Shinyanga: Kituo cha Afya chagundulika kuhifadhi Damu kwenye Majokofu ya nyumbani

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,379
8,123
Mkurugenzi wa huduma za afya ustawi wa jamii na lishe Ofisi ya Rais TAMISEMI Dkt.Rashid Mfaume amebaini ukiukwaji wa manunuzi ya vifaa ikiwamo jokofu za kuhifadhia damu katika kituo cha afya Mwalugulu, katika halmashauri ya Msalala wilayani Kahama mkoani Shinyanga.

Dkt. Mfaume amebaini hayo wakati wa kukagua shughuli za uendeshaji na usimamizi wa afya katika kituo hicho akiwa ameambatana na timu ya afya, ustawi wa jamii na lishe kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI ambapo majokofu mawili yaliyonunuliwa katika kituo hicho kwa ajili ya kuhifadhi damu yakabainika kuwa ya matumizi ya nyumbani.

“Ni majokofu kwa ajili ya kufungia nyanya,karoti na parachichi na wataalamu wametuthibitishia kuwa haya sio majokofu ya damu, huyu mzabuni tumemlipa bila kukagua tumeagiza majokofu ya kutunzia damu tumeletewa majokofu ya matunda” Amesema Dkt. Mfaume.

Kufuatia hatua hiyo Dkt. Mfaume ameelekeza mfamasia wa halmashauri kuondolewa kwenye nafasi yake kwa kutoa taarifa ya uongo wakati wa ukaguzi wa vifaa huku akielekeza kuonywa kwa maandishi kwa wajumbe wa timu ya usimamizi wa shughuli za Afya ya Halmashauri (CHMT) ya Msalala.

JAMBO TV
1712907837515.png
1712907844498.png
 
Inafikirisha. Ama contract yao ilikuwa inasema mzabuni alete jokofu lolote tu? Maana had linapokelewa ina maana walikuwa wamelizika nalo
 
Tunawapongeza hao Watumishi Kwa kujiongeza.Wanaolaumu walipeleka majokofu yanayohitajika?
Hawakujingeza, ni uzembe tu. Rudia kusoma vizuri:

“Ni majokofu kwa ajili ya kufungia nyanya,karoti na parachichi na wataalamu wametuthibitishia kuwa haya sio majokofu ya damu, huyu mzabuni tumemlipa bila kukagua tumeagiza majokofu ya kutunzia damu tumeletewa majokofu ya matunda” Amesema Dkt. Mfaume.
 
Lakin wewe si ndo unasifia Kila siku humu... Hakuna kama ccm. Madudu yote yanayofanyika humu nchini ya wizi wa Mali za uma. Huwezi tenganisha na ccm aisee
Sasa CCM hapo ina kosa lipi?

Hivi hizo shule mlienda kusomea ujinga?
 
Back
Top Bottom