Mkuu unapotosha.
1. Musa hakuwa "bubu", bali alikuwa na kigugumizi.
2. Musa hakuwa kuhani, hivyo hakuwahi kupakwa mafuta. Kuhani alikuwa Haruni. Wsliokuwa wsnapakwa mafuta kwa desturi ya kiyahudi ni makuhani na wafalme.
Asante kwa kunikosoa.
Hoja hujibiwa kwa hoja, nami nitajibu hoja zako zote mbili hapa hapa.
1/Nilisema Musa alikuwa na ulemavu katika kuongea(Bubu!?). Neno bubu nimeliweka ndani ya mabano likiwa na alama ya mchangao na kuuliza, hivyo neno bubu ni maelezo yangu ya ziada, yenye kushangaa na kujiuliza, nikimaanisha nahisi hivyo japokuwa sina uhakika.
Katika ulimwengu wa sasa wa lugha ya kiswahili, Maneno kama Bubu, Kipofu, Kiwete na Kiziwi yanapigwa vita kutumika kwa sababu yanaunyanyapaa fulani hivi, na yanapotosha. Hivyo kitaalamu hutupendi kuyatumia sana japokuwa kijamii yamezoeleka.
Kitaalamu Bubu(Speech Disability) maana yake ni uwezo duni wa kuweza kuongea au kujieleza ukaeleweka katika hali ya kawaida, na ububu uko katika viwango tofauti sana, kuwa 'bubu' haina maana huwezi kuongea kabisa, wapo 'mabubu' wengi wanaongea kwa sehemu fulani. Kama ilivyo kwa mtu asiyeona(kipofu?), wapo miongoni mwao wanaweza kuona pia, hata kwa 'bubu' wapo wengi wanao uwezo fulani wa kuongea.
Je, Musa alikuwa na Kigugumizi? Hapo inabidi pia uje na maelezo ya kuthibitisha hilo kwa kutumia biblia, otherwise itakuwa ni hadithi ya kutunga.
2/Kupakwa mafuta ni neno la jumla sana, tena la kawaida sana kwenye Biblia likiwa na maana
Mungu kukuteua mahususi ili kwenda kufanya kazi yake maalum.
Mungu anaweza 'kukupaka mafuta' kwenda kufanya kazi yake mahususi yoyote. Wapo walioteuliwa kuwa makuhani, wengine mitume, wengine manabii nk.
Makuhani ni watu walioteuliwa na Mungu mahususi kwenda kufanyakazi ndani ya Hekalu tu. Hao ni wapakwa mafuta pia.
Musa aliteuliwa mahususi na Mungu kwenda kufanya kazi ya kuongoza wana wa israeli kutoka utumwani Misri. Hivyo Musa ni mpakwa mafuta kwa 100%.