Siku hizi kila Fani na Cheo vinadharauliwa kwa sababu hii

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Mar 24, 2018
21,340
51,903
SIKU HIZI KILA FANI NA CHEO KINADHARAULIWA KWA SABABU HII

Anaandika, Robert Heriel.
Mtibeli

Siku hizi hata uwe Mfalme, sijui Waziri, sijui Hakimu, sijui Rais, sijui Kuhani, sijui Mwalimu, sijui Mwanasheria, sijui Mwanajeshi, sijui polisi, au hata uwe Nabii. Kote Huko Kwa kizazi hiki utadharauliwa tuu.

Zipo sababu za kizazi hiki kuwa na dharau.

Fikiria Kwa sasa unamiaka 30 hivi. Alafu ulisoma na marafiki zako kibao ambao unaujua uwezo wao. Unajua kabisa baadhi Yao walikuwa wadhaifu darasani, unajua kabisa Fulani alifeli kidato cha nne lakini Leo unaambiwa ati ni Mwalimu anafundisha Watoto. Automatic dharau itaingia

Fikiria unajua kabisa Fulani Wakati unasoma naye hakuwa mwadilifu, alikuwa mwizi na mtu asiye na uadilifu. Lakini Kutokana na connection unaambiwa Leo ni Mkurugenzi sijui WA nini Huko. Hivi utamheshimi mtu wa hivyo?

Fikiria Mchungaji au sheikhe Fulani ni mzinzi na anatoka na Wake za Watu. Sheikhe au Mchungaji huyohuyo kwenye matukio ya Gizani unakutana naye, hivi utaachaje kudharau fani na Cheo hicho?

Mtu unajua kabisa Fulani anauwezo mdogo wa shule lakini Kutokana na janjajanja za hapa na pale unamkuta paaap! Yule kule juu sijui ni Daktari WA nini Huko au Mwanasheria WA kitu gani sijui. Hivi mtu huyo na Cheo hicho utaacha kuvidharau.

Unajua kabisa Rafiki yako hakuenda jeshini Kwa mapenzi ya jeshi, isipokuwa alikosa option nyingine, na unajua kabisa amefuata Mshahara, hivi huo uanajeshi utauheshimu kweli?
Unajua kabisa marafiki zako baadhi wameingizwa Kwa connection na sio wito. Unafikiri utawaheshimu au kuheshimu hao Watu.

Unajua kabisa Mbunge Au Rais Fulani ameingia Kwa kuiba Kura, na anatumia nguvu ya Dola kulinda Cheo chake. Hivi Kwa Akili ya kawaida utamheshimu? Kwa maana kwa namna hiyo MTU yeyote hata mtoto Mdogo anaweza kuwa Mbunge au Rais ilimradi tuu Dola imlinde. Hivi hapo kuna heshima? Ni lazima Watu wadharau Cheo Hiko na fani husika.

Kizazi cha sasa kipi katika Njia sahihi. Kinaonekana hakina Maadili Kutokana na ukosefu WA uadilifu wa wale waliowatangulia. Huwezi mpa heshima MTU unayejua kabisa huyu sio muadilifu. Huwezi. Na katika Hilo Vijana WA sasa wapo wazi kabisa.

Heshima inatokana na uadilifu, maadili na nidhamu ya Watu Kwa Yale wanayoyafanya.
Utadharaulika tuu hata ungekuwa Nani kama iso mwadilifu. Pamoja na kuwa utajidanganya unaheshimika lakini ukitaka kujua kuwa wewe sio lolote wala chochote Subiri siku uwe nje ya hicho Cheo na hiyo fani ndio utajua kuwa wewe unadharaulika.

Hauhitaji kuwa na Cheo, Elimu, na utajiri ndipo uheshimike. Unahitajika kuwa tuu mwadilifu, kujiheshimu, nidhamu, na Maadili.

Kuna Watu wanaheshimika licha ya kuwa wapo Chini yako kifani, kielimu, kiutajiri na kicheo Kwa sababu ya uadilifu wao.

Unapodhulumu Haki za wengine wewe ni MTU uliyejidharau na kudhaulika tuu hata ujidanganye.

Nafasi uliyonayo unajua kabisa haustahili kuwa nayo na wapo wanaostahili. Hiyo pekee inakufanya ujidharau na kudharaulika.

Unaenda kuomba kazi, unatumia Rushwa Kupata kazi hiyo. Hakuna utakachopata zaidi ya kudharauliwa tuu. Utajidharau, utadharauliwa na familia yako hasa Mkeo na watoto, na Ndugu kisha na jamii.

Ninawajua Watu ambao wanakaribu kila kitu Kwa vitu vinavyoonekana lakini vitu hivyo ni vya dhulma, na wengi wao walidhani wangeheshimika lakini wanadharaulika hasa na familia zao wenyewe, mtu Hana furaha lakini anakila kitu. Huko ni kudharauliwa.

Mtu unakila kitu lakini Mkeo Hakupendi, anakupeleka peleka, Watoto wako wanakupasua kichwa. Hiyo pekee ni dharau. Ukidhulumu wengine na wewe utadhulumiwa na kudharaulika.

Tuwe waadilifu. Tenda Haki ikiwa ni pamoja na kujipa unayostahili na kuwapa wengine wanayostahili.
Usilazimishe mambo huo sio uadilifu, hiyo sio HAKI.
Sio lazima wewe uwe tajiri, sio lazima. Ukishafanya lazima ndipo unapoingia katika mazingira ya dhulma.

Sio lazima wewe uwe Waziri, Mbunge au Rais. Sio lazima. Ukishafanya lazima udhulumu wengine ambao hiyari imemchagua.

Sio lazima upate kazi unayoitaka, usilazimishe Mambo.

Sio lazima umpate Mwanamke ambaye umeshaona hakupendi. Hata utumie Pesa, Cheo au chochote. Hiyo Mwanamke sio wako. Hiyo ni dhulma. Na utadharaulika tuu Mimi Taikon nimesema.
Sio lazima mwanaume Fulani awe Mume wako ikiwa umeshaona hakutaki. Usitumie nguvu Sana. Hiyo ni dhulma. Ni kukosa uadilifu.

Acha nipumzike sasa.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
 
Pambana kijana, dharau huwezi kuzitambua kama upo kwenye nafasi nzuri, fanya chochote ambacho kitakufanya uwe na nafasi nzuri na pesa za kutosha.
 
Unajua hata magufuli mimi nilikuwa namkubali sana ila siku aliposema nireteeni gwajima aiseee nilishangwaza sana.unajua kuna watu uwezo unajionyesha kupitia hata kuongea kwake unajua kbs mweupe huyu kuna waziri fulani jina lake linaanzia Na.. aiseee connection hizi
 
Unajua hata magufuli mimi nilikuwa namkubali sana ila siku aliposema nireteeni gwajima aiseee nilishangwaza sana.unajua kuna watu uwezo unajionyesha kupitia hata kuongea kwake unajua kbs mweupe huyu kuna waziri fulani jina lake linaanzia Na.. aiseee connection hizi

Hatari Sana.
 
SIKU HIZI KILA FANI NA CHEO KINADHARAULIWA KWA SABABU HII

Anaandika, Robert Heriel.
Mtibeli

Siku hizi hata uwe Mfalme, sijui Waziri, sijui Hakimu, sijui Rais, sijui Kuhani, sijui Mwalimu, sijui Mwanasheria, sijui Mwanajeshi, sijui polisi, au hata uwe Nabii. Kote Huko Kwa kizazi hiki utadharauliwa tuu.

Zipo sababu za kizazi hiki kuwa na dharau.

Fikiria Kwa sasa unamiaka 30 hivi. Alafu ulisoma na marafiki zako kibao ambao unaujua uwezo wao. Unajua kabisa baadhi Yao walikuwa wadhaifu darasani, unajua kabisa Fulani alifeli kidato cha nne lakini Leo unaambiwa ati ni Mwalimu anafundisha Watoto. Automatic dharau itaingia

Fikiria unajua kabisa Fulani Wakati unasoma naye hakuwa mwadilifu, alikuwa mwizi na mtu asiye na uadilifu. Lakini Kutokana na connection unaambiwa Leo ni Mkurugenzi sijui WA nini Huko. Hivi utamheshimi mtu wa hivyo?

Fikiria Mchungaji au sheikhe Fulani ni mzinzi na anatoka na Wake za Watu. Sheikhe au Mchungaji huyohuyo kwenye matukio ya Gizani unakutana naye, hivi utaachaje kudharau fani na Cheo hicho?

Mtu unajua kabisa Fulani anauwezo mdogo wa shule lakini Kutokana na janjajanja za hapa na pale unamkuta paaap! Yule kule juu sijui ni Daktari WA nini Huko au Mwanasheria WA kitu gani sijui. Hivi mtu huyo na Cheo hicho utaacha kuvidharau.

Unajua kabisa Rafiki yako hakuenda jeshini Kwa mapenzi ya jeshi, isipokuwa alikosa option nyingine, na unajua kabisa amefuata Mshahara, hivi huo uanajeshi utauheshimu kweli?
Unajua kabisa marafiki zako baadhi wameingizwa Kwa connection na sio wito. Unafikiri utawaheshimu au kuheshimu hao Watu.

Unajua kabisa Mbunge Au Rais Fulani ameingia Kwa kuiba Kura, na anatumia nguvu ya Dola kulinda Cheo chake. Hivi Kwa Akili ya kawaida utamheshimu? Kwa maana kwa namna hiyo MTU yeyote hata mtoto Mdogo anaweza kuwa Mbunge au Rais ilimradi tuu Dola imlinde. Hivi hapo kuna heshima? Ni lazima Watu wadharau Cheo Hiko na fani husika.

Kizazi cha sasa kipi katika Njia sahihi. Kinaonekana hakina Maadili Kutokana na ukosefu WA uadilifu wa wale waliowatangulia. Huwezi mpa heshima MTU unayejua kabisa huyu sio muadilifu. Huwezi. Na katika Hilo Vijana WA sasa wapo wazi kabisa.

Heshima inatokana na uadilifu, maadili na nidhamu ya Watu Kwa Yale wanayoyafanya.
Utadharaulika tuu hata ungekuwa Nani kama iso mwadilifu. Pamoja na kuwa utajidanganya unaheshimika lakini ukitaka kujua kuwa wewe sio lolote wala chochote Subiri siku uwe nje ya hicho Cheo na hiyo fani ndio utajua kuwa wewe unadharaulika.

Hauhitaji kuwa na Cheo, Elimu, na utajiri ndipo uheshimike. Unahitajika kuwa tuu mwadilifu, kujiheshimu, nidhamu, na Maadili.

Kuna Watu wanaheshimika licha ya kuwa wapo Chini yako kifani, kielimu, kiutajiri na kicheo Kwa sababu ya uadilifu wao.

Unapodhulumu Haki za wengine wewe ni MTU uliyejidharau na kudhaulika tuu hata ujidanganye.

Nafasi uliyonayo unajua kabisa haustahili kuwa nayo na wapo wanaostahili. Hiyo pekee inakufanya ujidharau na kudharaulika.

Unaenda kuomba kazi, unatumia Rushwa Kupata kazi hiyo. Hakuna utakachopata zaidi ya kudharauliwa tuu. Utajidharau, utadharauliwa na familia yako hasa Mkeo na watoto, na Ndugu kisha na jamii.

Ninawajua Watu ambao wanakaribu kila kitu Kwa vitu vinavyoonekana lakini vitu hivyo ni vya dhulma, na wengi wao walidhani wangeheshimika lakini wanadharaulika hasa na familia zao wenyewe, mtu Hana furaha lakini anakila kitu. Huko ni kudharauliwa.

Mtu unakila kitu lakini Mkeo Hakupendi, anakupeleka peleka, Watoto wako wanakupasua kichwa. Hiyo pekee ni dharau. Ukidhulumu wengine na wewe utadhulumiwa na kudharaulika.

Tuwe waadilifu. Tenda Haki ikiwa ni pamoja na kujipa unayostahili na kuwapa wengine wanayostahili.
Usilazimishe mambo huo sio uadilifu, hiyo sio HAKI.
Sio lazima wewe uwe tajiri, sio lazima. Ukishafanya lazima ndipo unapoingia katika mazingira ya dhulma.

Sio lazima wewe uwe Waziri, Mbunge au Rais. Sio lazima. Ukishafanya lazima udhulumu wengine ambao hiyari imemchagua.

Sio lazima upate kazi unayoitaka, usilazimishe Mambo.

Sio lazima umpate Mwanamke ambaye umeshaona hakupendi. Hata utumie Pesa, Cheo au chochote. Hiyo Mwanamke sio wako. Hiyo ni dhulma. Na utadharaulika tuu Mimi Taikon nimesema.
Sio lazima mwanaume Fulani awe Mume wako ikiwa umeshaona hakutaki. Usitumie nguvu Sana. Hiyo ni dhulma. Ni kukosa uadilifu.

Acha nipumzike sasa.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Unapumzika kwa raha gani Childhood mate?



Sent from my CPH2387 using JamiiForums mobile app
 
Umeongea kweli, lakini Nina jambo ningependa kusema, Najua watu uwa na tabia Fulani Kwa vipindi na mazingira Fulani. Lakini kutokana na mazingira na muda watu hao Wana nafasi na uwezo wa kubadilika na kuwa na tabia tofauti.

Nina maana Gani katika hili, maana yangu ni hii wale walionekana kukosa uadalifu nyakati Fulani katika kipindi cha ukuaji wao wanaweza pata fursa ya kubadilika na kuwa waadilifu kutokana na mazingira na muda.

Kuhusu kufeli form four na kuonekana mwalimu siku za usoni. Katika hili Kuna fursa nyingi hasa baada ya kuanguka katika mitihani ya form four. Kuna fursa ya kurudia shule, ama kuresit kama mtihainiwa binafsi nk. na kufanya vyema na hatimae kutimiza ndoto yoyote ile kuwa mwalimu, daktar nk. Tunajua kuteleza siyo kuanguka, wapo waliofeli kwasababu kweli hawana uwezo wa kufaulu lakini wapo waliofeli kutokana na sababu mbalimbali tofauti na uwezo.

Hivyo katika kufupisha ningeshauri tu tujenge utamaduni wa kuwa hukumu watu kutokana na wakati uliopo na si kuwahukumu kupitia maisha Yao ya hapo nyuma. Kwasababu Kila mja ana nafasi ya kubadilika na kuwa Bora au kinyume chake.
 
Muhimu kumiliki pesa.
Ukishakuwa na pesa za kutosha dharau inakosa nafasi.
Ukikosa pesa hata mpuuzi atakudharau tu
 
Pambana kijana, dharau huwezi kuzitambua kama upo kwenye nafasi nzuri, fanya chochote ambacho kitakufanya uwe na nafasi nzuri na pesa za kutosha.
Kufanya chochote even kwa gharama ya damu za watu au kufanya chochote unamaanisha nini?
 
Ndio kilichonifanya niache kwenda kupoteza muda kwenye foleni ya kupiga kura eti kuchagua mbunge, diwani, mwenyekiti wa kijiji/mtaa/kitongoji wakati namfahamu uwezo wake darasani ulikuwa wa ajabuajabu. Kuna wavuta bangi, malaya, wezi kwa wanafunzi wenzao eti anipotezee muda nipange foleni, sina muda huo, kura atapewa na wasiomfahamu tabia yake huko nyuma alipokuwa shuleni/chuoni. Wengine walikuwa na uwezo mdogo wa kumudu masomo hata ishirini bora ya wanafunzi hawakuwahi kushika, kila weekly test wanaambulia sifuri au namba za viatu unakuja kushangaa kapitishwa anagombea ubunge/udiwani. Anaingia bungeni/halmashauri michango yake hainekani kachangia nini kwa wananchi anaowawakilisha. Sitoagi kura kwa wapuuzi na sina muda huo
 
Siku zote watu huongozwa na wale the best katika jamii...
Ukiona tunaongozwa na wezi basi jamii nzima imejaa wezi...
Ukiona janja janja ujue jamii nzima janja janja .....

Tazama Nigeria ...jinsi walivyo matapeli halafu washangae wanavyolalamika utapeli kwenye uchaguzi......
Watanzania Wengi wasanii janja janja...na Viongozi wetu watakuwa hivyo hivyo
 
Back
Top Bottom