Shinyanga Mjini Vs Tabora Mjini

Shinyanga Mjini Vs Tabora Mjini

Vichaa wengi huja kwa usafiri wa treni mkuu maana Tabora inahudumia karibia mikoa yote ya magharibi na Mwanza na mara hivyo Vichaa hupanda tu kwenye trains basi hujikuta wapo Tabora, na kwakuwa Tabora gari moshi huchelewa sana kuondoka (kwani hapa hufanyika kwanza shanting) hivyo abiria hulazimika kushuka kwanza na ndipo hapo hata vichaa hushuka na kuanza kulandalanda huku na huko.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hao vichaa wanapanda treni bure!? Mbona huko unakosema wanatoka (mwanza n.k) idadi ya vichaa ni wachache kuliko hapo tabora?
Punguzeni bangi na uchawi. Leo hii mnazidiwa kwa kila kitu na mkoa wa Kigoma (manispaa) kuanzia hotels kali, barabara, kumbi za starehe na huduma nyinginezo...amkeni.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huo ukame Tabora uko sehemu gani?
Eneo kame Tabora ni wilaya Igunga tu.

Sehemu zingine zote zina maji mengi sana chini tena maji laini.

Tabora ni mkoa ambao hauna mito lakini una mikondo ya maji mikubwa sana ambayo haina mchanga ( mbuga)

Hivi sehemu kame inaweza kuwa ya nne kwa uzalishaji wa mpunga nchini ?

Tabora karibu kila familia ina kisima chake cha maji jirani na nyumbani huo ukame utoke wapi ?

Sent using Jamii Forums mobile app
Alipitiwa huyo.
Na Igunga ni kame ila wanazalisha mpunga hujawahi ona utadhani umefika Kyela
 
Wewe muongo na nimnafik
Sasa ukisema barabara shinyanga nzuri Tabora wasemeje eti taa za barabarani unashangaa hilo je ungefika Tabora uone mpaka taa za kuongozea magari.
Tatizo ushamba mwingi sana hapo shinyanga.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mzee sasa huu ni ubishani wa kwenye Gahawa, kama tatizo ni traffic lights hata Kahama zipo tena ni wilaya tu.

Let's argue kuhusu vitu vya maana, kama mademu wa bila kutongoza Ipuli na madem wa kuhonga wanaume wa Ngokolo A na B
 
Barabara za lami Tabora zimekuwepo toka kipindi cha Mzee Mwinyi na sasa hivi kila mtaa ni lami tu

Sent using Jamii Forums mobile app
Kuna mkoa gani Tanzania hauna lami kila kona?
Tena Tabora, Shinyanga,Geita, Katavi, Simiyu, Singida, Dodoma, Songwe n.k walikuwa na project mpya za kujengewa barabara za mitaa zilizokuwepo zimevunjwa na kupigwa upya na mikoa mipya ambayo haikua na barabara za mitaa imekuwa nazo.
 
Ushuhuda wangu mimi naona Tabora bora kuliko kwa wasukuma Shinyanga. Sema tatizo la Tabora ardhi kame sana. Wanyamwezj wajanja na wamechangamka. Ila watani zao wasukuma wanazingua. Mfano mzuri si wenye lugha nzuri ya biashara aisee. Ila all in all penye ugumu ndiyo pakutoboa.
Wasukuma na Wanyamwezi ni ndugu na wanaongea lugha moja
Sio watani
Watani zao watu wa pwani

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Taa ya kuongozea magari hata kahama ipo wala co ajabu,,,Shinyanga wamewekewa rami sio chin ya 50 kilometres i think,, taa za barabara mpya na bado wanaenderea kuweka, tabora je?


Hebu nitajie viwanda vitatu tu mlivyonavyo huko ubangini?? Shinyanga nirienda napajua na tabora nirishawai kwenda.


Post ya juu naongeza na kiwanda cha bati kirichoko kahama,,,tabora je mnacho??

Nitajie viwanda vitatu jomba!
Tofautisha L na R

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Umemaliza kila kitu
Shinyanga mjini hovyo sana.

Hata ukitaka breakfast hakuna sehemu insyoeleweka ukanywa chai uka enjoy.

Chakula cha uhakika ni mchana tu tena sehemu moja tu ambayo wakati mwingine pia wanapika vibaya tu.

Ni sehemu ambayo bara bara ni chafu zimejaa udongo ijapokuwa ni za lami.

Usafiri wa tax ni wa shida,wafanya biashara hii wana nyodo na waongo.Unakubaliana nae unaamka mapema kuwahi basi,ikinyesha mvua tu anazima simu.

Biashara ni ngumu sana shinyanga,nadhani ni sehemu mojawapo ngumu Tanzania.

Maji ya ziwa yapo ila wanachanganya na maji ya bwawa chafu sana la ning"hwa na kuyafanya yawe ya chumvi na mabaya sana.

Bora Tabora sana utapata hata bookshop ya kueleweka,library nzuri,taasisi za mafunzo zinazoeleweka,na bara bara safi zisizo na mchanga

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wewe hao vichaa sio bangi ni ulozi
Nimekaa hapo Tabora miaka minne nimeuliza sana hilo wamenimbia hao ni wezi wakiiba wanarogwa ndio maana unaona vichaa wengi

Makokora
Ipuli
Isevya
Tabora Town

Watu watabora wanyamwezi waswahili sana

Sent using Jamii Forums mobile app
Bangi haiwezi kufanya mtu kua kicha ila labda akiwa anadalili za ukochaa ama anamikataba na majini ambayo hayataki harufu hiyo kabisa
 
Comment yako nzuri kwa matumizi ya baadae na inafaa kwa ajili ya ku-screen shot kwa kumbukumbu ya baadae, upiga mulemule maana vijana wengine huangalia madhari ya mji au huduma zitakazoweza kuwafanya wake eneo hilo comfortably pasipokuangalia changamoto zilizopo na kuzitafutia mradi.

Kuna mdau amesema Shinyanga pa hovyo hakuna huduma za chakula labda mchana, kwa kauli hii tayari wazo la biashara limepatikana kwa mtu kuanzisha baba lishe ila baada ya kufanya uchunguzi wa kwanini mchana kuna chakula alafu usiku magumashi
Sababu wanalala mapema,saa moja unusu,kuondoa stendi pale mjini Kati kumechangia kuua mji wa shinyanga ,hakunaga Tena amsha amsha Kama zamani,
 
Back
Top Bottom