FESTO Maganga Mkazi wa Seguchini, Kata ya Nala, Wilaya ya Dodoma Mjini, anadaiwa kumuua mkewe na mama mkwe wake, kisha na yeye kuuawa na wananchi. Tukio hilo limetokea jana Jumapili Januari 28, 2024 majira ya saa 10 :30 jioni katika Mtaa wa Seguchini.
Akizungumza na chombo kimoja cha habari, mmoja wa ndugu za marehemu hao, Samwel Lengole amesema wiki iliyopita mama mkwe, ambaye ni mama wa mke wa mtuhumiwa, Anna Ngalai alikwenda kwa mwanaye Maria Joseph kusalimia.
Hata hivyo, amesema (jana saa 10.30 kuelekea saa 12 jioni) pasipo kufahamu ni nini kilitokea, ilikutwa miili ya mama na mtoto wake jikoni ikiwa imechomwa na kitu chenye ncha kali shingoni.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Martin Otieno amethibitisha tukio hilo akisema taarifa atazitoa baadaye.
Source - Nipashe
Akizungumza na chombo kimoja cha habari, mmoja wa ndugu za marehemu hao, Samwel Lengole amesema wiki iliyopita mama mkwe, ambaye ni mama wa mke wa mtuhumiwa, Anna Ngalai alikwenda kwa mwanaye Maria Joseph kusalimia.
Hata hivyo, amesema (jana saa 10.30 kuelekea saa 12 jioni) pasipo kufahamu ni nini kilitokea, ilikutwa miili ya mama na mtoto wake jikoni ikiwa imechomwa na kitu chenye ncha kali shingoni.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Martin Otieno amethibitisha tukio hilo akisema taarifa atazitoa baadaye.
Source - Nipashe