Shibuda aishangaa demokrasia ya CHADEMA

Shibuda aishangaa demokrasia ya CHADEMA

Amakwelo Shibuda jembe, kila mtu ndani ya CDM anamgwaya. Mbona Slaa hamfukuzi kama anavyowafukuzaga viongozi wa kada nyingine?

Unafukuza insignificant figure? ni kama kuuza ng'ombe kwa kesi ya bata
 
Ikiwezekana wampime akili kwanza ili kumtendea haki! Wakigundua ni tatizo la akili, wamwache na kujifunza kumpuuza tu.

Kwani huyo alivyo unahitaji kupoteza rasilimali muda kumpima wakati tayari ashaonekana kuwa na matatizo kichwani?
 
  • Thanks
Reactions: SMU
Hivi kwa nini cdm mtu akitamka tu atagombea urais anaandamwa?tuliliona hili kwa mmoja wa viongozi pekee wawili tu huko chadema ambao hawakutokea ccm bwana zitto kabwe.Hiyo demokrasia yenu(chama cha demokrasia) mnaifanyia wapi labda ?

Ndani ya chama sio kwenye vyombo vya habari
 
Hivi ni makosa ndani ya Chadema kusema kugombea urais? Shibuda ana haki ya kugombea hakuna wa kumzuia Jembe Shibuda hakuna kulala mpaka kieleweke.

Kileleweke wapi wakati ndio term yake ya mwisho hii?
 
Wala shibuda asiwape presha kabisa mpe muda dawa yake inakuja kwa sasa mwache aendelee kuwa mchangamshaji,TIME WILL TELL.
 
Na bado, huo ni mwanzo wa kusambaratika kwa Chadema . Alianza Zitto na sasa Shibuda. Kila wanapotangaza wanakanuswa na wenye Chama . Kwa vile wenye Chama wanajua wanaemtaka .. Hawa ni wa kuja hawatakiwi.
 
Shibuda ni shushushu toka ccm!
Kazi aliyokuja kuifanya chadema ameshindwa, kwani chadema ni chama makini na walimwangalia tu kwa macho manne nini anachofanya kwa tahadhari kubwa sana, tofauti na wengi walivyotarajia achukuliwe hatua kwa mambo mbalimbali anavyokuwa kinyume na taratibu za chama. Alitegemea aleta mtafaruku na mgawanyiko ndani ya chama pindi atakapochukuliwa hatua yoyote ndani ya chama.
Sasa amerudisha majibu ya project yake ccm kwamba huko walikomtuma si kwa upinzani waliouzoea, ni zaidi ya upinzani na hasa ni kwenye harakati za ukombozi wa kweli, ndio maana ccm sasa hivi wana haha na kubuni na kubadilisha mifumo mbalimbali ya utendaji ndani ya ccm wakifikiri itasaidia kwani mbinu chafu nyingi walizokuwa wanazitumia dhidi ya upinzani zimegonga mwamba, hasa kwa CDM.
Haya yote anayofanya shibuda kwa hivi sasa ni kujijengea mazingira ya kurudi ccm kiulaini bila kuonekana ni issue.
 
Mwehu wa kijijini kwenu ni lazima umuzoee na siku ukitoka mjini kwenda kijijini lazima umuulizie jamani hivi furani yupo? Shibuda ni mwehu wa kuzaliwa kabisaaa na sisi tumeshamupuuza kwa sasa kauli zake hazitusumbui na hazina mashiko wala athari kwa M4C.
 
Sijaona mantiki ya huyu mpuuzi kumfukuza.Huyu ni wa kumwacha aendeleee kuropoka ila chama lazima kimwangalie kwa macho manne.Na wala hasishirikishwe kwa mambo muhimu ya kichama

Wana JF na wapenzi wa CDM,

Mimi naomba kutofautiana na wale wanaosema Shibuda aachwe ndani ya CDM kwani walishamzoea na uropokaji wake.Mimi nasema NO! Huyu Mhe.Shibuda inabidi atimuliwe kwa kuvuliwa Unachama na Ubunge! Huyu jamaa ni mpuuzi na
amethibitisha kabisa kuwa YEYE NI KIBARAKA WA CCM ambaye ameingia ndani ya CDM kuivuruga,kuichafua na hatimaye kuisambaratisha kwa kutumia mbinu zake chafu!

Hivi ni nani ambaye anaweza kukubali kukaa na nyoka ndani ya nyumba yake???Wewe umuone nyoka anaingia chumbani mwako halafu unasema hana neno ngoja tumwache tu maana sumu yake haina madhara hata akikuuma hutakufa na baadaye atatoka mwenyewe aende zake!!!Never!

Mimi napenda kuchukua nafasi hii kwa heshima na taadhima niwaombe viongozi waandamizi wa CDM akiwemo M/kiti Freeman Mbowe,Katibu Mkuu Dr.Slaa na uongozi wote kwa ujumla wachukue hatua za makusudi za kumwadibisha huyu mhe. Shibuda haraka iwezekanavyo na ikibidi AVULIWE UANACHAMA NA APOTEZE UBUNGE. Tunajua atakimbilia Mahakamani hiyo ni kawaida. Najua tuna Wanasheria mahiri sana kama Mhe.Tundu Lissu ambao wanaweza kusimama Mahakamani na kupinga huu ujinga wa MWANASIASA KUKIMBILIA MAHAKAMANI ILHALI ANAJUA KABISA KATIBA INASEMA HUWEZI KUWA MGOMBEA UBUNGE AU KUTEULIWA UBUNGE KAMA SI MWANACHAMA WA CHAMA CHOCHOTE! Sasa kama umevuliwa uanachama na uliingia Bungeni kwa ridhaa ya Chama na Wananchi unapokimbilia Mahakamani unataka UMWAKILISHE NANI KWA TIKETI YA MAHAKAMA????This is absolutely nonsense!

Shibuda lazima atimuliwe. Haiwezekani Mbunge wa CHADEMA akakae kwenye NEC ya CCM halafu aombe kugombea Urais wa Tanzania kupitia CHADEMA lakini kwa KUFANYIWA KAMPENI NA CCM. It sounds very crazy to be honest! Kwanini tubembeleze KIBARAKA WA CCM ndani ya chama???Yeye ni nani hasa na ana ubavu gani???Kama wao wenyewe CCM walimkataa kwenye kura za maoni za Ubunge CDM inamkumbatia wa kazi gani???

Nasema tena lazima Shibuda atimuliwe ili chama kiendelee na majukumu mengine muhimu ya kuwaandaa Watanzania kuwa chini ya uongozi wa CDM ifikapo 2015!

Nawasilisha.
 
Huko NEC ya CCM alienda kama mwalikwa kuiwakilisha CDM au alienda kama mjumbe halali toka Shinyanga au alienda kama mwezeshaji kutoa mada?


wana JF tunatumia muda mwingi sana kwa mambo yasiyo na tiba kwa jamii yetu; kwa nini tusitumie fursa tuliyonayo wana JF kujadili nini tunataka viwe vipaumbe kwenye bajeti ijayo ya serikali?
 
Jamaa huyu hafai kabisa,bora CHADEMA wakose jimbo

nikweli tuanzie kwa ZITTO maana yy ndo alikuwa wa kwanza kutangaza nia ya kuwania urais.Ila Shibuda anafaa tumuunge mkono wanajamvi,maana anakiokoa chama chetu CDM dhidi ya ukanda.
 
Shibuda yupo Chadema sio kwa mapenzi yake kwani mwajiri wake CCM amemtuma huko.Atakapomaliza kazi yake mtaona anarudi nyumbani kwao CCM.Yeye yupo pale kujifunza mbinu za wapinzani na jinsi gani yakuzitumia katika chama chake.Tatizo yeye hajifichi kuwaonyesha kuwa bado anataka kurudi nyumbani mapema iwezekanavyo.
 
" Habari zilizolifikia gazeti hili
kutoka ndani ya kikao cha CCM
tangu juzi zinasema Shibuda,
ambaye alihama CCM na
kujiunga CHADEMA mwaka
2010, alivishambulia vyama vya upinzani, kiasi cha
kuwaacha midomo wazi
Wana CCM wenyewe.

Mmoja wa vigogo wa CCM
waliozungumza na gazeti hili
juzi usiku alisema kwamba
baadhi ya maneno aliyotumia
Shibuda dhidi ya CHADEMA
yalikuwa makali kiasi kwamba hata katika mikanda
yao ya video wanazotumia
kwa matangazo ya vyombo
vyao vya habari, ilibidi
wayahariri au kuyakata."~chanzo:Tanzania daima

Hayo ndo yaliyojiri dodoma


Teh teh teh , Shibuda ni zaidi ya jembe ndani ya chadema sasa mbona mnakuwa na wasiwasi jamani? mwacheni agombee urais maana amesema yeye ndio anaefaa sasa sijui 2015 itakuwaje?
 
Ndugu zangu wanachadema huyu Mh,Shibuda ni kiongozi mwenye upeo mdogo sana kutambua kwa muda huu Wtz wanahitaji nini yeye nia yake ni kuwavuruga watu ambao tayari wameishaianza Safari kwenda kwenye ukombozi wa Tanzania yeye anahangaika kubomoa nguvu hiyo. Ushauri wa bure kwa Shibuda endapo CCM bado anaiiona ni nzuri basi tumuombe arudi huko huko kuliko wenzake kila siku wapo majimboni kuitangaza Chadema na kukijenga chama kiwe imara yeye mwenzetu bado anahangaika utafikiri kuna kitu kasahau alikotoka gari yetu bado inasubiri abiria wenye nia njema ya kulikomboa taifa hili endapo yeye anajiona amefika nyumbani tunamuomba ateremke kuelekea nyumbani kwao kwenye maisha bora awaache Wasukuma wenzake na Wtz wengine ambao tumebanwa na maisha kutokana na wale anao wasifia mwenzetu ana agenda ya Siri moyoni mwake na Magamba ccm..........tuendelee kumpuuza bila kumpa nafasi ya kushirikiana na Makamanda wetu wazuri ambao kila siku anaona wanapata taabu wengine wanatishiwa Uhai wao mwenzetu hilo halioni. Mujwahuzi.
 
CHADEMA lazima muwe makini na uwezo wa kujuwa kwamba hii stori imetengenezwa na magazeti kutimiza matakwa ya ccm. Kwanza angalia magazeti (Jambo Leo, Uhuru) yenyewe yaliyoandika yanamilikiwa na nani. Je ni kweli kasema wapinzani hawawezi kuchukuwa nchi au kura za wanachama wa CHADEMA hazitoshi? BAVICHA wanapiga kelele kutokana na walichosoma katika magazeti na sio alichosema Shibuda. Kilichotekea ni taasisi ya utawala bora “Good Governance …” ilialikwa kwenda kutoa ripoti ya tathmini yake kwenye hicho kikao na hii taasisi inaalikwa sehemu nyingi, shibuda ni mmoja ya watu waliopo ndani ya hiyo taasisi. Baada ya maongezi rasmi kulikuwa na utani kati ya kikwete na shibuda. Katika huo utani shibuda alisema atagombea urais kwa tiketi ya mgombea binafsi na sio kwa tiketi ya CHADEMA na akamuomba kikwete amuunge mkono. Lakini magazeti kwasababu ya malengo yao binafsi au ya CCM yaliamua kupindisha kauli hii na kusema Shibuda kaamua kugombea kupitia CHADEMA, na watu hao hao ndio walioleta stori hiyo jamii forum. Baada ya Zito kutangaza kugombea uraisi na kupingwa na Mtei inaonekana CCM wameshagundua udhaifu wa CHADEMA; hawataki mgombea atoke sehemu nyingine isipokuwa kaskazini, kwahiyo kutakuwa na juhudi za kulipigia mstari swala hili mpaka nchi yote ielewe kwamba kama wewe sio mchaga au hutoki kaskazini basi uraisi huruhusiwi kugombea kupitia CHADEMA. Kwahiyo kabla haujaanza ushabiki usiokuwa na umakini kwa kupinga mtu tu kwasababu kasema atagombea uraisi, lazima uwe makini kujuwa labda unawafaidisha CCM. Huyo Shibuda anaelewa CHADEMA hawawezi kupitisha jina lake kugombea uraisi labda awe mgombea binafsi kama alivyomwambia kikwete. Kwahiyo hiyo kauli yakusema atagombea kupitia CHADEMA imetengenezwa KUGOMBANISHA WACHAGA NA WASUKUMA KAMA SIO WATANZANIA WOTE. Kwahiyo kuweni makini, wanaosoma hapa sio tu wachaga bali na kabila nyingine. Hata ukitoa comment unajiita WAMBURA au MASANJA bado tu watu watajuwa ni mchaga kwasababu ya unavyokuwa MWEPESI NA HARAKA ya kupinga watu wa kabila nyingine. Msije mkafanya CHADEMA ionekane haina Demokrasia.
 
nimekusoma

CHADEMA lazima muwe
makini na uwezo wa kujuwa kwamba hii stori imetengenezwa na magazeti
kutimiza matakwa ya ccm. Kwanza angalia magazeti (Jambo Leo, Uhuru)
yenyewe yaliyoandika yanamilikiwa na nani. Je ni kweli kasema wapinzani
hawawezi kuchukuwa nchi au kura za wanachama wa CHADEMA hazitoshi?
BAVICHA wanapiga kelele kutokana na walichosoma katika magazeti na sio
alichosema Shibuda. Kilichotekea ni taasisi ya utawala bora “Good
Governance …” ilialikwa kwenda kutoa ripoti ya tathmini yake kwenye
hicho kikao na hii taasisi inaalikwa sehemu nyingi, shibuda ni mmoja ya
watu waliopo ndani ya hiyo taasisi. Baada ya maongezi rasmi kulikuwa na
utani kati ya kikwete na shibuda. Katika huo utani shibuda alisema
atagombea urais kwa tiketi ya mgombea binafsi na sio kwa tiketi ya
CHADEMA na akamuomba kikwete amuunge mkono. Lakini magazeti kwasababu ya
malengo yao binafsi au ya CCM yaliamua kupindisha kauli hii na kusema
Shibuda kaamua kugombea kupitia CHADEMA, na watu hao hao ndio walioleta
stori hiyo jamii forum. Baada ya Zito kutangaza kugombea uraisi na
kupingwa na Mtei inaonekana CCM wameshagundua udhaifu wa CHADEMA;
hawataki mgombea atoke sehemu nyingine isipokuwa kaskazini, kwahiyo
kutakuwa na juhudi za kulipigia mstari swala hili mpaka nchi yote ielewe
kwamba kama wewe sio mchaga au hutoki kaskazini basi uraisi huruhusiwi
kugombea kupitia CHADEMA. Kwahiyo kabla haujaanza ushabiki usiokuwa na
umakini kwa kupinga mtu tu kwasababu kasema atagombea uraisi, lazima uwe
makini kujuwa labda unawafaidisha CCM. Huyo Shibuda anaelewa CHADEMA
hawawezi kupitisha jina lake kugombea uraisi labda awe mgombea binafsi
kama alivyomwambia kikwete. Kwahiyo hiyo kauli yakusema atagombea
kupitia CHADEMA imetengenezwa KUGOMBANISHA WACHAGA NA WASUKUMA KAMA SIO
WATANZANIA WOTE. Kwahiyo kuweni makini, wanaosoma hapa sio tu wachaga
bali na kabila nyingine. Hata ukitoa comment unajiita WAMBURA au MASANJA
bado tu watu watajuwa ni mchaga kwasababu ya unavyokuwa MWEPESI NA
HARAKA ya kupinga watu wa kabila nyingine. Msije mkafanya CHADEMA
ionekane haina Demokrasia.
 
Back
Top Bottom