Kipara kikubwa
Member
- Jan 8, 2011
- 99
- 30
Hakuna kitu cha namna hiyo hapa bongo, lema kaambiwa apeleke ofsni
Hapa speaker amefanya kitu cha mbolea mana angepoteza muda wa watanzania
jEYKEYWAUKWELI YOU HAVE A VERY WEEK BRAIN! Suala hapa si brabra ni kuwa kosa lilifanyika na ama watendaji waliompatia PM majibu ambayo ni ya uongo hata akasema uongo bungeni ama Spika naye alikurupuka kudhani atamkomoa Lema, nimesema ktk post yangu juu kuwa busara ya jambo hili bila ushabiki, litatuliwe kiutuuzima na pengine watu wazima wamejua athari hizo ndo maana wameona si busara Lema kuwasilisha bungeni lingeleta taathira mbaya. Think as great thinker siyo shabiki. Hata kama ni Mwana CCM lazima kujua kuwa Umeya wa Arusha utatenguliwa na Mahakama kwani Mary Chatanda si diwani wa Arusha kwa mujibu wa Sheria ya serikali za mitaa na Mabaraza ya Miji. Hili lilisababishwa na uvivu wa kufikiri na kujipanga CCM uwezo wa kuchukua Umeya Arusha ungefanikiwa kama Mh Kikwete angeamua pengine kumteua Bi Batrida Burian kuwa Mbunge. Kwa Chatanda walikosea na hii ni sababu ya kutowatumia wataaalamu kwenye Chama na badala yake kukurupuka! Suala la Pinda Bungeni limeleta fedheha hata kwake, Pinda si tunayemjua asingekubali fedheha hizo, alilishwa kasa na watendaji na mi nadhani hapo anapaswa kuipitia repoer yote ya tukio la Arusha na kutaka ukweli zaidi ama atumia usalama wa Taifa wampatie taarifa za kweli. Styre hii aliitumia sana marehemu Edward Moringe Sokoine na hata Magufuli anaitumia japo pia Magufuli wakati mwingine ana mfumo wake wa kuapata na kutafuta taarifa ili kuwa na taarifa kamili bila hivo ina maana uanze kusoma wewe mwenyewe hakuna muda japo pia utamaduni wa kusoma vitu basic kama hivi hasa kwa muda mgogoro wa Arusha ulipoanza angeshakuwa na kujua ukweli upo wapi. Wtatue kiutuuzima na sisi watu wazima tutajua tu kama halijasemwa wazi basi imejulikana nani alidanganya na itajulikana kuwa kati ya hao wawili atakuwa nani ambaye amefanya suala hilo liseiwekwe wazi ni Lema ama PM ... WAKUBWA TUTAJUA na tunajua atajirekebisha kama binadamu ila si kama Spika alivosema kuwa PM hawezi kudanganya......Mi namwomba mama Makinda alinde heshima ya mwanamke.....asitekeleze matakwa ya watu..........ndoto zetu za kuwaamini wanawake zitakimbia na itakuwa amewachimbia wanawake wenzie kaburi ambalo kufukuliwa kwake ni siku ya ufufuko ama siku ya kiama. Jifunze na UGENDELAGE LUDODI, LUKAFU LULADENYEKA!