Sijawahi kupanda ndege...Nielimisheni

Sijawahi kupanda ndege...Nielimisheni

Joined
Sep 9, 2013
Posts
52
Reaction score
28
Wadau..mi kusema cha ukweli sijawahi kupanda ndege toka nimezaliwa. Nataman sana siku moja kuipanda. Umri wangu ni miaka 35. Naomba tuelimishane....siku ya kwanza inakuagaje?..Nikifika pale airpot JINIA...naelekea wapi na wapi mpaka naingia ndani ya ndege?..na humo kwenye ndege nasikia kuna mikanda unajifunga....je unaweza kutembea humo ndani wakati ndege ikiwa juu?..natamani kujua kiujumla...habari za ndege. Safari za ndani na za yale madege makubwa ya nje.
 
Kuna uzi humu wa mwaka jana kama sikosei. Mwenzio aliuliza swali kama hili alikuwa anajiandaa kutoka Mwanza kwenda Dar .Majibu aliyapata, nikikumbuka nacheka sana. Utafute uzi huo.
 
Kama utakuwa umebeba Sembe wewe relax tu, ukiwa na papara utadakwa. Ila kama unasafiri tu kama abiria mwema tulia na utajifunza kutoka kwa muudumu au kuiga kwa abiria wenzako.
 
Kama utakuwa umebeba Sembe wewe relax tu, ukiwa na papara utadakwa. Ila kama unasafiri tu kama abiria mwema tulia na utajifunza kutoka kwa muudumu au kuiga kwa abiria wenzako.

Hahaha mbona una assume mkuu
 
Mpaka sasa...sijapata jibu lolote. ..watu wa jf mnaudhi wakati mwingine..daah. Mnajibu mavimavi tu
 
Mpaka sasa...sijapata jibu lolote. ..watu wa jf mnaudhi wakati mwingine..daah. Mnajibu mavimavi tu

Ok,jibu ni hili, ndege ni kama usafiri mwingine wowote,huwezi kukwama ukifika airport kwani utadesa kwa abiria wengine, ndani ya ndege ukijisikia kuchimba dawa unabonyeza kengele rubani anasimamisha kwenye kichaka unashuka na kushusha mzigo,pia usisahau kuomba siti ya dirishani ili uweze kununua vitu njiani na pia iwe rahisi ukitaka kutapika unatoa tu kichwa nje...safari njema.
 
Kwanini unafungua threads mbili zenye contents sawa kwa mpishano wa dakika moja? Ni kosa la kawaida ama ulikusudia?
 
Sorry...nilitaka niiweke huku..nikakosea nikaiweka kwenye kazi na tenda. Na sijui jinsi ya kufuta thread. Sijui mnafutaje..mi mgeni humu...natokea Mwanza..kwimba.
 
Ok,jibu ni hili, ndege ni kama usafiri mwingine wowote,huwezi kukwama ukifika airport kwani utadesa kwa abiria wengine, ndani ya ndege ukijisikia kuchimba dawa unabonyeza kengele rubani anasimamisha kwenye kichaka unashuka na kushusha mzigo,pia usisahau kuomba siti ya dirishani ili uweze kununua vitu njiani na pia iwe rahisi ukitaka kutapika unatoa tu kichwa nje...safari njema.

Au ukikutana na huyu bwana mfatishe kila anachofanya
 

Attachments

  • Abiria.jpg
    Abiria.jpg
    21.8 KB · Views: 613
Sorry...nilitaka niiweke huku..nikakosea nikaiweka kwenye kazi na tenda. Na sijui jinsi ya kufuta thread. Sijui mnafutaje..mi mgeni humu...natokea Mwanza..kwimba.
Umeniharibia nadhiri yangu,nilitaka kununa siku nzima ona sasa nimecheka!
 
Wadau..mi kusema cha ukweli sijawahi kupanda ndege toka nimezaliwa. Nataman sana siku moja kuipanda. Umri wangu ni miaka 35. Naomba tuelimishane....siku ya kwanza inakuagaje?..Nikifika pale airpot JINIA...naelekea wapi na wapi mpaka naingia ndani ya ndege?..na humo kwenye ndege nasikia kuna mikanda unajifunga....je unaweza kutembea humo ndani wakati ndege ikiwa juu?..natamani kujua kiujumla...habari za ndege. Sagari za ndani na za yale madege makubwa ya nje.

Sasa mkuu hiyo ni nafasi ya kazi au tenda?
Ok. Kwa ufupi ni mkosi mkubwa kwa kufikia umri huo hujapanda ndege.
1.Ukifika JNIA ukisha kaguliwa wewe fuata uelekeo wa mizigo yako,kuna milango midogo imefunikwa na vitu vyeusi.(Elekea huko)
2.Hakikisha umeoga vizuri na kuvaa nguo mpya iliyonyooshwa kwa pasi barabara
3.Beba chili sause na tomato itakusaidia wakati wa chakula
4.Ukiwa kwenye ndege usiongee ongee sana maana kuna monita anaandika majina ya wapiga kelele
 
Kuna uzi humu wa mwaka jana kama sikosei. Mwenzio aliuliza swali kama hili alikuwa anajiandaa kutoka Mwanza kwenda Dar .Majibu aliyapata, nikikumbuka nacheka sana. Utafute uzi huo.

Yule jamaa anaitwa GREAT VISIONAIRE... alikuwa anakuja kwa mjomba ake Moshi bar.. Two weeks ago alileta uzi hapa kuwa amepata mtoto na akawaomba wateja wake wa bodaboda wamvumilie kwa wiki moja atakuwa anacheza na mwanawe..
 
Last edited by a moderator:
Ok,jibu ni hili, ndege ni kama usafiri mwingine wowote,huwezi kukwama ukifika airport kwani utadesa kwa abiria wengine, ndani ya ndege ukijisikia kuchimba dawa unabonyeza kengele rubani anasimamisha kwenye kichaka unashuka na kushusha mzigo,pia usisahau kuomba siti ya dirishani ili uweze kununua vitu njiani na pia iwe rahisi ukitaka kutapika unatoa tu kichwa nje...safari njema.

..Mkuu MbongoTZ, hapo kweny mstari umemdanganya mwenzetu anayetafuta Ushauri kwetu. Ndege haisimami kwenye Kichaka ila inasimama kwenye Wingu zito kwa ajili ya Abiria wanaotaka Kuchimba dawa!:becky:
 
..Mkuu MbongoTZ, hapo kweny mstari umemdanganya mwenzetu anayetafuta Ushauri kwetu. Ndege haisimami kwenye Kichaka ila inasimama kwenye Wingu zito kwa ajili ya Abiria wanaotaka Kuchimba dawa!:becky:

Maajabu ya jf yanaendelea. Ila hapa nilipo ni ful vicheko mpaka baaas!
 
Back
Top Bottom