Kamati ya Usalama Arusha yampongeza SACP Masejo kwa kupandishwa cheo na Rais

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,812
11,987
Kamati ya Usalama Mkoa wa Arusha imempongeza Kamanda wa Polisi Mkoani humo kwa kupandishwa Cheo hivi karibuni na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan.

Akitoa Pongezi hizo Mkuu wa Mkoa wa Arusha Ndugu John Mongella amebainisha kuwa kitendo cha Kamanda huyo kupandishwa cheo na Mheshimiwa Rais nikuaminiwa na kuonesha utendaji kazi mzuri ndani ya Mkoa huo ambao ni kitovu cha utalii hapa nchini .

Ameongeza kuwa Kamanda Masejo amekuwa chachu ya kuwaunganisha Askari wote kitendo kilichopelekea Mkoa huo kuwa shwari licha ya uwepo wa matukio madogo madogo ambayo yamedhibitiwa.
WhatsApp Image 2024-02-19 at 16.56.28_b09e5258.jpg
Kwa upande wake Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha ambaye amepandishwa Cheo kutoka Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) kuwa Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Justine Masejo pamoja na kumshukuru Mheshimiwa Rais kwa kumpandisha hicho, ameahidi kuwa ataendelea kushirikina na vyombo vingine vya ulinzi na usalama ili Mkoa huo uendelee kuwa shwari wakati wote.

Pia amemshukuru Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Camillus Wambura na Mwenyekiti wa Kamati ya Usalama Mkoa wa Arusha kwa usimamizi wao mzuri katika utendaji wa kazi.
 
Hongera, mwenye nacho huongezewa, ambaye hana, hunyang'anywa hata kile kidogo alicho nacho!
 
Kamati ya Usalama Mkoa wa Arusha imempongeza Kamanda wa Polisi Mkoani humo kwa kupandishwa Cheo hivi karibuni na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan.

Akitoa Pongezi hizo Mkuu wa Mkoa wa Arusha Ndugu John Mongella amebainisha kuwa kitendo cha Kamanda huyo kupandishwa cheo na Mheshimiwa Rais nikuaminiwa na kuonesha utendaji kazi mzuri ndani ya Mkoa huo ambao ni kitovu cha utalii hapa nchini .

Ameongeza kuwa Kamanda Masejo amekuwa chachu ya kuwaunganisha Askari wote kitendo kilichopelekea Mkoa huo kuwa shwari licha ya uwepo wa matukio madogo madogo ambayo yamedhibitiwa.
Kwa upande wake Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha ambaye amepandishwa Cheo kutoka Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) kuwa Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Justine Masejo pamoja na kumshukuru Mheshimiwa Rais kwa kumpandisha hicho, ameahidi kuwa ataendelea kushirikina na vyombo vingine vya ulinzi na usalama ili Mkoa huo uendelee kuwa shwari wakati wote.

Pia amemshukuru Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Camillus Wambura na Mwenyekiti wa Kamati ya Usalama Mkoa wa Arusha kwa usimamizi wao mzuri katika utendaji wa kazi.
Amepandishwa cheo na rais kama mkuu wa muhimili wa serikali sio kama amiri jeshi mkuu. Pia hakuna amiri jeshi mkuu wa vyombo vya ulinzi na usalama bali ni amiri jeshi mkuu ambacho ni cheo cha juu ndani ya jeshi la ulinzi. Hilo neno vyombo vya ulinzi na usalama sio sahihi.

Ukishatamka amiri jeshi mkuu au supreme commander tayari inaeleweka ni cheo cha kijeshi hivyo neno usalama halipo.
 
Kupandishwa cheo bongo haitokani na kufanya kazi vizuri bali kutimiza matakwa ya bosi
 
Back
Top Bottom