Show ya Lema vs Pinda featuring Makinda

Show ya Lema vs Pinda featuring Makinda

Ndo maana wahenga walisema " Hasira Hasara" Makinda amezinduka akagundua ni heri ya aibu kuliko fedheha.

Kama ni dume jike ajaribu kuweka mpira kati kwani leo CDM wamejaza ukumbi kusikiliza " HUKUMU YA KESI ALIYO BAMBIKIZIWA LEMA"

Na Mzee mzima DR. (PhD) Wilbroad Slaa yuko ndani ya bunge leo kama mgeni .......
Naona alikuja kuweka sawa timu yake....
 
hii ishu imekaa vibaya hata kwa wahisani kwani kidonda kilichoanza kupona kimefumuliwa upya.
 
Lema alisema akisha iwasilisha ataongea na waandishi wa habari...tusubiri
 
Hamaki ya Makinda ilikuwa imetoa fursa kwa CDM kukomesha huu mtindo wa Pinda wa kutoa majibu mepesi kwa masuala magumu. Sasa wanapiga danadana ili fursa hiyo ipite. CDM hisikubali kupoteza fursa hiyo adimu; mambo yakishindikana wakutane na waandishi wa habari na kuweka kila kitu wazi.
 
Kwa hiyo huo ushahidi haujawasilishwa bado? Tunasubiri utolewe bungeni na sio ofisini kwa spika.
 
Chadema wapo makini sana hongera mh.mnyika,kwa kumkumbusha spika,maaana alikua analipotezea::clap2::clap2::clap2:
 
Nitafurahi sana kama waraka huu utawekwa wazi ili wadau tuweze kuusoma.
 
Hamaki ya Makinda ilikuwa imetoa fursa kwa CDM kukomesha huu mtindo wa Pinda wa kutoa majibu mepesi kwa masuala magumu. Sasa wanapiga danadana ili fursa hiyo ipite. CDM hisikubali kupoteza fursa hiyo adimu; mambo yakishindikana wakutane na waandishi wa habari na kuweka kila kitu wazi.

Yule mama kajishtukia kuwa siku ile alikurupuka!!
 
kam ni hivyo kweli ccm wamejichimbia kaburi wao wenyewe. Huyu mama anaogopa nini. Mimi ninamfahamu nimkurupukaji sana. Wacha yamtokee puani.

huyu mama kaanza vibaya sana . Wiki mbili tu ameshaonyesha dalili za wazi za kulishindwa kuliendesha hili bunge. Sipati picha miaka mitano ijayo itakuwaje kuwaje
 
Hakuna kitu cha namna hiyo hapa bongo, lema kaambiwa apeleke ofsni

Hapa speaker amefanya kitu cha mbolea mana angepoteza muda wa watanzania
Nimegundua kuwa wewe una matatizo ya akili. Hivi unaona wabunge wako wanavyotumiana salamu za valentine ndio mambo muhimu kuliko hili la lema. Angalia bwana ushabiki wako huo kwa chama kilifilisika kama CCM.
 
Kwa hiyo huo ushahidi haujawasilishwa bado? Tunasubiri utolewe bungeni na sio ofisini kwa spika.

ushahidi bado aujawasilishwa,mama makinda ameupotezea kwa muda,hata baada ya mh.mnyika kuomba muongozo mama makinda bado anabana:kitaeleweka tu hata kama huyu mama atabana:
 
Ndugu zangu, hapa hachomoki mtu! Mtoto wa mkulima sasa hivi kiroho kinamdunda. Simmeona wenyewe leo asubuhi spika anajibaraguza eti "naendesha bunge ninavyoona inafaa". Alisema hayo baada ya kubanwa na Mh. Mnyika aseme ni lini Mh. Lema atapewa nafasi ya kuonyesha kwamba Kiongozi wetu yuko "uchi"......

Tena wale mnaoleta habari ya Rebecca hapa mnatupoteza. Tunachoongelea ni uharamu wa meya wa Arusha kwa sababu ya kura zilizopigwa. Rebecca hakupiga kura. Hata kama angekuwa amepiga kura makosa mawili yanayofanana hayafuti ukweli kwamba kuna kosa limetendeka. Hata Said Mwema analisema sana hili. Kwa maneno yake. "two wrongs dont make a right"........

Yaani, hii ni "pandora box" anayoisema Mh. J. Mbwambo kila siku.....
 
Nishaurini ninao Ushahidi wote wa mauaji ya wananchi Arusha,ninataka watanzania wajue ukweli ili tujue Lema na Pinda nani Mwongo nitumie njia gani kufikia umma.Pinda amepewa ushahidi na polisi ambao walisha edit hivyo anafikiri yeye yupo sahihi wakati amejipalia makaa ya mawe kichwani.

Nakushauri uwasiliane na ofisi ya CHADEMA uliyo karibu nayo. Wape huo ushahidi wako kisha uwaambie wauwasilishe makao makuu. Kwa kufanya hivyo itakuwa rahisi kuwafikia wahusika na kufanyiwa kazi kwa haraka. Lakini pia unaweza kuwataarifu kupitia mawasilianao yao yanayopatikana kwenye website ya CHADEMA kuwa umewasilisha ushahidi wa mauaji ya Arusha kwa mtu flani wa tawi flani ili autume makao makuu. Jitahidi ujue cheo cha huyo mtu utakaye mwachia ili ujiridhishe kama anahusika au laa! Na hapo wewe utakuwa raia mwema. Au kama unaweza upeleke mwenyewe makao makuu. Uwapatie wao watajua jinsi ya kudeal nao wakisha jiridhisha kwamba ni ushahidi makini unaojitosheleza. Huo ndo ushauri wangu pengine wengine watakushauri vizuri zaidi.
 
Back
Top Bottom