiza imbebe Ethan, kulikuwa na fedha zake za biashara zilizokuwa zikifanyika barani Afrika na Asia, kiasi cha dola milioni ishirini na tano ambacho kidogo kingemfanya kujisikia faraja juu ya hasara aliyokuwa ameipata baada ya Ethan kumkacha kufanya kazi.
“Mmefikia wapi?” aliwasiliana na vijana wake.

“Msumbiji.”
“Safi sana.”
Mbali na kuambiwa hivyo pia aliambiwa kwamba walimpata Ethan na msichana ambaye alimsababishia kutokufanya kazi yake.

Bwana Cook hakutaka Annabel auawe kwani hakuwa akihusika, alitaka msichana huyo aachwe huru lakini alipofikiria kwamba endapo angeachwa ni lazima angetoa taarifa polis, akawaagiza waondoke naye, na kama kumuua wasimuue hapo Tanzania na hivyo kuweka mikakati kwamba ilikuwa ni lazima kumuua katika makutano ya Bahari ya Indi na Atlantiki kwani hata mwili wake usingeonekana kabisa.

Alicheza na simu tu, kila wakati ilikuwa ni lazima kuwasiliana nao na kujua wapi walikuwa wamefiia. Baada ya kukaa kwa muda wa siku tano na ndipo alipoamua kuwapigia tena, kitu cha ajabu kilichomshangaza ni kwamba simu haikupatikana.

Hiyo haikuwa kawaida lakini hakutaka kuwa na wasiwasi kwani aliamini kwa sababu walikuwa baharini, kutokuwa na netwoki lilikuwa suala la kawaida. Masaa yaliendelea kukatika, siku zikaenda mbele na kila alipojaribu kuwapigia simu, bado hali ilikuwa ileile kwamba simu haikupatikana.

“Kuna nini kimetokea? Au wamekimbia na meli yangu?’ alijiuliza lakini akakosa jibu.
Hakuwa na raha tena, kitendo cha kuwakosa vijana wake simuni kilimuhuzunisha mno, aliendelea kuvumilia kwa kuamini labda kungekuwa na siku ambayo angeweza kupatya mawasiliano nao lakini hali ilikuwa ileile.

Hakutaka kukaa nchini Marekani, akili yake haikumpa kabisa kuendelea kuishi huko, alichokifanya ni kuondoka na kuelekea Afrika Kusini ili aende kufuatilia na kujua ni kitu gani kilikuwa kimetokea.

Alipofika huko, hata kabla hajauliza kitu chochote kile, taarifa za kuzama kwa meli zilianza kusikika katika kila kona nchini humo. Hakutaka kupitwa na lolote lile, alichokifanya ni kwenda mpaka bandarini ambapo huko akakutana na taarifa zilizosema kwamba kulikuwa na meli ya mizigo ilikuwa imezama.

“Ilikuwaje?” aliuliza huku akionekana kuchanganyikiwa, hakumfikiria Ethan wala mtu yeyote, alichokifikiria yeye ni fedha zake tu.
“Hatujui, ila meli ilizama usiku, mnara ulionyesha signo.”

“Kuna watu wamekwenda?”
“Ndiyo! Walikwenda wakati meli inazama, bahati mbaya wote wamekufa, hakuna aliyenusurika,” alisema mtu aliyehusika na kuuongoza mnara wa baharini.

“Lakini si kulikuwa na maboya?”
“Ndiyo! Ila kilichowaua ni baridi kali, hawakupata msaada kwa muda mrefu, meli ilizama saa tatu usiku, sisi pale tulikwenda saa kumi alfajiri,” alisema mzee huyo.

Maneno hayo yalimchanganya mno, hakuamini kama meli yake ya mizigo ilikuwa imezama, tena ilizama na fedha zake za biashara. Alihisi kuchanganyikiwa, hakuamini kile alichokuwa akiambiwa. Wakati mwingine alihisi kama alikuwa ndotoni na muda mfupi baadaye angeshtuka kutoka usingizini.

Ukweli haukubadilika, uliendelea kuwa vilevile kwamba meli yake ilizama na fedha zote zilipotea. Hakutaka kukubali, alichokitaka kwa wakati huo ni kuifahamu sehemu ambayo meli iliyo ilipozamia ili ajue ni wapi angeanzia kuzipata fedha zake.

Hilo halikuwa tatizo, akalipia kiasi alichokitka na kwenda huk ambapo meli ilipozama. Walipofika katika eneo husika, akaonyeshewa na kuwaagiza vijana wazame ili kwenda kuangalia huko ndani ya meli kama wangefanikiwa kuyaona maboksi.

Vijana watatu waliovalia mavazi ya kuogelea tena huku wakiwa na mitungi ya gesi migongoni mwao wakazama majini na kwenda chini kabisa.

Meli waliikuta, ilishiliwa na tope zito, haikuweza kutoka hata mara moja, walichokifanya ni kuanza kuingia katika sehemu moja hadi nyingine, hawakukuta kitu chochote kile.
“Mnasemaje?”
“Hatukukuta kitu chochote kile.”

“Kweli?”
“Ndiyo mzee!”
“Hata maboksi?”
“Hapana! Hatukukuta.”
Alichanganyikiwa mno, maboksi yale yalikuwa muhimu mno kwake, hakuamini kile alichoambiwa hivyo kutaka kuiona miili ya watu waliofariki dunia.

Wakaondoka hapo na kwenda hospitali ambapo bado miili ilikuwa imehifadhiwa.
Alipofika huko, akaonyeshewa miili yote isipouwa miili ya watu wanne tu, Ethan na vijana ambao aliwatuma kwenda kumteka kijana huyo ili wampeleke nchini Marekani.

“Wengine wapo wapi?” aliuliza bwana Cook.
 
Sehemu ya 25

“Wengine wakina nani?”
“Kuna vijana wanne nawahitaji,” alijibu mzee huyo.

“Mzee! Hizi ni maiti tulizozikuta zikielea huku zikiwa na maboya, inawezekana hizo unazoziulizia ni miongoni mwa zile zilizokwama kwenye tope, zilie zilizoliwa sana na samaki,” alisema jamaa mmoja.
“Kuna nyingine zimebaki?”

“Ndiyo! Zipo kama sita hivi, zimeliwa sana na samaki, zimeharibika sana na zimekwamba kwenye tope,” alisema jamaa huyo.

“Hamuwezi kuzitoa kweli?”
“Ni kazi ngumu sana, maiti za hivyo huwa zinaachwa,” alisema jamaa huyo.
“Kwa hiyo ndani ya meli hamkukuta maboksi?”

“Maboksi gani tena mzee?”
“Maboksi fulani hivi!”
“Ila mizigo ilikuwa mingi.”
“Jamani! Kweli hamjayaona maboksi?”
“Hata kama yalikuwepo kutyaona ni vigumu, mizigo ilikuwa mingi,” alisema jamaa huyo.

Bwana Cook alichanganyikiwa, hakuamini kama kweli fedha zake alizoagiza ziwekwe kwenye maboksi zilikuwa zimepotea, moyo wake ulimuuma mno ila hakuwa na jinsi. Maiti zile alizokuwa ameambiwa kwamba zilikwamba kwenye tope na kuliwa na samani, aliamini kwamba Ethan alikuwa mmoja wao.

Akawa mtyu wa kuomboleza kila siku, kila kitu kilichotokea kwake kiliacha historia yenye maumivu makubwa. Pamoja na maumivu hayo lakini alishukuru kwani yule Ethan, kija aliyemrudisha nyuma naye alikuwa amekufa maji.

“Sawa! Nashukuru Mungu kwa kila kitu, ila kifo cha Ethan, hakika kimenifariji,” alisema bwana Cook huku akiwa hajui kama mtu aliyemzungumzia alikuwa hai na ndiye aliyekuwa na fedha zake.
*****
Wakayafungua maboksi yale, walichokiona ndicho kilekile walichohisi, maboksi yote hayo yalikuwa na fedha nyingi huku kila boksi likiwa limeandikwa $5 Milion yaani Dola milioni tano. Mioyo yao ilifarijika mno, furaha ambayo ilipotea ikarudi tena na kujiona wakiwa matajiri.

Usiku huo hawakulala, walikuwa macho huku wakipongezana. Ilipofika asubuhi, wakamuita Michael na kumwambia kwamba wanampa fedha kwa kuwa alionyesha ujasiri wa kuwasaidia kwani bilala yeye hakika wangeuawa.

Michael hakuamini kama kiasi kile cha fedha alikabidhiwa yeye, alifurahi mno. Akawashukuru na huo ndiyo ukawa mwisho wa kuoana nao, alichoambiwa ni kwamba alitakiw kujificha kwani kwa namna moja au nyingine bwana Cook angefikiri kwamba wote walikufa baharini, na hivyo ndivyo ilivyokuwa.

Baada ya kukaa Afrika Kusini kwa siku mbili ndipo walipoamua kurudi nchini Tanzania huku wakiwa wameziweka zile fedha katika akaunti zao.

Walipofika nchini Tanzania, askofu Benedicto alichanganyikiwa na furaha, hakutaka kuamini kama kweli binti yake alikuwa amerudi salama nchini Tanzania
 
Sehemu ya 26

“Ila ninakuchukia Ethan,” alimwambia Ethan.

“Baba! Hautakiwi kumchukia Ethan bali unatakiwa kumshukuru,” alisema Annabel.
“Nimshukuru kwa lipi?”

“Kuniokoa, bila yeye ningekwishakufa.”
Irakoza hakuamini, muda wote alipokuwa akimwangalia binti yake alibaki akimkumbatia tu.

Kwake, kumuona tena binti yake ulionekana kuwa kama muujiza fulani hivi, hakuamini hata mara moja.
Kama alivyokuwa amempata, hakutaka kumpoteza tena, aliamua kuwa naye, aliamua kumshikilia vilivyo ili asije kupotea tena kama ilivyokuwa.

Huku furaha hiyo ikiendelea na ndipo Askofu Benedicto akaamua kumwambia ukweli binti yake kwamba alikuwa nani na ilikuwaje mpaka kuwa na mama yake.

“Wewe ni padri?” aliuliza Annabel.
“Si padri, mimi ni mkuu wa mapadri wote Tanzania, Kardninari Benedicto,” alijibu askofu huyo.
“Baba!” aliita Annabel huku akionekana kutokuamini.

“Ndiyo hivyo binti yangu! Tumekuwa tukiishi katika siri hii kwa kipindi kirefu, siwezi kuendelea kuishi hivi, ni lazima nikae na familia yangu,” alisema Benedicto.

“Kwa hiyo?”
“Nitatangaza wazi kuachana na hii kazi, sityotaka tena kuendelea kuwa kardinari,” alisema Benedicto.
“Baba! Kwa nini ufanye hivyo?”
“Ninataka kuishi nanyi kwa amani, hakuna kingine,” alisema Benedicto.

Maneno aliyoongea ndiyo aliyomaanisha, hakutaka kuishi kisiri kama alivyofanya, alitaka kuishi na familia yake kwa amani hivyo kitendo cha kuitangazia dunia kwamba alikuwa na mtopto wa nje na kuamua kuachana na upadri kingemfanya kujisikia amani moyoni mwake.

Hakutaka kupokea ushauri kutoka kwa mtu yeyote yule, kile alichokuwa amekiamua ndicho alichoona kuwa bora kukifanya mahali hapo. Alichokifanya ni kunyanyua mkonga wa simu na kuwapigia viongozi wengine wa dini, wakutane sehemu na kuwaambia juu ya uamuzi wake.
 
Sehemu ya 27

Lilikuwa jambo gumu mno, aliamini kwamba angekwenda kulichfua kanisa, hakutaka kujali, alichokuwa akikitaka mahali hapo ni uhuru wa kuishi na familia yake tu.
****

Mapadri walikusanyika katika ukumbi uliokuwa katika Kanisa kubwa lililokuwa Posta jijini Dar es Salaam.

Mapadri wote walikusanyika mahali hapo kwa ajili ya kumsikiliza mkuu wao aliyekuwa amewaita kwa kuwa kulikuwa na jambo kubwa alilotaka kuwaambia.

Kila mmoja alikuwa na maswali kichwani mwake, hakukuwa na aliyeelewa kile alichotaka kuambiwa, walichokifanya ni kuwa makini na kusikiliza kwa makini.

Mpaka muda huo Askofu Benedicto alikuwa ndani ya ofisi iliyokuwa pembeni ya ukumbi huo wa kanisa, alikuwa akisali, muda wote huo machozi yalikuwa yakimtoka, hakuamini kile alichokuwa akienda kukifanya, hakutegemea hata siku moja kama angefanya kile alichotaka kukifanya.

Familia yake ilikuwa muhimu zaidi, aliipenda zaidi ya kitu chochote, hakutaka kukaa nayo mbali, kwake, familia hiyo ilikuwa kila kitu. Hakutaka kujificha, alitaka kila mtu ajue kile kilichokuwa kikiendelea, hakutaka kuishi maisha ya kujificha tena.

Baada ya saa moja, akatoka ofisini mule, macho yake yalikuwa mekundu sababu ya kulia sana, moyo wake uliumia lakini hakuwa na jinsi. Katika maisha yake alijifunza kwamba wakati mwingine mtu unatakiwa kuweka maamuzi magumu pasipo kujali ni muda gani na wapi.

Alipowaona mapadri waliokuwa wamekusanyika, uso wake ukaongezeka kuwa na majonzi zaidi, kila alipowaangalia, moyo wake uliumia sana kwani hiyo ndiyo ilikuwa nafasi ya mwisho kuonana nao katika masuala yote yaliyokuwa ya kidini.

“Tumsifu Yesu Kristo,” aliwasalimia.
“Milele amina!” wakaitikia, akakaa kitini.
Kila mmoja akabaki kimya, mkuu wao alionekana kuwa na jambo zito alilotaka kuwaambia mahali hapo, wote walibaki kimya, walikuwa wakimsikiliza juu ya kile alichotaka kukizungumza.

Alichokifanya Askofu ni kukohoa na kuchukua karatasi iliyokuwa katika meza na kisha kuiweka vizuri kwa ajili ya kuisoma.

“Ninataka kujiuzulu,” alisema askofu Benedicto.

Kila mmoja aliyesikia hilo akashtuka, hawakuamini kile walichokuwa wamekisikia, wengine wakajiuliza kama walisikia vizuri au walisikia vibaya. Wakayategesha masikio yao vizuri, alichokifanya Askofu Benedicto ni kuirudia sentensi yake.

“Ninataka kujiuzulu, na hilo linafanyika leo, tena sasa hivi,” alisema Askofu Benedicto.

“Askofu....” aliita padri mmoja.
“Hivyo ndivyo ninavyotaka, ninajiuzulu nyadhifa hii, na barua nimekwishaiandika kwenda Vatican,” alisema askofu Benedicto.

Aliongea kimasihara, wengi wakahisi kwamba alidanganya lakini kile alichokuwa akikizungumza kilikuwa kweli kabisa.

Hakutaka kuficha, akawaambia kile kilichokuwa kikiendelea katika maisha yake kwamba alitaka kuishi na familia yake.
“Kumbe una mtoto?” aliuliza askofu mmoja.
 
Sehemu ya 28

“Kumbe una mtoto?” aliuliza askofu mmoja.

“Ndiyo! Najua nimemtenda Mungu wangu dhambi, ila ninaomba Mungu anisamehe,” alisema askofu Benedicto.

Huo ndiyo ulikuwa ukweli wenyewe, na haukubadilika, alipomaliza kusema maneno hayo, machozi yakaanza kumbubujika, akasimama na kuondoka zake.

Mapadri wote wakabaki katika chumba kile, walikuwa wakiulizana, kila mtu aliongea lake lakini ukweli uleule aliokuwa ameuzungumza ndiyo ulikuwa wenyewe, aliachia madaraka kwa kuwa tu alikuwa akifanya dhambi ya uzinzi.

Aibu kubwa ilionekana kuliogelea kanisa, hakukuwa na aliyeamini. Kwa kuwa lilikuwa ni jambo kubwa ambalo kanisa lilitakiwa kuambiwa, likatangazwa makanisani na hata kwenye vyombo vya habari.

Kila mtu aliyesikia hakuamini, kiongozi mkubwa, aliyeaminika, aliyeheshimika Tanzania nzima, leo hii alitangaza kujiuzulu tena kwa kashifa ya kuzaa mtoto kitu ambacho hakutakiwa kuwa nacho.
“Haiwezekani,” alisikika mwanamke mmoja.

“Jamani mwenzenu wala siamini,” alisema mwanamke mwingine.
“Kweli mwanaume mzuri si wa kumuamini,” aliingilia mwingine.

Baada ya wiki moja, Askofu Benedicto akaitwa Vatican ambapo huko alitakiwa kusimulia kilichokuwa kimetokea, hakuficha, alikuwa muwazi kwa kila kitu, alieleza vitu vyote vilivyotokea katika maisha yake.

Uongozi wa kanisa hilo kubwa duniani halikuwa na jinsi zaidi ya kumuondoa katika uongozi wa kanisa hilo nchini Tanzania na nafasi yake kuchukuliwa na mtu mwingine.

Watu walilizungumzia sana lakini hakujali, maneno ya watu, kashfa za watu hazikuwa zaidi ya furaha aliyokuwa nayo kuwa karibu na familia yake.

Baada ya miezi miwili, akiwa kama baba, akamfungisha ndoa binti yake, Annabel akaolewa na Ethan harusi iliyotangazwa sana kwani tayari umaarufu wa Benedicto ulikuwa mkubwa zaidi.

“Nilikuwa radhi kwa kila kitu, hakika uamuzi nilioufanya ulikuwa sahihi,” alisema Benedicto huku akionekana kuwa na furaha tele.

Kila kitu kilichotokea katika maisha yake kilibaki kubwa historia. Kwa bwana Cook, hakumtafuta tena Ethan, hakumfuatilia kwa kuwa alijua kwamba mwanaume huyo alikuwa amekufa baharini nchini Afrika Kusini.


MWISHO
 
Asante sana shunnie hadithi ni tamu sana from teja to hero big up ethan
 
Shunie hongea Sana..
Yamekwisha hongera shunnie

Sent using Jamii Forums mobile app
Nyingine hiyo
 
Back
Top Bottom