Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,813
- 11,991
Siku chache baada ya Mwanachama wa JamiiForums.com kudai kuwa kuna changamoto ya lifti katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda Bugando iliyopo Jijini Mwanza, hoja hiyo imejibiwa na uongozi wa Bugando.
Kusoma zaidi kuhusu Hoja ya Mdau Bonyeza hapa - Uongozi wa Hospitali ya Bugando chukueni hatua za haraka kurekebisha lifti zenu kabla hazijaleta madhara
Tamko rasmi la Bugando hili hapa:
22 Machi, 2024 Mwanza.
Uongozi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda Bugando unapenda kuwatoa hofu Wananchi na kutoa ufafanuzi kuhusiana na taarifa zinazosambaa katika mitandao ya kijamii kupitia kurasa za JAMII FORUMS zikiutaka Uongozi wa Hospitali ya Bugando kuchukua hatua za kurekebisha lifti zake.
Hospitali ya Bugando ina utaratibu wa kufanya marekebisho makubwa ya lifti zake kwa utaratibu uliopangwa na kuwa na wasimamizi wa lifti (Lift attendants) wanaohakikisha lifti zinafanya kazi.
Aidha, kama ilivyo utaratibu wa matumizi ya lifti Duniani kote, ndani ya lifti zetu kuna namba za simu zinazomuwezesha mtumiaji wa lifti kuweza kuwasiliana na msimamizi wa lifti pindi anapopata changamoto katika lifti hizo.
Hivi karibuni hatujapata changamoto ya lifti kutokufanya kazi, hivyo tunapenda kuwahakikishia Wananchi wote na watumiaji wa lifti kuwa lifti zinafanya kazi vizuri.
Imetolewa na;
Idara ya Mawasiliano na Uhusiano kwa Umma
HOSPITALI YA RUFAA YA KANDA BUGANDO
Kusoma zaidi kuhusu Hoja ya Mdau Bonyeza hapa - Uongozi wa Hospitali ya Bugando chukueni hatua za haraka kurekebisha lifti zenu kabla hazijaleta madhara
Tamko rasmi la Bugando hili hapa:
22 Machi, 2024 Mwanza.
Uongozi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda Bugando unapenda kuwatoa hofu Wananchi na kutoa ufafanuzi kuhusiana na taarifa zinazosambaa katika mitandao ya kijamii kupitia kurasa za JAMII FORUMS zikiutaka Uongozi wa Hospitali ya Bugando kuchukua hatua za kurekebisha lifti zake.
Hospitali ya Bugando ina utaratibu wa kufanya marekebisho makubwa ya lifti zake kwa utaratibu uliopangwa na kuwa na wasimamizi wa lifti (Lift attendants) wanaohakikisha lifti zinafanya kazi.
Aidha, kama ilivyo utaratibu wa matumizi ya lifti Duniani kote, ndani ya lifti zetu kuna namba za simu zinazomuwezesha mtumiaji wa lifti kuweza kuwasiliana na msimamizi wa lifti pindi anapopata changamoto katika lifti hizo.
Hivi karibuni hatujapata changamoto ya lifti kutokufanya kazi, hivyo tunapenda kuwahakikishia Wananchi wote na watumiaji wa lifti kuwa lifti zinafanya kazi vizuri.
Imetolewa na;
Idara ya Mawasiliano na Uhusiano kwa Umma
HOSPITALI YA RUFAA YA KANDA BUGANDO