Missile of the Nation
JF-Expert Member
- May 24, 2018
- 13,502
- 51,098
Katika hali inayoonekana ni muendelezo wa maisha magumu kwa wananchi.
Hospitali ya Kairuki nchini imekuja na utaratibu wa kushangaza wa kutoza malaki ya hela kwa siku kwa mtu atakayeenda katika hospitali hiyo kutibiwa ugonjwa wa mifumo ya hewa.
Katika utaratibu huo mgonjwa yeyote atakayekwenda kupata huduma ya ugonjwa wa mfumo wa hewa, Hospitali hiyo itamtoza shilingi Laki sita kwa siku (600,000)kama hatahitaji huduma ya Ventilator. Na kama atahitaji huduma ya ventilator basi atalazimika kulipa shilingi Laki nane na nusu (850,000).
Nilipokuwa naongea na wananchi kuhusiana na suala hili, wengi wameonyesha kuwa na wasiwasi kuwa hospitali hiyo inataka kuwakimbiza wananchi wenye matatizo hayo wasiende kwenye hospitali hiyo. Na kwa kuwa ni kinyume cha maadili ya kidaktari kukataa kuhudumia mgonjwa basi hospitali hiyo inataka kukwepa kuhudumia wananchi katika maradhi hayo kijanja.
Kwa kweli hili jambo ni la kusikitisha na la kutia aibu kwa wamiliki na waendesha hospitali hiyo.
Kwanza kuna maswali ya kujiuliza, kwa nini hatua hii ya ajabu ije kwenye kipindi hiki cha Korona?.
Je, ni kweli kuwa kwa utaratibu huu hospitali hiyo inafukuza wananchi wanaohitaji huduma hiyo kijanja kwa kisingizio cha pesa?
Na kama hailengi kukwepa wajibu wa kuhudumia wagonjwa, je wamiliki wa hiyo hispitali wameamua kuigeuza Korona kuwa dili, yaani kuvuna mamilioni ya pesa kupitia wananchi wanaohitaji huduma ya hospitali?
Je, kuna baraka za serikali katika hatua hii, ili kulazimisha wananchi wafanye tiba mbadala majumbani ili takwimu halisi za wenye ugonjwa wa Korona zisipatikane?
Tunaitaka serikali kupitia Waziri wa Afya aingilie kati suala hili.
Tunajua serikali inayo mamlaka ya kuingilia kati utendaji wa hospitali zote nchini katika mfumo wao wa utoaji huduma nchini.
Tunamtaka Waziri wa Afya aje public atueleze kama anaunga mkono kitendo kama hiki cha hospitali ya Kairuki ili hiki walichokifanya kisije kikageuka kuwa ni mfano wa hospitali nyingine nao kufanya kama wao.
Ubaya wa kitendo cha hospitali ya Kairuki, hawajaspecify hata ugonjwa husika, wametumia jina la jumla la "magonjwa ya mfumo wa hewa!" . Kwa hiyo watoto wetu wachanga wakipata nimonia ya kawaida kabisa isiyokuwa hata hiyo Korona ndo mnataka kuwatoza Laki nane na nusu kwa siku? - Hii hospitaki inataka tupoteze hata watoto wetu kwa sababu ya watu wenye mawazo. mfu wachache!
Tunataka hii hospitali ibadirishe huu utaratibu maramoja!. Mwanzilishi wa hii hospitali hayati profesa Kairuki atakuwa anajigeuza kaburini sasa kwa baadhi ya cowards wachache kutaka kuwatosa wananchi katika kipindi hiki kigumu cha kiafya duniani!
Hili halikubaliki:
Angalia fomu hii hapa chini kutoka hospitali hiyo.
Hospitali ya Kairuki nchini imekuja na utaratibu wa kushangaza wa kutoza malaki ya hela kwa siku kwa mtu atakayeenda katika hospitali hiyo kutibiwa ugonjwa wa mifumo ya hewa.
Katika utaratibu huo mgonjwa yeyote atakayekwenda kupata huduma ya ugonjwa wa mfumo wa hewa, Hospitali hiyo itamtoza shilingi Laki sita kwa siku (600,000)kama hatahitaji huduma ya Ventilator. Na kama atahitaji huduma ya ventilator basi atalazimika kulipa shilingi Laki nane na nusu (850,000).
Nilipokuwa naongea na wananchi kuhusiana na suala hili, wengi wameonyesha kuwa na wasiwasi kuwa hospitali hiyo inataka kuwakimbiza wananchi wenye matatizo hayo wasiende kwenye hospitali hiyo. Na kwa kuwa ni kinyume cha maadili ya kidaktari kukataa kuhudumia mgonjwa basi hospitali hiyo inataka kukwepa kuhudumia wananchi katika maradhi hayo kijanja.
Kwa kweli hili jambo ni la kusikitisha na la kutia aibu kwa wamiliki na waendesha hospitali hiyo.
Kwanza kuna maswali ya kujiuliza, kwa nini hatua hii ya ajabu ije kwenye kipindi hiki cha Korona?.
Je, ni kweli kuwa kwa utaratibu huu hospitali hiyo inafukuza wananchi wanaohitaji huduma hiyo kijanja kwa kisingizio cha pesa?
Na kama hailengi kukwepa wajibu wa kuhudumia wagonjwa, je wamiliki wa hiyo hispitali wameamua kuigeuza Korona kuwa dili, yaani kuvuna mamilioni ya pesa kupitia wananchi wanaohitaji huduma ya hospitali?
Je, kuna baraka za serikali katika hatua hii, ili kulazimisha wananchi wafanye tiba mbadala majumbani ili takwimu halisi za wenye ugonjwa wa Korona zisipatikane?
Tunaitaka serikali kupitia Waziri wa Afya aingilie kati suala hili.
Tunajua serikali inayo mamlaka ya kuingilia kati utendaji wa hospitali zote nchini katika mfumo wao wa utoaji huduma nchini.
Tunamtaka Waziri wa Afya aje public atueleze kama anaunga mkono kitendo kama hiki cha hospitali ya Kairuki ili hiki walichokifanya kisije kikageuka kuwa ni mfano wa hospitali nyingine nao kufanya kama wao.
Ubaya wa kitendo cha hospitali ya Kairuki, hawajaspecify hata ugonjwa husika, wametumia jina la jumla la "magonjwa ya mfumo wa hewa!" . Kwa hiyo watoto wetu wachanga wakipata nimonia ya kawaida kabisa isiyokuwa hata hiyo Korona ndo mnataka kuwatoza Laki nane na nusu kwa siku? - Hii hospitaki inataka tupoteze hata watoto wetu kwa sababu ya watu wenye mawazo. mfu wachache!
Tunataka hii hospitali ibadirishe huu utaratibu maramoja!. Mwanzilishi wa hii hospitali hayati profesa Kairuki atakuwa anajigeuza kaburini sasa kwa baadhi ya cowards wachache kutaka kuwatosa wananchi katika kipindi hiki kigumu cha kiafya duniani!
Hili halikubaliki:
Angalia fomu hii hapa chini kutoka hospitali hiyo.