Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,812
- 11,987
Akitoa Pongezi hizo Mkuu wa Mkoa wa Arusha Ndugu John Mongella amebainisha kuwa kitendo cha Kamanda huyo kupandishwa cheo na Mheshimiwa Rais nikuaminiwa na kuonesha utendaji kazi mzuri ndani ya Mkoa huo ambao ni kitovu cha utalii hapa nchini .
Ameongeza kuwa Kamanda Masejo amekuwa chachu ya kuwaunganisha Askari wote kitendo kilichopelekea Mkoa huo kuwa shwari licha ya uwepo wa matukio madogo madogo ambayo yamedhibitiwa.
Pia amemshukuru Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Camillus Wambura na Mwenyekiti wa Kamati ya Usalama Mkoa wa Arusha kwa usimamizi wao mzuri katika utendaji wa kazi.