Should CHADEMA Fire Zitto?

Should CHADEMA Fire Zitto?

Should Zitto get FIRED from CHADEMA?

  • YES

    Votes: 137 65.9%
  • NO

    Votes: 57 27.4%
  • May be

    Votes: 10 4.8%
  • I don't know

    Votes: 4 1.9%

  • Total voters
    208
Status
Not open for further replies.
pumba tupu!!!!

JF baada ya 2010 imejaa wajinga na wapuuzi no wonder hakuna issues tena zaidi ya CHADEMA, CCM, Zitto, Slaa na ujinga mwingine mwingi tofauti na kabla ya 2010 ambapo kilikuwa ni kisima cha maarifa.....

big up pal.tatizo member wengi walioingia ni wanafunzi wakidato ama cha kwanza hadi cha nne.hata ukiwafahamisha na ukiwapa facts ndo wanazidi kukushambulia kwa matusi.wanafunzi hao hao wajf ndo wanaopinga kitu bila ya kutoa sababu maalum koz wengi wemepinga kitu hicho.wanasaikologia wamegundua kua akili za wanafunzi kama hawa waliomo ndani ya jf wanaziita mob saikology kwa sababu yakufuata mkumbe.kwa jina mashughuri ni akili za samaki.kama mimi ninauwezi ningeliwapiga vita wanafunzi wa lower forms kuwepo jf wanatuchafu.
 
aaag..... yaani zito ni jembe kwa ujumla . na pia ana mapungufu kama binadam mwingine. ki msingi kwa walioingia cdm juzii ndio wenye walakini
 
Ingawa siamini kwamba Zitto ni muhimu zaidi kuliko chama, ila Siungi mkono Zitto Kuondolewa kwenye chama (fired).CDM should be careful na tuhuma zinazotolewa dhidi ya kiongozi mmoja dhidi ya mwingine.Thorough investigation with impacable evidence has to be done without biasness to justify any allegation against any conspiracy.Mapambano ya Zitto na waficha fedha Uswiss ni vita vikubwa na vinamjazia maadui wa kummaliza, ukizingatia wanazo nguvu ya fedha za kumhujumu kisiasa.

Adhabu zipo nyingi, ila adhabu ya kumfukuza uanachama is not the ultemate sln for betrayal,hypocritic leaders etc Dawa nikuwatenga, kutowashirikisha na harakati na ikibidi kuwaondoa madarakana kwa mujibu wa katiba.wabakie huru kwenye chama ili kujimaliza wenyewe kisiasa.

kama ni kufukuza watu mtafukuza mpaka lini? mtafukuza wangapi? Chama kisiendeshwe kwa HISIA au UTASHI wa ubinafsi wa mtu au kikundi.
 
kama ataonekana amechukua rushwa basi chama akina namna zaidi ya kumtoa lakini kama hakuna ushahidi unajitosheleza basi no way out braaaa
 
Nashauri asiwe fired. Lazima tukubali changamoto za kuwa na mtoto ambaye si mtiifu kwa mzazi kama tulivyokuwa tunataka. Anatumiwa na CCM, yes, na sisi tumtamia kwa ajili ya CCM. Walishamwamini na ana access, this is special asset. Kwahiyo huyu ni lulu kwa kazi zetu za kiinteligensia dnhidi ya kumwondoa Mkoloni mweusi.

CHADEMA kama chama nao lazima tuwe na namna ya kupata taarifa na ziwe na self check. Majukumu kama haya hufanywa na viongozi wakuu wa kitaifa bila kuwafahamisha wanachama. Ndio maana hawamjamtimua, I guess. Kwahiyo Zitto nahisi anatumika kotekote. Hongera kwa Mwenyekiti na timu yako katika hili.

Jambo lingine kama Kiongozi wa Kitaifa apewe kazi ya Kurudisha Kigoma yote CHADEMA. Kwavile keshashtukiwa atafanya kazi kwa bidii zote. Failure of that awe fired.

Mtazamo wangu

Kiwera Mikaeli
 
kivuli cha zitto kinawatesa sana mbowe na slaa, nguvu kubwa wanayotumia kumchafua tangu autake uenyekiti wa chama ni kubwa kuliko ya kujenga chama, kibaya zaidi wanataka kummaliza kisiasa kitu walicho prove failure af wapo kama wachawi mana hawakati tamaa na kila mbinu wanayotumia. Zitto for presidency 2015
 
kivuli cha zitto kinawatesa sana mbowe na slaa, nguvu kubwa wanayotumia kumchafua tangu autake uenyekiti wa chama ni kubwa kuliko ya kujenga chama, kibaya zaidi wanataka kummaliza kisiasa kitu walicho prove failure af wapo kama wachawi mana hawakati tamaa na kila mbinu wanayotumia. Zitto for presidency 2015

Jamani wimbi la ukosefu wa ajila ni tatizo kwa sasa,watu wamenunuliwa kama nini iisshi! Nlifikili ni wanawake pekee tunaogombea wanaume kumbe adi wanaume wamevamia biashala hii..huyo Zitto sijui ana nini kaka angu nakushangaa unagombana na bulungutu la watu kuliko kuweka wazi mahaba waziwazi ni bori usingesema chochote siasa ndiyo maana sizipendi. Ivi unampenda baba yako kama unavyompenda uyu ndugu zito?
 
Hii nchi tuekezeke kufanya kazi tuacheni sihasa azisahidii kabisa..pia ushilikina sipendi
 
CCM wanaogopa kuwawajibisha mafisadi kwa sababu ni sehemu yao ni wenzao hivyo kwa wao kuwawajibisha wanaogopa kukigawa, kukiyumbisha hata kukisambaratisha Chama Chao.
Ndivyo ilivyo kwa Chadema, wanaogopa kumuwajibisha Zitto, kwa sababu ni usaliti na mengineyo ni sehemu yao, zito ni mwenzao wana hofu kama ya wenzao CCM.
The big picture tuipatayo hapa ni kuwa hakuna Chama chenye uwezo wa kufanya maamuzi, yawe magumu au mepesi, vyama vyetu vinachoweza kufanya ni kushambuliana, kukosoana na kujitetea tu, baasi.

naamini cDM itafanya maamuzi hayo
 
huwezi kumkashifu kiongozi wa chama kwa faida zako.yaani zzk amekuwa mbaya kuliko ccm
 
Mtoto akiuliza swali la msingi hapaswi kujibiwa? Yaani yote hii ni katika kumtetea slaa? huu mgogoro si Zitto pekee babu ni mshiriki kwa asilimia 110%; walioshikwa akili watu kama wewe ni mmoja mimi naangalia pande zote za shilingi.

Chama
Gongo la mboto DSM
Huwezi kuangalia pande zote za shilingi kwenye issue hii,huo ni uongo,wewe ni anti Slaa hilo halina ubishi,danganya wengine siyo mimi.

Issue hii kama unaiangalia kwa maslahi ya chama husika,yani chadema,basi huwezi kuona kama Dr Slaa ndiyo tatizo.Wewe ni miongoni mwa wale wanaompinga kwa kutumia vigezo vya dini,umri na ukanda.Hivyo ni vigezo muflisi,na ndivyo ambavyo Zitto amekuwa akivitumia yeye na masalia.Hilo halina ubishi.

Zitto alipoamuwa kwamba anagombea urais,aliamuwa kushirikiana na nyie ccm kuitumia hoja ya kibaguzi ya umri,pia na hoja nyingine za kibaguzi za ukanda na udini.

Kwa kupitia wana ccm kama Nape,Januari Makamba pamoja na kina Shigela na Mwigulu Nchemba.Wewe ni gamba halafu unataka kusema unaingalia issue ya chadema pande zote za shilingi?Usitype kwasababu una access ya mtandao na vidole,shirikisha ubongo,ama hata ukitaka kudanganya usitumie akili ya kitoto.

Tatizo la ubinafsi na kutokuwa mvumilivu ni la Zitto,na pia nimegunduwa ni mbaguzi.Matatizo hayo si madogo.Wakati viongozi wenzake wanajitahidi kujenga chama yeye anavuruga kwa maslahi yake binafsi.Haiwezekani nyie magamba muwe mnamfagilia kwasababu toka lini mkakippenda chama cha upinzania kama si kwa maslahi ya chama chenu?
 
Mtoto akiuliza swali la msingi hapaswi kujibiwa? Yaani yote hii ni katika kumtetea slaa? huu mgogoro si Zitto pekee babu ni mshiriki kwa asilimia 110%; walioshikwa akili watu kama wewe ni mmoja mimi naangalia pande zote za shilingi.

Chama
Gongo la mboto DSM

Umekurupuka kijana!angalia post ilianzishwa lini halafu urudi utoe hoja yako na baada ya hapo upige kura yako hapo juu.
 
jamaa afukuzwe kabisaa coz kama kuvumiliana kumepita kiasi!ashavumiliwa vya kutosha sana, ameropoka sana akidhani ndio democrasia!watever the case wamfunue kila kitu alichowahi kufanya ili watz wajue kua CDM ndicho chama pekee kinachoweza kusimamia maadili na ukweli na kwamba mtu ndani ya CDM hawezi kua maarufu kuliko chama.Wamfungie jiwe la kusagia na kumtosa baharini kama alivosema Jesus.(hypothetically)

chama cha demokrasia na maendeleo!!!taasisi ya malaika Mbowe na Slaa!!!waguse uone cha motooooo!!!
 
Umekurupuka kijana!angalia post ilianzishwa lini halafu urudi utoe hoja yako na baada ya hapo upige kura yako hapo juu.

Siangalii ilianzishwa lini naangalia imerudishwa lini; kumbe pro slaa vita dhidi y Zitto mlianza siku nyingi sana hivi sasa unafiki wenu ndio unajidhihirisha wazi

Chama
Gongo la mboto DSM
 
Last edited by a moderator:
Huwezi kuangalia pande zote za shilingi kwenye issue hii,huo ni uongo,wewe ni anti Slaa hilo halina ubishi,danganya wengine siyo mimi.

Issue hii kama unaiangalia kwa maslahi ya chama husika,yani chadema,basi huwezi kuona kama Dr Slaa ndiyo tatizo.Wewe ni miongoni mwa wale wanaompinga kwa kutumia vigezo vya dini,umri na ukanda.Hivyo ni vigezo muflisi,na ndivyo ambavyo Zitto amekuwa akivitumia yeye na masalia.Hilo halina ubishi.

Zitto alipoamuwa kwamba anagombea urais,aliamuwa kushirikiana na nyie ccm kuitumia hoja ya kibaguzi ya umri,pia na hoja nyingine za kibaguzi za ukanda na udini.

Kwa kupitia wana ccm kama Nape,Januari Makamba pamoja na kina Shigela na Mwigulu Nchemba.Wewe ni gamba halafu unataka kusema unaingalia issue ya chadema pande zote za shilingi?Usitype kwasababu una access ya mtandao na vidole,shirikisha ubongo,ama hata ukitaka kudanganya usitumie akili ya kitoto.

Tatizo la ubinafsi na kutokuwa mvumilivu ni la Zitto,na pia nimegunduwa ni mbaguzi.Matatizo hayo si madogo.Wakati viongozi wenzake wanajitahidi kujenga chama yeye anavuruga kwa maslahi yake binafsi.Haiwezekani nyie magamba muwe mnamfagilia kwasababu toka lini mkakippenda chama cha upinzania kama si kwa maslahi ya chama chenu?

Kwa hiyo wewe unaangalia pande ipi ya shilingi? Ni afadhali ya Zitto ameweka wazi azma yake kuliko huyo mnafikia aliyeanzisha mtandao wa kujichagua

Chama
Gongo la mboto DSM
 
Last edited by a moderator:
Demokrasia katika chama ni pamoja na kusikia maoni ya wanachama, wafuasi na wapenzi. Demokrasia pia ina misingi na mipaka yake.
Chama kinapoanza kufanya shughuli zake bila kufuata katiba, kanuni na taratibu bali kwa kufuata upepo wa mawazo na kura za kwenye mitandao ambazo hata hazijahakikiwa inakuwa ni kuvuka mipaka ya demokrasia na kuendesha chama bila misingi ya katiba, kanuni na taratibu.

Hii inakuwa kama kuendesha chama kwa misingi ya 'kangaroo court' na kuitumia vibaya falsafa ya chama kama ilivyoanishwa katika sura ya 3.1, 3.2 ndani ya katiba ya chama.

Hata kama chama kitafanya maamuzi yake kwa kuwa 'influenced' na upepo wa mawazo na kura kutoka humu jf bado itakuwa ni maamuzi ya ulevi wa mawazo kwa sababu hata wengi wanaopiga kura hapa hawana ukweli (fact) achilia mbali ukweli hasa (absolute fact) wa matendo na nyendo za Mh Zitto Kabwe katika shughuli za chama.

Anyway, hii ndiyo demokrasia ya chama (The people's power)
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom