jkipaji
JF-Expert Member
- Sep 22, 2019
- 5,703
- 7,581
Ndiyo tatizo la hizi Elimu za kukariri, Walimu wanajuwa Watoto wakienda likizo yote, Watoto watasahau yale yote walio wakaririsha,kwa hiyo inabidi waendelee kuwakaririsha hata kipindi cha likizo! Na upande wa pili Walimu nao wanafaidika na hivyo vimichango vya likizo! Mimi kwenye kikao Cha shule anakosoma mwangu niliwashauri kipindi Cha likizo Watoto wasome kuanzia saa mbili hadi saa tano,masaa matatu yanatosha! Nashukuru Walimu walilifanyia kazi japokua waliongeza lii saa limoja na nusu! Watoto wanaingia saa moja na nusu asubuhi na kutoka saa sita mchana,na kwa siku wanasoma masomo mawili tu!!Imekuwa ni kawaida kwa watoto wanasoma Shule za Binafsi kuwabebesha watoto mafurushi ya kazi za kufanya wakiwa likizo almaarufu Kama HOLIDAY PACKAGES na wakati mwingine watoto wanaendelea kwenda shuleni wakati wa likizo kwa kile kinachoitwa HOLIDAY COACHING. Sasa hizi ni likizo?
Likizo zingeachwa huru ili watoto wawe huru kuwasaidia wazazi wao kazi za nyumbani au kusafiri kwenda kuwasalimia bibi zao huko vijijini ili wafahamu asili yao na pia kujumuika na ndugu zao wengine.
Tungeomba Serikali ilitazame hili jambo na ikiwezekana itoe mwongozo kuhusiana na jili jambo. Tusiwafanye watoto wetu kuwa kama ndondocha, kuna maarifa mengine ambayo watoto wanayahitaji zaidi ya hesabu, fizikia na jiorafia.
Naomba kuwasilisha.