Shibuda aishangaa demokrasia ya CHADEMA

Shibuda aishangaa demokrasia ya CHADEMA

CHADEMA lazima muwe makini na uwezo wa kujuwa kwamba hii stori imetengenezwa na magazeti kutimiza matakwa ya ccm. Kwanza angalia magazeti (Jambo Leo, Uhuru) yenyewe yaliyoandika yanamilikiwa na nani. Je ni kweli kasema wapinzani hawawezi kuchukuwa nchi au kura za wanachama wa CHADEMA hazitoshi? BAVICHA wanapiga kelele kutokana na walichosoma katika magazeti na sio alichosema Shibuda. Kilichotekea ni taasisi ya utawala bora "Good Governance …" ilialikwa kwenda kutoa ripoti ya tathmini yake kwenye hicho kikao na hii taasisi inaalikwa sehemu nyingi, shibuda ni mmoja ya watu waliopo ndani ya hiyo taasisi. Baada ya maongezi rasmi kulikuwa na utani kati ya kikwete na shibuda. Katika huo utani shibuda alisema atagombea urais kwa tiketi ya mgombea binafsi na sio kwa tiketi ya CHADEMA na akamuomba kikwete amuunge mkono. Lakini magazeti kwasababu ya malengo yao binafsi au ya CCM yaliamua kupindisha kauli hii na kusema Shibuda kaamua kugombea kupitia CHADEMA, na watu hao hao ndio walioleta stori hiyo jamii forum. Baada ya Zito kutangaza kugombea uraisi na kupingwa na Mtei inaonekana CCM wameshagundua udhaifu wa CHADEMA; hawataki mgombea atoke sehemu nyingine isipokuwa kaskazini, kwahiyo kutakuwa na juhudi za kulipigia mstari swala hili mpaka nchi yote ielewe kwamba kama wewe sio mchaga au hutoki kaskazini basi uraisi huruhusiwi kugombea kupitia CHADEMA. Kwahiyo kabla haujaanza ushabiki usiokuwa na umakini kwa kupinga mtu tu kwasababu kasema atagombea uraisi, lazima uwe makini kujuwa labda unawafaidisha CCM. Huyo Shibuda anaelewa CHADEMA hawawezi kupitisha jina lake kugombea uraisi labda awe mgombea binafsi kama alivyomwambia kikwete. Kwahiyo hiyo kauli yakusema atagombea kupitia CHADEMA imetengenezwa KUGOMBANISHA WACHAGA NA WASUKUMA KAMA SIO WATANZANIA WOTE. Kwahiyo kuweni makini, wanaosoma hapa sio tu wachaga bali na kabila nyingine. Hata ukitoa comment unajiita WAMBURA au MASANJA bado tu watu watajuwa ni mchaga kwasababu ya unavyokuwa MWEPESI NA HARAKA ya kupinga watu wa kabila nyingine. Msije mkafanya CHADEMA ionekane haina Demokrasia.

Hivi ni virus vya kisiasa,
makala nzuri yenye ufafanuzi mzuri inapoingizwa kejeli za ukabila inatia shaka na maandiko ya mwandishi kama kweli lengo lake ni keulewesha wale wasiolewa ama kueneza hoja zake mgando. Nafasi ya mgombea uaraisi ni Moja, mwenzetu na kundi lako lililojikita kwenye ukabila unataka awe nani, kinyume na yule aliyegombea na wenzake wengi na kuibuka mshindi? mimi si mchaga na wala sitoki kaskazini kama ulivyojaribu kujieleza hapa, lakini uliyoyaongea yanaongelewa sana na wanamagamba katika harakati zao za kipropaganda walizojifunza pale magogoni, Isaraeli na urusi. Ni nani asiye wa kaskazini aliyeomba kugombea uraisi akashindwa kupewa nafasi kwa sababu tu yeye sio wa kaskazini ama Mchaga?
CDM ni chama cha watanzania na wanachama wake tunajua kuwa yeyote aliye mwanachama ana haki kamili ya kugombea nafasi yoyote katika chama na anao uwezo wa kushinda kama wanachama wenzake watamuona anaweza kuwaongoza. epuka hizo siasa za propaganda za kisoshalist hazikusaidii kabisa.
 
Kama magezeti ya ccm yamesema uwongo, basi ni jukumu la Shibuda kusahihisha. Kitendo cha yeye kuendelea kukaa kimya tafsiri yake ni kwamba ameafiki kila neno liloandikwa kwenye hayo mageziti. CHADEMA wana haki ya kumkata shingo unless aseme kuwa magezeti yamepotosha.
 
CHADEMA lazima muwe makini na uwezo wa kujuwa kwamba hii stori imetengenezwa na magazeti kutimiza matakwa ya ccm. Kwanza angalia magazeti (Jambo Leo, Uhuru) yenyewe yaliyoandika yanamilikiwa na nani. Je ni kweli kasema wapinzani hawawezi kuchukuwa nchi au kura za wanachama wa CHADEMA hazitoshi? BAVICHA wanapiga kelele kutokana na walichosoma katika magazeti na sio alichosema Shibuda. Kilichotekea ni taasisi ya utawala bora "Good Governance …" ilialikwa kwenda kutoa ripoti ya tathmini yake kwenye hicho kikao na hii taasisi inaalikwa sehemu nyingi, shibuda ni mmoja ya watu waliopo ndani ya hiyo taasisi. Baada ya maongezi rasmi kulikuwa na utani kati ya kikwete na shibuda. Katika huo utani shibuda alisema atagombea urais kwa tiketi ya mgombea binafsi na sio kwa tiketi ya CHADEMA na akamuomba kikwete amuunge mkono. Lakini magazeti kwasababu ya malengo yao binafsi au ya CCM yaliamua kupindisha kauli hii na kusema Shibuda kaamua kugombea kupitia CHADEMA, na watu hao hao ndio walioleta stori hiyo jamii forum. Baada ya Zito kutangaza kugombea uraisi na kupingwa na Mtei inaonekana CCM wameshagundua udhaifu wa CHADEMA; hawataki mgombea atoke sehemu nyingine isipokuwa kaskazini, kwahiyo kutakuwa na juhudi za kulipigia mstari swala hili mpaka nchi yote ielewe kwamba kama wewe sio mchaga au hutoki kaskazini basi uraisi huruhusiwi kugombea kupitia CHADEMA. Kwahiyo kabla haujaanza ushabiki usiokuwa na umakini kwa kupinga mtu tu kwasababu kasema atagombea uraisi, lazima uwe makini kujuwa labda unawafaidisha CCM. Huyo Shibuda anaelewa CHADEMA hawawezi kupitisha jina lake kugombea uraisi labda awe mgombea binafsi kama alivyomwambia kikwete. Kwahiyo hiyo kauli yakusema atagombea kupitia CHADEMA imetengenezwa KUGOMBANISHA WACHAGA NA WASUKUMA KAMA SIO WATANZANIA WOTE. Kwahiyo kuweni makini, wanaosoma hapa sio tu wachaga bali na kabila nyingine. Hata ukitoa comment unajiita WAMBURA au MASANJA bado tu watu watajuwa ni mchaga kwasababu ya unavyokuwa MWEPESI NA HARAKA ya kupinga watu wa kabila nyingine. Msije mkafanya CHADEMA ionekane haina Demokrasia.

Ulianza vizuri kumbe una upuuzi wa udini, ukabila na ukanda. huko ni kufilisika kimawazo kama alivyotuasa Mwalimu Nyerere1
 
Kwa muda mrefu sasa mheshimiwa(asiyekuwa na heshima) amekuwa mzigo katika cdm tangu achaguliwe kuwa mbunge.aananzisha zogo akiona limeisha anaanzisha lingine .hataki kabisa kuona cdm imetulia.Naomba washauri nasaha wamsaidie katika hili.
 
Dawa ya Shibuda siyo kumjibu upumbavu wake! huwezi kukimbizana na kichaa!
 
shibuda ni kansa mbaya sana.........

he deserves kutandikwa fimbo uchi tena hadharani
 
Anajitahidi kutekeleza kazi aliyotumwa lakini mbaya amekuta makamanda wapo macho wanamuangalia anavohangaika kama samaki aliyetupwa jangwani! hakuna anayemsemesha na kwenye vikao nyeti vya chama hashirikishwi! hata Arumeru hakukanyaga! hiyo ndio dawa yake basi!!
 
Jifurahishe kidogo na habari za huyu mwenzetu! John Shibuda

Mo Blog: Shibuda umekuwa mwanasiasa kwa siku nyingi nini rai yako kwa viongozi wenzio wa kiasiasa.?
Shibuda: Napenda kutoa rai kwa vyama na viongozi wa kisiasa ambavyo viko karibu 21 hapa Tanzania, la kwanza kila chama kijifanyie tathmini, kinawajibika vipi kutekeleza mipango ya kuendeleza amani na utulivu katika hii nchi.
Vinatekeleza mipango gani? Na kila chama kifanye tathmini kijiulize mambo gani ambayo ni makosa kwa ustawi na maendeleo ya nchi yetu inaoongozwa na kulindwa na tabia, mila na desturi za Mtanzania.
Vyama vya siasa viwe na wito unaoitwa ‘kwa maslahi ya umma' na viongozi pia watekeleze wito unaoitwa kwa maslahi ya umma.

Mo Blog: Kwani una shaka na baadhi ya vyama?
Shibuda: Vyama ambavyo vina mdudu shetani anayeitwa ibilisi wa kujenga tafrani, migongano, misuguano au vyama vinavyoitwa ‘chama kampuni' kwa maslahi binafsi, havistahiki kuwa sehemu moja wapo ya mbegu ya kuzalisha amani.
Hivyo watanzania tutafakari, tusemezane, tutazame viwango vya kila chama, katika vyama 21 kwamba je? Tija ya kila chama ni kwa kujenga ustawi na maendeleokwa jamii? Ili mwaka kesho tusherehekee tena siku ya amani duniani. Kusoma zaidi mahojiano yote ingia

Source: Mo Blog

 
Shibuda ni Ndumilakuwili hata hayo ya moyoni yamekaa kindumilakuwili ndumilakuwili
 
Wangemuuliza ni sababu zipi zilifanya akatemwa CCM?
 
director1 Ameshindwa tu kutamka analenga watu gani, jamaa ana hatari huyu haogopi kumwagwa!
 
Last edited by a moderator:
Naona kama shibuda ameongea mambo mazuri tupu hapo. Vyama vingi vya siasa vina matatizo makubwa vikiwemo ccm na cdm. Ninapendekeza tumuelewe hata kama hatumpendi yeye binafsi kwani katika maisha, hakuna jambo la kijinga kwa asilimia 100.
 
Back
Top Bottom