Sijawahi kuona Padre kilema

Sijawahi kuona Padre kilema

Kusali kwangu kote hapa duniani sijawahi kukutana na padre kilema. Au ni makanisa ninayo sali tuu? Je nikigezo kimojawapo cha kuwa Padre?
maelekezo ya mungu hayaruhusu,soma kitabu cha mambo ya walawi chote utapata habari za hayo yote na sababu zake,wakati musa akipewa maelekezo na MUNGU nae akimweleza HALUNI aliye kuwa KUHANI.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sasa kama alikuwa hawezi kuongea hata Mungu aliongea nae vipi? Haiingii akilini kuwa waliongea kwa ishara maana haikuandikwa hivyo ila alisema kuwa mimi siyo msemaji tangu utotoni.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu mbona hilo Andiko la Kutoka 4:10-17 limeweka wazi kila kitu kuhusu ulemavu wa kuongea wa Musa. Mpaka Musa akajenga hoja ya kusema kutokana na tatizo lake hilo la kutokuweza kuongea vyema anaona hafai kupakwa mafuta(kwenda kumtumikia Mungu).

Na Mungu akaipangua hiyo sababu ya Musa kwa hoja Tatu...
1/Ni Mungu yeye mwenyewe aliyeumba huo Ulemavu (Akimaanisha analijua hilo na sio kikwazo cha Musa kwenda kumtumikia) Kutoka 4:11

2/Katikati ya huo ulemavu wa kinywa cha Musa basi Mungu mwenyewe atamwezesha kushinda. (Kutoka 4:12)

3/Atamtumia Haruni ambaye hana huo ulemavu wa kinywa kumsaidia Musa. (Kutoka 4:14-15)

Kuwa na ulemavu wa kuongea hakuna maana kuwa mtu hawezi kuwasiliana kabisa, anaweza kuwasiliana kwa namna tofauti, na hata kuongea huenda anaweza lakini sio kama inavyotakiwa.
 
Nimuewahi muona mmoja hata asubuhi hii nimeonana naye. Though naye aliwahi nisimulia chamgamoto alizopitia mpaka hapo alipofika. Ni dhahiri kuna ubaguzi na mapokeo ya kipuuzi kuhusiana na ulemavu ktk utumishi huu.

Sent using Jamii Forums mobile app
Kama aliupata akiwa kazini lkn sheria za MUNGU hazikuruhusu soma mambo ya walawi mpaka mwanzoni mwa HESABU ambavyo vyote ni vitabu vya musa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndio ni kigezo kimojawapo...Na pia hakuna padre hanithi(ashakum si matusi)

Kwanini...?

Upadre na Sadaka(Sacrifice)...yani unajitoa mzima mzima kama ulivyo....Yani si una-opt kuwa padre kwasababu wewe ni mlemavu, au wewe audi.n...d ndio unakimbilia upadre..upadre ni Sadaka iliyosafi..ni kujitoa..bila kujibakiza..

Wajuzi watajazia nyama
Ni maelekezo ya MUNGU kwa musa juu ya makuhani wake watakavyokuwa wenye kasoro za ki maumbile hawakuruhusiwa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwahiyo padri akipata ajali na kukakatika mguu anavuliwa upadri wake?

Sent using Jamii Forums mobile app
Upadri ni daraja ukishafika hapo harifutiki ila waweza simamishwa secrament zote kusmamia lkn hata ukiumia ukavunjika miguu na ukaea huna nguvu tena za huduma basi utaishi katika makazi ya mapadre hata mauti kwakuwa ww ni mwana wa kanisa huna kwenu isipokuwa kwa kwanisa utahudumiwa na wala hutotengwa .

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama aliupata akiwa kazini lkn sheria za MUNGU hazikuruhusu soma mambo ya walawi mpaka mwanzoni mwa HESABU ambavyo vyote ni vitabu vya musa.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu naona unachanganya mambo mengi hapo.
Kuna tofauti kubwa kati ya kumtumikia Mungu na kutumika katika madhabahu ya hekalu(Hema) ya wayahudi.

Utaratibu wa kutumika katika madhabahu ya Hekalu(Hema) la Wayahudi ulikuwa mahususi sana, tena kabila moja tu la walawi ndio waliruhusiwa. Na hao ndio makuhani wa enzi hizo.

Leo hii hakuna Mahekalu ya kujengwa kwa mikono katika ukristo. Yapo majengo ya makanisa, na hayo sio mahekalu, ni nyumba zilizojengwa kawaida tu na watu wakaingia na kuabudu humo. Havina viwango vya kwenye biblia vilivyotumika kujenga mahekalu ya wayahudi.

Katika ukristo(Ndani ya Yesu) hekalu ni mwili wako(1Kor 6:19). Na kila mkristo ni Kuhani.(1Petro2:9)

Kumtumia Mungu(Kupakwa mafuta) ni jambo pana sana, ni zaidi ya ukuhani wa madhabahuni. Hivyo mtu yoyote yule anaweza 'kupakwa mafuta' na Mungu kwenda kumtumikia Mungu.
 
Kusali kwangu kote hapa duniani sijawahi kukutana na padre kilema. Au ni makanisa ninayo sali tuu? Je nikigezo kimojawapo cha kuwa Padre?
Swali juu ya swali....
Ushamuona mchungaji kiwete, au shekhe.... Au askofu...

Nyongeza..

Ushawah ona mchungaji kipofu au kiziwi...

Kingo
 
Mkuu usikufuru.
Mbele ya Mungu, mapungufu yako ya kimwili sio issue kabisa. Mungu akikuchagua, hakuna wa kupinga. Yeyote yule anaweza kupakwa mafuta. Ni mungu mwenyewe anaamua.

Unamjua Musa wewe?
Nenda kamsome halafu utagundua alikuwa na ulemavu gani.
Musa alikuwa na kigugumizi na karibu yake alisogea haruni kwa hiyo MUNGU alipozungumza na musa kwa maelekezo kwa wana wa Israel mMUNGU huyo huyo alimwambia musa mwambie Haruni awaambie wana wa Israel maneno hayo na huo ulikuwa mpango wa MUNGU na ndiyo maana kuhani mkuu wa kwanza alikuwa haruni kwann hakuwa musa?musa alikuwa mkuu wa msafara kuwa vusha wana wa Israel na kumbuka pia musa alipopewa maelekezo ya kimueleza farao walikwenda na haruni kwa hivyo basi musa hakuwa kuhani,mapadre ni makuhani kama ilivyokuwa kwa watoto wa haruni,kwa kutambua mapungufu ya musa hakumfanya kuwa kuhani.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndio ni kigezo kimojawapo...Na pia hakuna padre hanithi(ashakum si matusi)

Kwanini...?

Upadre na Sadaka(Sacrifice)...yani unajitoa mzima mzima kama ulivyo....Yani si una-opt kuwa padre kwasababu wewe ni mlemavu, au wewe audi.n...d ndio unakimbilia upadre..upadre ni Sadaka iliyosafi..ni kujitoa..bila kujibakiza..

Wajuzi watajazia nyama

Naheshimu utaratibu uliokubaliwa na taasisi yoyote kuendesha masuala yake, ikiwepo makanisa na misikiti.

Lakin ni muhimu tuheshimu pia watu wengine kwa namna tunavyoongelea,tusinyanyapae wengine,ingetosha kusema tu ndivyo utaratibu ulivyo.

Walemavu nao ni watu kamili kama walivyo wengine, nao wanaweza kujikana na kujitoa wazima kwa Mungu wao.

Rejea Matendo ya Mitume 10:15, alivyoviumba Mungu mwanadamu usiviite najisi.
 
Kwani sakrament ya wagonjwa ina kikomo cha kupakwa mafuta?
Nilitaka utamke hivyo ili watu wanapojadili wafahamu kuwa wanajadiliana na mtu aliyekaribia kufa kitandani (sio kwenye ajali) mara mbili hadi mapadri wakalazimika kuja kumuendeshea ibada za mwisho mbili tofauti
 
Back
Top Bottom