DOKEZO Unyanyasaji kwa Walimu wanaofundisha shule ya St. Matthew

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

Dad165

Member
Sep 9, 2023
64
186
Natumaini mu-wenye afya njema. Poleni na mapambano ya kila siku. Ni mara yangu ya kwanza kuandika katika jukwaa hili hasa baada ya kuwa nasoma maandiko mengi tu ya wadau mbalimbali yanayohusu mambo mengi katika jamii zetu.

Ni jukwaa pendwa pia kuwazungumzia watanzania wenzetu ambao wanashindwa kupaza sauti pale wanapokuwa wanapitia masahibu katika maeneo yao ya kazi.

Kuna shule ipo Mkuranga, umbali tu kidogo kutoka Kongowe Mbagala, inaitwa St. Matthew's. Ni shule ya sekondari japo pia wana msingi. Shule hii ni shule dada na St. Mark's- Mbagala, Ujenzi sec.-Vikindu na Imagevosa-iringa.

Ni shule kubwa yenye wastani wa wanafunzi 680-700 kwa kidato cha kwanza hadi cha sita. Kwa muda sasa mrefu sasa, walimu wanahangaika kwa kutokulipwa mishahara. Ndugu yangu wa karibu anaefanya kazi pale ameniambia "kwa ushahidi" kwamba ni zaidi ya miezi saba na hajalipwa mahahara wake.

Kila anaesimama kuhoji mshahara wake anaondolewa kazi bila hata notice. Walimu wanaishi kwa shida sana. Wamewahi kuchukua hatua na kuripoti katika halmashauri ya mkuranga. Waliobanika kufikisha taarifa hizo walifukuzwa kazi na tena bila kulipwa stahiki zao na bado halmashauri ya mkuranga haikushughulika na suala hilo. Mwezi huu wa tisa baada ya likizo fupi kuisha, kuna walimu wengine wanne wameondoshwa.

Sababu ni kwamba watoto wapatao asilimia kumi katika masomo yao hawajafikisha wastani. Lakini hawa ni walimu wapya, wameajiliwa miezi mitatu tu iliyopita kabla ya kufanya mitihani ya midterm. Wanawazungusha kuwalipa stahiki zao.. Uongozi unawazungusha kuwalipa stahiki zao hasa baada ya kuachishwa kazi.

Naziomba mamlaka zinazohusika, kufuatilia suala hili hasa kwa kuzingatia kwamba vijana wengi wanaofanya kazi katika taasisi za binafsi wana malengo wanataka kuyafikia pia. Tukemee vitendo vya unyanyasaji katika sehemu za kazi.

Ikiwa kuna mtu yeyote mwenye details za wapi pa kuanzia ili kuwasaidia kwa ngazi za kiserikali tafadhali toa maoni.

Asanteni sana.
 
Natumaini mu-wenye afya njema. Poleni na mapambano ya kila siku. Ni mara yangu ya kwanza kuandika katika jukwaa hili hasa baada ya kuwa nasoma maandiko mengi tu ya wadau mbalimbali yanayohusu mambo mengi katika jamii zetu.
Ni wahuni sana wale jamaa. Rafiki yangu alikuwa akifanya kazi hapo. Yeye alikuwa anakwenda kudai mshahara wake kila mwezi. Mwezi wa nane mwaka huu alisitishiwa mkataba eti ni msumbufu🤣🤣. Ila yeye alikomaa hadi akalipwa. Inaongozwa kihuni sana ile shule. Rushwa ya ngono pia nje nje kwa viongozi. Serikali itupie jicho hapo.
 
Shule za private kwa sasa hazina mapato... Serikali imejenga na inaendelea jenga Sekondari, na hakuna Ada.

Poleni sana.
Mtoa hoja amesema shule ina wanafunzi wanaokaribia mia saba. Shule ya namna hiyo inakosaje pesa za kuwalipa walimu? Kuna shule nyingine ukisikia habari ya walimu kutolipwa, unaweza kuanza kufikiria uchache wa wanafunzi. Kwa idadi hiyo ya wanafunzi, hapana!

Ni ukorofi na dharau kwa walimu wetu. Kama walitoa malalamiko yao kwa halmashauri ya mkuranga na viongozi mpo humu, tunaomba kesi hii ishughulikiwe haraka ili watoto waendelee kupata elimu bora. Nimepata taarifa nyingine kuhusu hii shule na ni hatari sana kwa maendeleo na ustawi wa watoto. Mamlaka chukueni hatua. Walimu si kundi la kuchezea.
 
Mtoa hoja amesema shule ina wanafunzi wanaokaribia mia saba. Shule ya namna hiyo inakosaje pesa za kuwalipa walimu? Kuna shule nyingine ukisikia habari ya walimu kutolipwa, unaweza kuanza kufikiria uchache wa wanafunzi. Kwa idadi hiyo ya wanafunzi, hapana! Ni ukorofi na dharau kwa walimu wetu. Kama walitoa malalamiko yao kwa halmashauri ya mkuranga na viongozi mpo humu, tunaomba kesi hii ishughulikiwe haraka ili watoto waendelee kupata elimu bora. Nimepata taarifa nyingine kuhusu hii shule na ni hatari sana kwa maendeleo na ustawi wa watoto. Mamlaka chukueni hatua. Walimu si kundi la kuchezea.!
Tunatumia fake ID ni sehemu sahihi ya kuweka hizo taarifa zingine ili zitasaidia sisi wazazi tuliokuwa tunategemea kupeleka watoto katika hizo shule. Zinawezekana taarifa hizo zikawa sahihi au lah, lakini za kuambiwa tutachanganya na za kwetu sisi kama wazazi. Ebu funguka bro.
 
Tunatumia fake ID ni sehemu sahihi ya kuweka hizo taarifa zingine ili zitasaidia sisi wazazi tuliokuwa tunategemea kupeleka watoto katika hizo shule. Zinawezekana taarifa hizo zikawa sahihi au lah, lakini za kuambiwa tutachanganya na za kwetu sisi kama wazazi. Ebu funguka bro.
Baada ya kazi leo, nahitaji kufuatilia ili nipate uhakika zaidi. Lakini pia tayari nimepata contacts za baadhi ya wanyanyaswaji. Nitaweka hapa taarifa yote baadae nikishajiridhisha. Mtoa hoja naomba pia uni-pm ukishakuwa hewani. Pm yako imefungwa!
 
Baada ya kazi leo, nahitaji kufuatilia ili nipate uhakika zaidi. Lakini pia tayari nimepata contacts za baadhi ya wanyanyaswaji. Nitaweka hapa taarifa yote baadae nikishajiridhisha. Mtoa hoja naomba pia uni-pm ukishakuwa hewani. Pm yako imefungwa!
Pm huko tusiguse maana bado hatufahamiani. Muhimu ni wahusika kushughulikia suala hili mapema. Kama kuna lolote la kuongezea tiririka mkuu.
 
Natumaini mu-wenye afya njema. Poleni na mapambano ya kila siku. Ni mara yangu ya kwanza kuandika katika jukwaa hili hasa baada ya kuwa nasoma maandiko mengi tu ya wadau mbalimbali yanayohusu mambo mengi katika jamii zetu.

Ni jukwaa pendwa pia kuwazungumzia watanzania wenzetu ambao wanashindwa kupaza sauti pale wanapokuwa wanapitia masahibu katika maeneo yao ya kazi.

Kuna shule ipo Mkuranga, umbali tu kidogo kutoka Kongowe Mbagala, inaitwa St. Matthew's. Ni shule ya sekondari japo pia wana msingi. Shule hii ni shule dada na St. Mark's- Mbagala, Ujenzi sec.-Vikindu na Imagevosa-iringa.

Ni shule kubwa yenye wastani wa wanafunzi 680-700 kwa kidato cha kwanza hadi cha sita. Kwa muda sasa mrefu sasa, walimu wanahangaika kwa kutokulipwa mishahara. Ndugu yangu wa karibu anaefanya kazi pale ameniambia "kwa ushahidi" kwamba ni zaidi ya miezi saba na hajalipwa mahahara wake.

Kila anaesimama kuhoji mshahara wake anaondolewa kazi bila hata notice. Walimu wanaishi kwa shida sana. Wamewahi kuchukua hatua na kuripoti katika halmashauri ya mkuranga. Waliobanika kufikisha taarifa hizo walifukuzwa kazi na tena bila kulipwa stahiki zao na bado halmashauri ya mkuranga haikushughulika na suala hilo. Mwezi huu wa tisa baada ya likizo fupi kuisha, kuna walimu wengine wanne wameondoshwa.

Sababu ni kwamba watoto wapatao asilimia kumi katika masomo yao hawajafikisha wastani. Lakini hawa ni walimu wapya, wameajiliwa miezi mitatu tu iliyopita kabla ya kufanya mitihani ya midterm. Wanawazungusha kuwalipa stahiki zao.. Uongozi unawazungusha kuwalipa stahiki zao hasa baada ya kuachishwa kazi.

Naziomba mamlaka zinazohusika, kufuatilia suala hili hasa kwa kuzingatia kwamba vijana wengi wanaofanya kazi katika taasisi za binafsi wana malengo wanataka kuyafikia pia. Tukemee vitendo vya unyanyasaji katika sehemu za kazi.

Ikiwa kuna mtu yeyote mwenye details za wapi pa kuanzia ili kuwasaidia kwa ngazi za kiserikali tafadhali toa maoni.

Asanteni sana.
Njia ni Moja tu,

Unganeni tafuteni peter kibatala au Tundu lisu mkutane na mmiliki mahakamani.

Halmashauri wakikatiwa fungi we huna chako.Utapigishwa swaga za kutosha.

Dawa ni kwenda mahakamani
 
Ama kweli mambo yanabadilika,St. Mathew leo ndo imefikia hatua hii😂😂😂🙌🙌. Miaka ile darasa langu la form four tuliofanya mtihani wa taifa tulikuwa 406,hiyo ni kidato kimoja tu,walimu walikuwa wakijituma sana,walikuwa wakipewa motisha ya safari za nje,magari na pesa taslim kutoka kwa mmiliki wa shule,sikuwahi kusikia lawama za hivi. Hakikia imenivunjavunja moyo.
Kwenye mambo haya inajihidhirisha makosa ambayo wazazi wengi wanayafanya,unakuwa na mali na vitega uchumi lakini huwaandai warithi wako katika kuzisimamia mali na vitega uchumi vyao,mzee Mtembei nilisikia alikuwa akiumwa,akapelekwa India mara kadhaa sifahamu hali yake kwa sasa ila chini ya usimamizi wake ilikuwa vyema. Baada ya kuumwa NASIKIA aliweka watoto na mke wasimamie na kasheshe zikaanzia hapo na sasa ni wazi wameshindwa kabisa au wanaiharibu kabisa.
 
Natumaini mu-wenye afya njema. Poleni na mapambano ya kila siku. Ni mara yangu ya kwanza kuandika katika jukwaa hili hasa baada ya kuwa nasoma maandiko mengi tu ya wadau mbalimbali yanayohusu mambo mengi katika jamii zetu.

Ni jukwaa pendwa pia kuwazungumzia watanzania wenzetu ambao wanashindwa kupaza sauti pale wanapokuwa wanapitia masahibu katika maeneo yao ya kazi.

Kuna shule ipo Mkuranga, umbali tu kidogo kutoka Kongowe Mbagala, inaitwa St. Matthew's. Ni shule ya sekondari japo pia wana msingi. Shule hii ni shule dada na St. Mark's- Mbagala, Ujenzi sec.-Vikindu na Imagevosa-iringa.

Ni shule kubwa yenye wastani wa wanafunzi 680-700 kwa kidato cha kwanza hadi cha sita. Kwa muda sasa mrefu sasa, walimu wanahangaika kwa kutokulipwa mishahara. Ndugu yangu wa karibu anaefanya kazi pale ameniambia "kwa ushahidi" kwamba ni zaidi ya miezi saba na hajalipwa mahahara wake.

Kila anaesimama kuhoji mshahara wake anaondolewa kazi bila hata notice. Walimu wanaishi kwa shida sana. Wamewahi kuchukua hatua na kuripoti katika halmashauri ya mkuranga. Waliobanika kufikisha taarifa hizo walifukuzwa kazi na tena bila kulipwa stahiki zao na bado halmashauri ya mkuranga haikushughulika na suala hilo. Mwezi huu wa tisa baada ya likizo fupi kuisha, kuna walimu wengine wanne wameondoshwa.

Sababu ni kwamba watoto wapatao asilimia kumi katika masomo yao hawajafikisha wastani. Lakini hawa ni walimu wapya, wameajiliwa miezi mitatu tu iliyopita kabla ya kufanya mitihani ya midterm. Wanawazungusha kuwalipa stahiki zao.. Uongozi unawazungusha kuwalipa stahiki zao hasa baada ya kuachishwa kazi.

Naziomba mamlaka zinazohusika, kufuatilia suala hili hasa kwa kuzingatia kwamba vijana wengi wanaofanya kazi katika taasisi za binafsi wana malengo wanataka kuyafikia pia. Tukemee vitendo vya unyanyasaji katika sehemu za kazi.

Ikiwa kuna mtu yeyote mwenye details za wapi pa kuanzia ili kuwasaidia kwa ngazi za kiserikali tafadhali toa maoni.

Asanteni sana.
Vumilieni ni mapito tu hayo, mtanzania ukimtetea usimshangae atakapokukana.
 
Baada ya kazi leo, nahitaji kufuatilia ili nipate uhakika zaidi. Lakini pia tayari nimepata contacts za baadhi ya wanyanyaswaji. Nitaweka hapa taarifa yote baadae nikishajiridhisha. Mtoa hoja naomba pia uni-pm ukishakuwa hewani. Pm yako imefungwa!
Nimejiridhisha na kwa uchache tu, madhara yatokanayo na hali iliyoelezwa na mdau alie leta hoja ni pamoja na:
1. Baadhi ya walimu hawasahihishi mitihani ya wanafunzi. Baada ya mitihani kumalizika, walimu hao hujaza alama za wanafunzi kwa kukadiria ili kukwepa alama "F" kwa wanafunzi walio wengi(Nimethibitisha hili na walengwa wamenionesha baadhi ya mitihani ya masomo hayo ikiwa hajasahihishwa lakini alama za wanafunzi zimejazwa-rejea ikiwa mitihani iliyofanyika mwezi wa nane mwaka huu). Madarasa athirika ni kidato cha kwanza na tatu.
2. Baada ya kumaliza kusahihisha, walimu hulazimika kubadilisha alama halisi za wanafunzi kwa kuingezea alama ili kuendana na matakwa ya viongozi.
3. Nidhamu mbovu kwa wanafunzi. Mwalimu(jina kapuni) anaeleza kwamba baadhi ya wanafunzi wa kike wamekuwa na tabia ya kujirekodi usiku wakiwa bwenini na kisha kurusha picha hizo kwenye mtandao wa kijamii wa tiktok. Pamekuwepo na tabia ya watoto wa kiume kuruka kuta za bwenini na kwenda nje ya shule.
4. Baadhi ya walimu kujihusisha na vitendo vya ngono na wanafunzi. Mfano; Ametajwa mwalimu mmoja ambae alikutwa akifanya mapenzi na mwanafunzi na baadae akahamishwa kwenda shule mojawapo kati ya zile tajwa na baada ya yule mwanafunzi wa kike kumaliza shule amerudishwa tena na aneendelea na hivyo vitendo na safari hii kwa siri. Imeelezwa pia kwamba mhusika huyo hana vyeti vya kitaaluma ila anabebwa na udugu kati yake na mwenye shule.
5. Viongozi wamehusishwa pia kuwataka kimapenzi walimu wa kike ili kuendelea kuwapa nafasi ya kusalia hapo kazini.
Note: Uongozi wa shule unatakiwa kuwalipa walimu stahiki zao ili kuondokana na changamoto hizi. Wazazi pia tujitahidi kukagua matokeo ya wanafunzi pindi wanaporejea wakati wa likizo na kuhakikisha wana scripts zote za masomo waliofanya.
Hayo ndio machache yaliyopatikana na nimeyaandika baada ya kujiridhisha kwamba ni sahihi. Usiku mwema!
 
Natumaini mu-wenye afya njema. Poleni na mapambano ya kila siku. Ni mara yangu ya kwanza kuandika katika jukwaa hili hasa baada ya kuwa nasoma maandiko mengi tu ya wadau mbalimbali yanayohusu mambo mengi katika jamii zetu.

Ni jukwaa pendwa pia kuwazungumzia watanzania wenzetu ambao wanashindwa kupaza sauti pale wanapokuwa wanapitia masahibu katika maeneo yao ya kazi.

Kuna shule ipo Mkuranga, umbali tu kidogo kutoka Kongowe Mbagala, inaitwa St. Matthew's. Ni shule ya sekondari japo pia wana msingi. Shule hii ni shule dada na St. Mark's- Mbagala, Ujenzi sec.-Vikindu na Imagevosa-iringa.

Ni shule kubwa yenye wastani wa wanafunzi 680-700 kwa kidato cha kwanza hadi cha sita. Kwa muda sasa mrefu sasa, walimu wanahangaika kwa kutokulipwa mishahara. Ndugu yangu wa karibu anaefanya kazi pale ameniambia "kwa ushahidi" kwamba ni zaidi ya miezi saba na hajalipwa mahahara wake.

Kila anaesimama kuhoji mshahara wake anaondolewa kazi bila hata notice. Walimu wanaishi kwa shida sana. Wamewahi kuchukua hatua na kuripoti katika halmashauri ya mkuranga. Waliobanika kufikisha taarifa hizo walifukuzwa kazi na tena bila kulipwa stahiki zao na bado halmashauri ya mkuranga haikushughulika na suala hilo. Mwezi huu wa tisa baada ya likizo fupi kuisha, kuna walimu wengine wanne wameondoshwa.

Sababu ni kwamba watoto wapatao asilimia kumi katika masomo yao hawajafikisha wastani. Lakini hawa ni walimu wapya, wameajiliwa miezi mitatu tu iliyopita kabla ya kufanya mitihani ya midterm. Wanawazungusha kuwalipa stahiki zao.. Uongozi unawazungusha kuwalipa stahiki zao hasa baada ya kuachishwa kazi.

Naziomba mamlaka zinazohusika, kufuatilia suala hili hasa kwa kuzingatia kwamba vijana wengi wanaofanya kazi katika taasisi za binafsi wana malengo wanataka kuyafikia pia. Tukemee vitendo vya unyanyasaji katika sehemu za kazi.

Ikiwa kuna mtu yeyote mwenye details za wapi pa kuanzia ili kuwasaidia kwa ngazi za kiserikali tafadhali toa maoni.

Asanteni sana.
Usitulilie sie. Walimu mliopo hapo wote kwa pamoja ACHENI KAZI! Na endeleeni kuwashawishi wengine wasiombe kufanya kazi hapo. Mkianikiwa Hilo yatatokea mambo mawili; aidha wenye shule kuwaangungia ninyi walimu na kuwalipa stahiki zenu zote au kuifunga shule na Majengo kufugia nguruwe. Ila kama hamna Umoja, ni kazi Bure kuja humu JF na kuloloma!
 
Back
Top Bottom