Synthesizer
JF-Expert Member
- Feb 15, 2010
- 11,143
- 18,774
Hivi sisi waswahili tuna tatizo gani lakini? kwa nini tunaona kwamba kuna watu fulani wanastahili kupewa fursa za uongozi hata wafanye madhambi ya ajabu kiasi gani? Ina maana hapa nchini suala la uongozi kuna watu wanaostahili na wengine wasiostahili?
Mtu anafanya makosa makubwa katika nafasi fulani, anaondolewa, anapumzishwa na baada ya muda fulani anateuliwa tena katika nafasi nyingine ya uongozi. Au utakuta mtu anaharibu sana katika sehemu moja, badala ya kuwajibishwa anahamishiwa sehemu nyingine.
Imekuwa kawaida sasa kusikia Raisi, au Waziri Mkuu au Waziri wakisema kwamba mtu fulani ameharibu sana hapa. Arudishwe wizarani akapangiwe kazi nyingine. Au Raisi kamtumbua mtu fulani, atapangiwa kazi nyingine. Ina maana apewe nafasi ya kuharibu sehemu nyingine? Hivi ina maana kuna watu ambao wanapewa hati miliki za uongozi? Na wengine hawastahili?
Kwa mfano, watu walilalamika kuhusu tabia za baadhi ya wakuu wa mikoa, kuhusu dharau zao, lugha zao, pamoja na Chalamila, lakini hawakusikilizwa. Kweli ilibidi Raisi Samia asubiri hadi na yeye awe mhanga wa lugha zisizofaa ndio achukue hatua? Kwa nini alipoambiwa hakutaka kusikiliza?
Kuna mkuu wa mkoa mwingine ambae alichakachua msaada wa seikali, Jakaya Kikwete akakasirika na kumwondoa kwenye nafasi yake. Leo Raisi Samia anaamua kumteua kuwa Mkuu wa Mkoa. Hatuna watu wengine Tanzania wanaoweza kuwa wakuu wa mkoa bali yeye tu?
Mtu anafanya makosa makubwa katika nafasi fulani, anaondolewa, anapumzishwa na baada ya muda fulani anateuliwa tena katika nafasi nyingine ya uongozi. Au utakuta mtu anaharibu sana katika sehemu moja, badala ya kuwajibishwa anahamishiwa sehemu nyingine.
Imekuwa kawaida sasa kusikia Raisi, au Waziri Mkuu au Waziri wakisema kwamba mtu fulani ameharibu sana hapa. Arudishwe wizarani akapangiwe kazi nyingine. Au Raisi kamtumbua mtu fulani, atapangiwa kazi nyingine. Ina maana apewe nafasi ya kuharibu sehemu nyingine? Hivi ina maana kuna watu ambao wanapewa hati miliki za uongozi? Na wengine hawastahili?
Kwa mfano, watu walilalamika kuhusu tabia za baadhi ya wakuu wa mikoa, kuhusu dharau zao, lugha zao, pamoja na Chalamila, lakini hawakusikilizwa. Kweli ilibidi Raisi Samia asubiri hadi na yeye awe mhanga wa lugha zisizofaa ndio achukue hatua? Kwa nini alipoambiwa hakutaka kusikiliza?
Kuna mkuu wa mkoa mwingine ambae alichakachua msaada wa seikali, Jakaya Kikwete akakasirika na kumwondoa kwenye nafasi yake. Leo Raisi Samia anaamua kumteua kuwa Mkuu wa Mkoa. Hatuna watu wengine Tanzania wanaoweza kuwa wakuu wa mkoa bali yeye tu?