Shule Binafsi ziheshimu likizo za watoto wetu

Imekuwa ni kawaida kwa watoto wanasoma Shule za Binafsi kuwabebesha watoto mafurushi ya kazi za kufanya wakiwa likizo almaarufu Kama HOLIDAY PACKAGES na wakati mwingine watoto wanaendelea kwenda shuleni wakati wa likizo kwa kile kinachoitwa HOLIDAY COACHING. Sasa hizi ni likizo?

Likizo zingeachwa huru ili watoto wawe huru kuwasaidia wazazi wao kazi za nyumbani au kusafiri kwenda kuwasalimia bibi zao huko vijijini ili wafahamu asili yao na pia kujumuika na ndugu zao wengine.

Tungeomba Serikali ilitazame hili jambo na ikiwezekana itoe mwongozo kuhusiana na jili jambo. Tusiwafanye watoto wetu kuwa kama ndondocha, kuna maarifa mengine ambayo watoto wanayahitaji zaidi ya hesabu, fizikia na jiorafia.

Naomba kuwasilisha.
Ndiyo tatizo la hizi Elimu za kukariri, Walimu wanajuwa Watoto wakienda likizo yote, Watoto watasahau yale yote walio wakaririsha,kwa hiyo inabidi waendelee kuwakaririsha hata kipindi cha likizo! Na upande wa pili Walimu nao wanafaidika na hivyo vimichango vya likizo! Mimi kwenye kikao Cha shule anakosoma mwangu niliwashauri kipindi Cha likizo Watoto wasome kuanzia saa mbili hadi saa tano,masaa matatu yanatosha! Nashukuru Walimu walilifanyia kazi japokua waliongeza lii saa limoja na nusu! Watoto wanaingia saa moja na nusu asubuhi na kutoka saa sita mchana,na kwa siku wanasoma masomo mawili tu!!
 
Ni kweli kabisa.

Hii inatokana na walimu wa shule hizo kuwa wavivu kumaliza syllabus.

Kingine ni kwamba ma director wa shule pia huchelelewa kuwalipa walimmu mishahara au kutowalipa kabisa na hivyo walimu hawafundishi.

Wanakuja kukurupuka mwezi wa 5 umekaribia na ndiyo matokeo yake wanaleta hizi HOLIDAY PACKAGE.

Serikali iingilie kati hili suala maana madirector wanaadhbu mtu asiyetoa HOLIDAY PACKAGE
Holiday package inatolewa kama revision ya kile kilichofundishwa na haihusiani na walimu kutokufundisha mana huwezi toa package sehem ambayo hukufundisha mwanafunzi atajaza nini?
 
Yaani likizo ya wiki 4 watoto wanaendelea kwenda shule kwa wiki 3 halafu watapumzika wiki moja ya mwisho. Unalipa ziada kwa ajili ya hiyo holiday programme halafu wanataka mtoto akakae boarding. Eti watasoma kuanzia alfajiri mpaka saa Tatu usiku ( like seriously?).Sasa basi unalazimika kununua mahitaji ya boarding kwa ajili ya wiki tatu kumbuka na likizo ikiisha unadaiwa ada. Bila kusahau kwamba ulishalipia picnic ambayo walienda siku ya kufunga shule. Jaman hata huruma hawana. Wanalazimisha kutunyang'anya watoto wakiwa bado wadogo na mazingira yenyewe ya boarding hata hayaridhishi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kumbe naongea na mtu asiyejua hata Lesson Plannig ni nini.

I am wasting my time
Alitaka umwambie lesson plan, ila hiyo lesson planning ndo kwanza anaisikia kwako. Ndo elimu zetu za madesa, tuvumiliane tu, mheshimiwa mkuu.
 
Hakuna faida yoyote mkuu, mtoto anatakiwa ku-refresh akili kwa kufanya mambo mengine tofauti na ABC za huko shuleni. Imagine kama wewe unapata likizo then boss anasema uje kazini kila siku, kisa kuna pending issues hakukupa wakati ukiwa ofisini.

Kwani zamani tulisoma vipi, mbona watu walifaulu tu!!
Tena usiongee kabisa kuhusu sie wa zamani,nakumbukua mimi kwa bibi yangu nilikua sina likizo,nasoma daily nikitoka shule
Huwezi kujifananisha wewe mtu mzima na mtoto ndugu,wewe huwezi sahau majukumu yako ya kazi lakini mtoto ni rahisi kusahau vitu haraka
 
Yaani likizo ya wiki 4 watoto wanaendelea kwenda shule kwa wiki 3 halafu watapumzika wiki moja ya mwisho. Unalipa ziada kwa ajili ya hiyo holiday programme halafu wanataka mtoto akakae boarding. Eti watasoma kuanzia alfajiri mpaka saa Tatu usiku ( like seriously?).Sasa basi unalazimika kununua mahitaji ya boarding kwa ajili ya wiki tatu kumbuka na likizo ikiisha unadaiwa ada. Bila kusahau kwamba ulishalipia picnic ambayo walienda siku ya kufunga shule. Jaman hata huruma hawana. Wanalazimisha kutunyang'anya watoto wakiwa bado wadogo na mazingira yenyewe ya boarding hata hayaridhishi.

Sent using Jamii Forums mobile app
Maana za mzazi au mlezi wa mtoto ni kumlinda mtoto dhidi ya dhuluma na unyang'au wa aina yoyote ile. Watoto wa haki ya kupata mapunziko yaliyo kwisha ainishwa na wanasaikologia(na hata ya dharura kama misiba na maradhi), kwamba ni ya lazima kwa kila mtoto kwa mihula yote ya masomo.
 
Hii ni kwa faida ya mwanao
Mtoto sio kama wewe,akiwa nyumbani mchezo ukikolea+vikatuni anasahau kila kitu cha shuleni kiasi kwamba akifika shule inahitaji juhudi za ziada ili aweze kucatch up na ndo mana unapewa hiyo package ili mtoto asisahau sana ya shuleni
It's simple kama hutaki acha chukua hiyo package choma moto as sio kwamba atatakiwa apeleke isahishwe irekodiwe kwenye ripoti yake!
Hata sisi tulisoma na wakati wa likizo tulikuwa tunacheza.

Shule zikifunguliwa week ya kwanza inakufanya urudi darasani.

Kuna sababu za kuwekwa kwa likizo.

Ila shule za sasa kama kanisa, kulazimisha kupata vipato.
 
Hakuna faida yoyote mkuu, mtoto anatakiwa ku-refresh akili kwa kufanya mambo mengine tofauti na ABC za huko shuleni. Imagine kama wewe unapata likizo then boss anasema uje kazini kila siku, kisa kuna pending issues hakukupa wakati ukiwa ofisini.

Kwani zamani tulisoma vipi, mbona watu walifaulu tu!!
Na hizo shule zinazolazimisha watoto waendelee kusoma ndo zinazidi kuwa za mwisho kwenye mitihani mingine.

Shule ya uhakika inakuwa na program nzuri za kueleweka na watoto wanapewa likizo.
 
Wewe ndiye unaujua ukweli.

Wababaishaji watupu hao wamejaa kwenye elimu yetu.

Na hizo shule zinazolazimisha watoto waendelee kusoma ndo zinazidi kuwa za mwisho kwenye mitihani mingine.

Shule ya uhakika inakuwa na program nzuri za kueleweka na watoto wanapewa likizo.
 
Hata sisi tulisoma na wakati wa likizo tulikuwa tunacheza.

Shule zikifunguliwa week ya kwanza inakufanya urudi darasani.

Kuna sababu za kuwekwa kwa likizo.

Ila shule za sasa kama kanisa, kulazimisha kupata vipato.
Mwisho wa siku sio lazima mtoto afanye hayo maswali,kama vipi we mwache mwanao acheze weee,arukeruke,aige vikatuni vyote,ajipikilishe,komborera hapo yani kikubwa uhai!
 
Kama wewe ni mzazi na umepleka mwanao shula na unakuja hapa kulalamika basi kuna shida mahali tena kubwa sana................. halafu wewe ni wale hamna elimu mmepata pesa mnafuata mkumbo wa kuwapeleka watoto shule sio mbaya lakini ukafuata kinachofanywa sio uwe na hisia tuu wewe lazima Elimu uako iko chini sana tuu
 
Anzisha shule yako hayo mambo usiyaweke!

Wazazi ni vichwa ngumu sana, kesho mwanao akifeli lawama kwa shule
akipewa shughuli za masomo ili afahulu vizuri napo maneno
Wwe lazima utakua Mwalimu aliyegeuza Elimu kuwa bishara!!
 
Mwambe bibi yao AJE ,shule zakata zipo wapelekee endapo unataka bibiyao awaone....
Wwe Kama ni Mwalimu pole sana, maana hujui hata kujenga hoja ya Msingi,mjibu mtu kwa hoja,Mipasho ya nini!? eti sijui amwambie Bibi yake,Sasa Bibi yake anaiingiaje hapa!?
 
Back
Top Bottom