Sijui nianzie wapi?

Sijui nianzie wapi?

Asante, nitaufanyia kazi ushauri wako.
ila swala bado lipo pale pale, baada ya hayo yote then what shall I do? should I sacrifice my happiness so that my children are happy? or should I keep on searching till god say yes? totally confused.

Pole kaka. Msamehe mke wako ila usimrudie. Watoto wanaolelewa chini ya dari la wazinzi na wagomvi wanatoka wabaya kuliko wanaoishi kwa upweke, tena wa muda. Huwa napenda kusisitiza quality ya wazazi/walezi kuliko idadi ya wazazi au walezi. Umeshaulizwa mke angekufa ingekuwaje? Wapo wanaume wenzio wamefiwa au kuachwa na wake zao wakaachiwa watoto wadogo na hawajaoa wala kupeleka watoto boarding. Wengine nawafahamu ni wanachama hapa wanaweza kukupa uzoefu. Unachotakiwa ni kubadilisha maisha tu na kuvaa kofia mbili za ubaba na umama kama wanavyofanya single parents wengine. Manake ni kuwa kama ulikuwa ukitoka kazini unapitia kwa mama kamche kupata bia na ktm unaacha, unaenda moja kwa moja nuumbani kwanza.

That you should sacrifice your happiness for your children's happiness is out of question. It is an OBLIGATION. Maadam umeamua kuzaa basi lengo lako la kwanza, la pili na la tatu ni kuhakikisha ustawi wa watoto wako. Manake ni kuwa utalala njaa wewe wao wale, utatembea kwa mguu wao wasome, utaomba ruhusa kazini ukakae nao dada akiondoka......yaani watoto wako wanatakiwa kuwa kila kitu kwako ikiwa ni pamoja na kujikana mwenyewe ili wafurahi. Ila kujikana huko kusihusishe kuhatarisha uhai wako. Ukitaka utaweza tu. Ondoa kichwani kwako kuwa malezi ni taaluma ya wanawake tu. Maadam we si mnyama, hili unaliweza.

Sikushauri kupeleka watoto boarding, na ukilazimika basi liwe ni suluhisho la muda wakati we unajipanga. Omba ndugu yako, pia tafuta yaya mzuri, mpe mshahara mzuri watoto wako watakuwa vizuri bila shida. Cha msingi upatikane, usiwe baba wa wikiendi, au baba mtoa hela tu.

Hilo la kuoa kaka tuliza boli. Subiri maji yapoe. Sasa hivi tunaongelea watoto. Au unamaanisha unataka uoe ili upate mlezi wa watoto? Kama ndivyo hii si sababu nzuri ya kuoa kwa sasa. Utaishia kupata garasa bure. Mke anayeweza kukulelea watoto hata watano yupo, ila atapatikana ukiwa umetulia. Kama unahofia ukipata mwenye m/watoto mzigo utakuwa mkubwa basi utatafuta mke anayeingiza kipato, au wewe utafute hela zaidi. Kwani huyo dadako na housegirl nani alikuwa anawagharamia? Hofu tu. Sasa utampata wapi binti ambaye hajazaa umuoe halafu asizae. Labda umpate ambae anajijua ni mgumba. Sasa hivi ume-panick kila kuti unataka kushika. Kwa jinsi mambo yalivyo sasa hivi bado huna uwezo wa kutafuta mke bora. Yaani unataka kufanya kata mti panda mti kwenye jambo sensitiv namna hii? Hapo bado jeraha linauma unarukaruka. Settle issue ya watoto kwanza, ukimaliza sasa ndo uanze kuskilizia maumivu yako. Ukishapona utatafakari njia ya kuchukua kuelekea kwenye mahusiano na wanawake. Sijui we ni mtu wa aina gani kimtazamo kwa hiyo ni vigumu kukushauri. Kama unaamini sana katika dini basi utataka uoe haraka ili usizini. Hii inaweza kukudidimiza shimoni endapo utakosea kuchagua. Kama unaweza kukaa bila ngono muda mrefu jaribu kwa muda tu au jifunze. Kama huwezi tafuta mwanamke ila mambo yenu yaishie huko nje ya geti watoto wasione wala kusikia. Nitarudi baadae.
 
I love this, haitofautiani Sana na ushauri Wangu kwake..though yako imeenda deep Sana na Ina ushauri nzuri Sana.
asante kwa ushauri wako kwa memba mwenzetu , ni Wa busara Sana , hope atachanganya na zake then atafanyia kazi.
Mimi pia kuna mawili matatu nimeya absorb from your ushauri .thanks
Karibu Crucial Man , nafurahi kusikia hivyo
Hopefully mto mada nae atapata cha kuchukua hapo. Pole na wewe kwa kutendwa bana..msikate tamaa. MAISHA LAZIMA YAENDELEE.
 
Last edited by a moderator:
Pole kaka. Msamehe mke wako ila usimrudie. Watoto wanaolelewa chini ya dari la wazinzi na wagomvi wanatoka wabaya kuliko wanaoishi kwa upweke, tena wa muda. Huwa napenda kusisitiza quality ya wazazi/walezi kuliko idadi ya wazazi au walezi. Umeshaulizwa mke angekufa ingekuwaje? Wapo wanaume wenzio wamefiwa au kuachwa na wake zao wakaachiwa watoto wadogo na hawajaoa wala kupeleka watoto boarding. Wengine nawafahamu ni wanachama hapa wanaweza kukupa uzoefu. Unachotakiwa ni kubadilisha maisha tu na kuvaa kofia mbili za ubaba na umama kama wanavyofanya single parents wengine. Manake ni kuwa kama ulikuwa ukitoka kazini unapitia kwa mama kamche kupata bia na ktm unaacha, unaenda moja kwa moja nuumbani kwanza.

That you should sacrifice your happiness for your children's happiness is out of question. It is an OBLIGATION. Maadam umeamua kuzaa basi lengo lako la kwanza, la pili na la tatu ni kuhakikisha ustawi wa watoto wako. Manake ni kuwa utalala njaa wewe wao wale, utatembea kwa mguu wao wasome, utaomba ruhusa kazini ukakae nao dada akiondoka......yaani watoto wako wanatakiwa kuwa kila kitu kwako ikiwa ni pamoja na kujikana mwenyewe ili wafurahi. Ila kujikana huko kusihusishe kuhatarisha uhai wako. Ukitaka utaweza tu. Ondoa kichwani kwako kuwa malezi ni taaluma ya wanawake tu. Maadam we si mnyama, hili unaliweza.

Sikushauri kupeleka watoto boarding, na ukilazimika basi liwe ni suluhisho la muda wakati we unajipanga. Omba ndugu yako, pia tafuta yaya mzuri, mpe mshahara mzuri watoto wako watakuwa vizuri bila shida. Cha msingi upatikane, usiwe baba wa wikiendi, au baba mtoa hela tu.

Hilo la kuoa kaka tuliza boli. Subiri maji yapoe. Sasa hivi tunaongelea watoto. Au unamaanisha unataka uoe ili upate mlezi wa watoto? Kama ndivyo hii si sababu nzuri ya kuoa kwa sasa. Utaishia kupata garasa bure. Mke anayeweza kukulelea watoto hata watano yupo, ila atapatikana ukiwa umetulia. Kama unahofia ukipata mwenye m/watoto mzigo utakuwa mkubwa basi utatafuta mke anayeingiza kipato, au wewe utafute hela zaidi. Kwani huyo dadako na housegirl nani alikuwa anawagharamia? Hofu tu. Sasa utampata wapi binti ambaye hajazaa umuoe halafu asizae. Labda umpate ambae anajijua ni mgumba. Sasa hivi ume-panick kila kuti unataka kushika. Kwa jinsi mambo yalivyo sasa hivi bado huna uwezo wa kutafuta mke bora. Yaani unataka kufanya kata mti panda mti kwenye jambo sensitiv namna hii? Hapo bado jeraha linauma unarukaruka. Settle issue ya watoto kwanza, ukimaliza sasa ndo uanze kuskilizia maumivu yako. Ukishapona utatafakari njia ya kuchukua kuelekea kwenye mahusiano na wanawake. Sijui we ni mtu wa aina gani kimtazamo kwa hiyo ni vigumu kukushauri. Kama unaamini sana katika dini basi utataka uoe haraka ili usizini. Hii inaweza kukudidimiza shimoni endapo utakosea kuchagua. Kama unaweza kukaa bila ngono muda mrefu jaribu kwa muda tu au jifunze. Kama huwezi tafuta mwanamke ila mambo yenu yaishie huko nje ya geti watoto wasione wala kusikia. Nitarudi baadae.
i see ! ndo maana niliamua kuja hapa jamvini.
asante sana kiongozi.
 
amekucheat bado unamtamani? mimi nakushauri tu nenda ukapime na DNA za watoto inawezekana wawili sio wako!!ukikuta sio wako nakushauri mrudie usimuache mkeo
 
Kahema, mrejeshe mkeo lakini umtenge kwa muda katika tendo la ndoa hadi baada ya kupima afya kwa muda utakao faa, hii isaidie kulea watoto kwa wazazi wote wawili....
 
Last edited by a moderator:
Kahema nimesoma tena thread yako pamoja na comments za watu na wewe ulivyojibu. Nimegundua kuna tatizo kubwa nyuma yenu ambalo hujafunguka. usipofunguka hata kwa kifupi, itakua ngumu kupata ushauri muafaka. na withdraw kwa sasa comments zangu za mwanzo za nini ufanye. Jaribu kufunguka kidogo ili tukupe ushauri unaostahili. Sipati picha mke kukimbia watoto wake for 6 days...!!! what went wrong, hebu funguka hapa na utuambie mlikutana wapi katika mazingira gani. Kingine usimlaumu sana, duniani hapa kuna mambo mengi, kuna mwanamke namfahamu alimkimbia mume wake na watoto watatu, mdogo akiwa na 9 months, akaenda kwa mwanamme mwingine, huko akazaa watoto wawili. hapa ninapoandika comments hizi, alishaachana na huyo mwanamme wa pili sasa hivi ni teja (mla unga na bangi) wa kupindukia. Ni mama mwenye degree yake huyu, above 40 lakini hapa ndipo alipoishia. watoto wake wote kaacha kwa baba zao. familia yake inadai aliondoka kimazingara kwa mume wa mwanzo. sina hakika na hili. hainingii akilini mwanamke kupotea na kuacha watoto watatu. mimi hata mmoja simuachi no matter what... Funguka kaka yangu, hapa ndio penyewe kwa ushauri.

sijui kama keshafunguka ila simshauri afunguke hapa labda aku-PM kama atakuamini. Sasa huyo mke unayemuongelea aliondoka kwa mume wa kwanza kimazingara, huko kwa wa pili ni mazingara pia? Kama watu walijua ni mazingara kulifanyika juhudi yoyote ya kumfungua kwenye hicho kifungo? Nimemsikitikia sana. Wapo wanawake negligent. Nina jirani ni mke wa hivyo. Muda wake mwingi ni saluni na "katalunya" kwa wale wanaopajua. Mume kaamua kuishi naye hivyo hivyo kwa hiyo malezi ya watoto anayafanya mume na housegirl ila unaweza kujiuliza hao watoto wa kike watakuja kuwa wanawake wa aina gani na wa kiume watakuja kupata wanawake wa aina gani. Sababu ya kuondoka na kuacha watoto iwe nzito au nyepesi, sababu ya kuzini iwe nzito au nyepesi haileti nafuu kwenye hili swala. Mwenzi mzinzi ni hatari kwa mwenzie na wanae. hakuna asiyejua matokeo ya dhambi yanaathiri waliomo na wasiokuwemo. Hata mleta mada asipofunguka ni wazi kuwa mpaka wamefikia kuachana walikuwa wakikwaruzana mara kwa mara kutokana na huo uzinzi - mara tatu zenye ushahidi. Kuaminiana kukikosekana ugomvi haukosekani.
 
asante sana, ila shida inakua nini? ningejua kafanya uchafu huu kwa mtu mmoja ningejitahidi kufumba macho ila nizaidi ya watu 3 niliodhibitisha. inakua ngumu kusamehe kirahisi hivi

I can feel u,pole sana mkuu
 
Kutenda kosa sio kurudia kosa huna budi kummsamehe Mama watoto wako ili mlee vijana wenu
 
Pole sana mkuu Muombe Mungu akujalie wepesi ila wazo la boarding hata mm nalikubali na huyo mtoto mdogo mpeleke kwa mama yako mzazi maana kwako itakuwa ngumu kumlea.Halafu kaa chini ujipange tena vizuri.Kwa vile umeshafunga naye ndoa omba kikao cha familia aelezwe huo upuuzi wake.Baada ya kikao mpe muda akae na mama yake apelekwe kitchen party upya.
 
Jaribu kusamehe....najua ngumu lakini rudi nyuma labda kuna attention fulani ulikuwa humpi ndo maana akaamua kutoka nje. Msione majumba watu wanavumilia mengi to keep family together. Siwezi kukupa uhakika kuwa huyo atakayekuja atakuwa na mapenzi kamilifu na watoto wako.

Usisahau ile methali yetu ya zimwi likujualo Kahema
 
Last edited by a moderator:
Duniani kweli kuna maajabu!!! yaani nimuache mtoto wa miezi 9 hata angekuwa wa miaka18,sio aniambie ondoka eti na mimi nifungashe virago vyangu haiwezekani,labda andoke aniache mimi na watoto wangu jamani mle leba pachungu pasikieni tu nyie wanume,ebu jichunguze na wewe kwanini atoke nje?mara tatu usimuone mbaya sababu binadamu ndio humfanya binadamu mwenzie aonekane mbaya, halafu yeye anajisifia mzuri
 
Kapime DNA, kama ni wako komaa nao mwenyewe, wewe ndiyo uwe baba-mama, kamwe usiwaletee mama wa kambo, ukiwa na uhusiano wa kimapenzi hakikisha usifanyie nyumbani kwako yale makitu ya wakubwa, pia mtambulishe kwa wanao. Mwanume kuishi bila mwanamke inawezekana. Mwisho weka nguvu sana kuboresha uchumi wako, kwani kuishi na watoto peke yako bila uchumi mzuri itakusumbua.
 
Pole mkuu ushauri mwingi mzuri umetoka naungana na wanaokushauri kutomrudia huyo aliyeweza kutoka nje na wanaume watatu ulowajua achilia mbali usiowajua. Huyu atakuwa na lile pepo la ngono. Kumrudia ni udhalili na ni hatari kwa ustawi wa famili yako. Nenda taratibu kuweza kuhakikisha watoto wanapata malezi mazuri na wanaathirika kwa kiwango kidogo inavyowezekana maana athari zitakuwepo tu. Pia naunga mkono ushauri wa kwanza utulie na usijitoe muhanga kwa kuoa bora mke ukaumia tena. By the way nakusifu kwa subira na uvumilivu kuweza kuthiitisha kwama katemea na wanaume watatu na bado ukaenda kwenye kufanya kesi! Una moyo mkubwa wa ujasiri. Nisingeweza. Mitihani uliyopitia ni midogo wapo waliopatwa na makubwa zaidi ya yako usikate tamaa. Kwa wanaohusika ''A clans man in trouble should be helped not blamed''
 
Aseee!!
yani mwanamke na watoto wa3 unacheat? Then?
ona sasa mateso kwa watoto.
Inamana huyo wa miezi 9 kaacha kunyonya ama?

Pole sana asee!!!

ubinadamu kazi!!!!!
 
Mpe talaka yake. Huna wazee wewe hao watoto wakalelewa na bibi yao?

Hili ni kama tu unaushahidi 100% without doubt na si circumstantial.

Na wenye kusamehe ni wabora zaidi.
 


4. mama watoto kila siku anapiga simu kuomba msamaha( japo najua kabisa jasiri haachi asili)

Hii nimeipenda bana ila hukuna njia nyingine zaidi kumrudisha mama nyumbani ili watoto wapate malezi ya wazazi wote wawili
vinginevyo hata darasani hawatakuwa vizuri.
 
Vipi hao watoto 3 wote wako au wengine ndo mama kapata huko kwa michepuko
 
Back
Top Bottom