Sijawahi kuona Padre kilema

Wapo wengi vilema wa kiroho.
Sahihi mkuu. Upadre ni kama kuwa mwanajeshi. Huingii kwa kufanya escapism ya maisha ya kawaida. Unapaswa kuwa mzima tena mzima hasa. Ni uzima wa kimwili, kiroho na kiakili pia.
Uwe vema kiuweledi, nidhamu, uchaji wa MUNGU nk. Kule kwa uelewa mzuri si kichaka cha kujificha na kuyakimbia maisha ya kawaida.
Nzuri..
 
nimemkumbuka padre ndemino parokia ya uparo jimbo la moshi miaka ya 90, sijui bado yupo kwenye utumishi?
 
Mkuu mbona hilo Andiko la Kutoka 4:10-17 limeweka wazi kila kitu kuhusu ulemavu wa kuongea wa Musa. Mpaka Musa akajenga hoja ya kusema kutokana na tatizo lake hilo la kutokuweza kuongea vyema anaona hafai kupakwa mafuta(kwenda kumtumikia Mungu).

Na Mungu akaipangua hiyo sababu ya Musa kwa hoja Tatu...
1/Ni Mungu yeye mwenyewe aliyeumba huo Ulemavu (Akimaanisha analijua hilo na sio kikwazo cha Musa kwenda kumtumikia) Kutoka 4:11

2/Katikati ya huo ulemavu wa kinywa cha Musa basi Mungu mwenyewe atamwezesha kushinda. (Kutoka 4:12)

3/Atamtumia Haruni ambaye hana huo ulemavu wa kinywa kumsaidia Musa. (Kutoka 4:14-15)

Kuwa na ulemavu wa kuongea hakuna maana kuwa mtu hawezi kuwasiliana kabisa, anaweza kuwasiliana kwa namna tofauti, na hata kuongea huenda anaweza lakini sio kama inavyotakiwa.
ZASP unataka ligi sasa! Haya umeshinda. Hata hivo tofautisha kazi ya kanisa na ya mungu.So kila mtumishi ni mpakwa mafuta mungu hachukui sadaka vilema ila akijitwalia kilema nani amzuie? Upadre ni uamuzi wa mtu kujidhabihu kwa kazi ya mungu sasa tukimpelekea walemavu inakuwaje?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Musa alikuwa na kigugumizi na karibu yake alisogea haruni kwa hiyo MUNGU alipozungumza na musa kwa maelekezo kwa wana wa Israel mMUNGU huyo huyo alimwambia musa mwambie Haruni awaambie wana wa Israel maneno hayo na huo ulikuwa mpango wa MUNGU na ndiyo maana kuhani mkuu wa kwanza alikuwa haruni kwann hakuwa musa?musa alikuwa mkuu wa msafara kuwa vusha wana wa Israel na kumbuka pia musa alipopewa maelekezo ya kimueleza farao walikwenda na haruni kwa hivyo basi musa hakuwa kuhani,mapadre ni makuhani kama ilivyokuwa kwa watoto wa haruni,kwa kutambua mapungufu ya musa hakumfanya kuwa kuhani.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu nimependa hoja yako,ila ni yupi alikuwa mkuu kati ya hawa wawili?mbona akazungumza na musa badala ya Haruni?Ni kazi ya kuhani kwenda mbele za Bwana kwa niaba ya kundi sasa hapa ukisema musa hakuwa kuhani napata shaka kidogo kwani hata waliposubu sanamu ni musa aliyeanguka kifudifudi kwa siku 40 mbele za mungu je hili unalizungumziaje?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Musa alikuwa na kigugumizi na karibu yake alisogea haruni kwa hiyo MUNGU alipozungumza na musa kwa maelekezo kwa wana wa Israel mMUNGU huyo huyo alimwambia musa mwambie Haruni awaambie wana wa Israel maneno hayo na huo ulikuwa mpango wa MUNGU na ndiyo maana kuhani mkuu wa kwanza alikuwa haruni kwann hakuwa musa?musa alikuwa mkuu wa msafara kuwa vusha wana wa Israel na kumbuka pia musa alipopewa maelekezo ya kimueleza farao walikwenda na haruni kwa hivyo basi musa hakuwa kuhani,mapadre ni makuhani kama ilivyokuwa kwa watoto wa haruni,kwa kutambua mapungufu ya musa hakumfanya kuwa kuhani.

Sent using Jamii Forums mobile app
Ndugu yangu naona unaandika kwa kubahatisha sana, una unga unga maelezo sana.

Ngoja nikupe ufafanuzi wa kina kidogo.

1/Musa ndio alikuwa mtu wa kwanza kutumika katika Madhabahu ya kikuhani. Aliandaa yeye madhabahu na akaizindua yeye. (Kutoka 40:1-11)

2/Ndio kuhani pekee wa madhabahu ya kwanza aliyepakwa mafuta na Mungu mwenyewe. (Kutoka 3:12)

3/Na ni yeye Musa aliyewapaka mafuta makuhani wengine wote waliofuata kuja kutumikia madhabahuni.(Kutoka 40:12-16)

4/Hakuna mahali popote ambapo Biblia inasema Musa alikuwa na Kigugumizi, Biblia inasema Musa alikuwa hawezi kuzungumza vizuri kwa sababu alikuwa ana ulimi mzito. (Kutoka 4:10-12). Kitaalamu Kuwa na ulimi mzito kunaweza kumfanya mtu ashindwe kuzungumza vyema(Slagish speech) lakini hakuwezi kumfanya mtu awe na kigugumizi.

5/Suala la kuwa kuhani lilikuwa ni Full time duty, kwa nafasi aliyokuwa nayo Musa lisingewezekana kwake(Alikuwa akihusika na mambo mengi sana), na Mungu aliichagua koo ya haruni kutoka kabila la walawi kuwa jamii pekee ya ukuhani.
Zipo dhana za kiimani zinazosema kuwa kwa sababu Musa alikuwa na damu ya hatia(Aliwahi kuua) hivyo nafasi ya kuwa kuhani mkuu isingempasa, na wapo wanaosema japokuwa Musa alikuwa Mlawi, lakini uzao rasmi wa Musa ulikuwa una utata fulani kwa wayahudi(inasemekana Musa alioa mwanamke kutoka Afrika!!), hivyo suala ukuhani kwenda kwa Musa lingekuwa tata pia.

6/Hakuna uhusiano wowote wa kimantiki kati ya Ukuhani wa Kwenye Biblia na Upadri wa kanisa katoliki, kwa sababu hizi...
-Makuhani walioa na kuzaa.
-Ukuhani ulikuwa ni wa kikabila tu(Kabila la Walawi)
-Ukuhani ulikuwa ni wa kikoo tu(Ukoo wa Haruni tu)
-Ukuhani lilikuwa ni jambo la kiyahudi tu.
-Ukuhani ulikuwa kwenye Hekalu/Hema tu.
 
MOD mijadala ya aina hii inachochea ubaguzi na unyanyapaa.Hakuna tofauti na kuuliza kwa misingi ya ukabila,rangi au itikadi.
 
Hii sijui imekaaje! Ila kwa mapadre ni nadra sana kusikia anasema njoooni kwangu wenye mapepo niwaombee wasiojiweza watajiweza. Na toka nianze kusali katoliki mwaka wa 38 sasa sijawahi ona mtu kaanguka kisa pepo ndani ya kanisa.
Mkuu kutoa mapepo hakutokani na kusoma theolojia bali ni karama ya uponyaji, kimsingi kuna baadhi ya mapadri wanazo hizo karama ila siyo kwakuwa ni mapadri kupata hizo karama bali ni zawadi ya roho mtakatifu kwa mtu mmoja mmoja..!
 
Naheshimu utaratibu uliokubaliwa na taasisi yoyote kuendesha masuala yake, ikiwepo makanisa na misikiti.

Lakin ni muhimu tuheshimu pia watu wengine kwa namna tunavyoongelea,tusinyanyapae wengine,ingetosha kusema tu ndivyo utaratibu ulivyo.

Walemavu nao ni watu kamili kama walivyo wengine, nao wanaweza kujikana na kujitoa wazima kwa Mungu wao.

Rejea Matendo ya Mitume 10:15, alivyoviumba Mungu mwanadamu usiviite najisi.
Wewe wasema lkn ninani hata amkosoe MUNGU kwa maamuzi yake?hayo ndiyo aliyomuelekeza musa na haruni kuijulisha hazara ya wana wa Israel na wala c kunyanyapaa mbona wana wake hawakuhesabiwa?na haki ya mtoto kupewa baba badala ya mama?usimkosoe MUNGU kwa maamuzi yake,usje ukalaaniwa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndio ni kigezo kimojawapo...Na pia hakuna padre hanithi(ashakum si matusi)

Kwanini...?

Upadre na Sadaka(Sacrifice)...yani unajitoa mzima mzima kama ulivyo....Yani si una-opt kuwa padre kwasababu wewe ni mlemavu, au wewe audi.n...d ndio unakimbilia upadre..upadre ni Sadaka iliyosafi..ni kujitoa..bila kujibakiza..

Wajuzi watajazia nyama
Duh hawa jamaa hawapigagi nyeto kweli?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom