Shinyanga: Mume aua mke wake kwa Panga akimtuhumu kusaliti Ndoa yao

Unawekaje mambo sawa na msaliti ndugu? Kuna watu wanafanya umalaya bila kujali mioyo ya wenza wao...wakatwe tu mapanga hakuna namna
... ni ujinga kumuua mkeo/mumeo kwa sababu ya kinachoitwa usaliti kwenye ndoa! Achaneni kwa amani kila mtu aendelee na maisha yake. Ya nini kuharibiana maisha kuozea jela?
 
Sasa mtu kama huyu ndio anakufumania live siju kitatokea nini,ila wake za watu na nyinyi tulieni majumbani mwenu...
 
Eti atafikishwa mahakamani upelelezi ukikamilika. Mtuhumiwa kaua mbele ya balozi, akajipeleka mwenyewe Polisi kuwaambia nimeua, sasa upelelezi gani wanautaka?

Maiti ipo, panga lipo, balozi yupo, mtuhumiwa yupo!

Polisi bhana!
Sheria inawataka kujijakikishia pasi na shaka kwamba hayo ndo yaliyotokea.
 
Ugumu wa kesi ni mashahidi wengi wameona ila watakaokuwa tayari kutoa ushahidi ndio mtihani unaanzia hapo hasa ukizingatia hii kesi itasomwa mahakama za kawaida wakati upelelezi unaendea then baadae inahamishiwa Mahakama kuu ukute hiyo mahakama kuu ipo mwanza nani ataacha kazi zake asafiri kwa garama zake na ajitegemee malazi?

Siku ya tukio watu hujaa ila wakiona polisi walioshuhudia tukio likitendeka wanaingia mitini
...ila wakiona polisi walioshuhudia tukio...! POLISI WANASHUHUDIAJE TUKIO?
 
Kesi ni process mkuu lazima watafutwe mashahidi zaidi ya mmoja aliyeshuhudia tukioa sio kuambiwa, Polisi walienda baada ya mtuhumiwa kujipeleka so lazima wajiridhishe watachoiambia mahakama, na ushahidi wao usiache shaka.
Aaa bana mapolisi nao waache ujinga, sasa panga, mashahidi, maiti, mtuhumiwa, vyote vipo wanakwama wapi???
 
Back
Top Bottom