Sheria ya kumhudumia Mwanamke ifutwe, kwa sasa Ajira zinatolewa kwa Wote bila upendeleo

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Mar 24, 2018
21,340
51,895
SHERIA YA KUMHUDUMIA MWANAMKE IFUTWE, KWA SASA AJIRA ZINATOLEWA KWA WOTE BILA UPENDELEO.

Anàandika, Robert Heriel
Mtibeli.

Sheria ya Mwanaume kumhudumia Mwanamke ifutwe. Sheria ya mke kuchukua mkopo kwa Jina la mumewe nayo ifutwe. Ni sheria zilizopitwa na wakati na zisizoendana na ulimwengu wa sasa.

Ni sheria kandamizi, zinazomkandamiza Mwanaume.
Kwa zamani zilikuwa sheria nzuri lakini sio sasa. Zilikuwa nzuri kwa sababu Wanaume walipewa fursa zaidi kuliko wanawake.
Wanaume walipewa fursa ya kumiliki Mali huku wanawake walikatazwa.

Wanaume walipewa fursa ya kusoma na kutafuta elimu huku wanawake wakiachwa nyuma.
Wanaume walipewa fursa ya kutafuta kazi na kufanya shughuli za uzalishaji huku wanawake wakibaguliwa.

Ndio maana sheria ya kumhudumia Mwanamke ilikuwa ya maana na tunaweza kuiita sheria ya haki kama Watibeli tupendavyo Haki

Lakini siku hizi Kila mtu anahaki. Haki sawa baina ya jinsia zimeboreshwa na kulinganishwa.
Ikiwa ni hivyo basi na wajibu lazima uboreshwe.

Isiwe wajibu kwa mwanaume kumhudumia Mwanamke katika ulimwengu wa haki Sawa.

Vijana, sio wajibu wako kumhudumia Mwanamke katika ulimwengu huu wa haki sawa. Ndio maana dunia ya sasa imetoa usawa wa kifursa.

Mwanamke afanye kazi na wewe ufanye kazi. Wote mlete mezani. Hiyo ni Haki.

Mwanamke akifanya kazi alafu anataka kuhudumiwa tuu yaani hela yako anaikodolea macho fukuza. Usiwe mjinga. Huo ni ubinafsi.

Mwanamke ambaye atakuambia pesa ya Mwanamke hailiwi wakati unamuita sijui mpenzi, sijui mkeo, huyo ni tapeli, nyonyaji. Huyo hakufai. Piga chini wala usisite mara mbili mbili.

Ndoa za kitapeli, mahusiano ya kibeberu na kikoloni. Unakuta mwanaume mzima kumbe ni koloni la mtu. Unanyonywa kama mwendawazimu. Alafu miaka 45 hii hapa kisukari, presha, mara Stroke unaacha mke Watu tunapiga. Shauri yako. Usijesema sijakuambia.

Alafu kwa ujinga wenu mnauliza maswali ya kijinga, ooh! Mbona wanaume wanawajibika kufa mapema kabla ya Wake zao. Hivi utaachaje kufa mapema ikiwa wewe umegeuzwa kisukule, kuzuka. Mbona kwetu Babu zetu wamepiga age ya kutosha. Tumieni akili. Jinga kabisa.

Usiendekeza ujinga. Mimi nimemaliza. Mwenye hasira za karibu aje tupigane.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
 
Mkuu Kuna dini pia, sheria ya dini moja inataka mwanaume ndio amuhudumie mwanamke hata Kama mwanamke huyo ni billionaire na mwanaume ni kapuku!!

Na Kama wote mnafanyakazi na mshahara ni sawa, Basi mshahara wa mwanaume pekee ndio utakao tumika nyumbani na kumtunza mwanamke pia. Na Kama mwanamke akitoa hela yake hata kununua chumvi Basi lazima arejeshewe fedha zake, labda mwanamke huyo atoe mwenyewe tu kwakupenda kutokurudishiwa!

Sasa hapo huo usawa sijui utakuwaje?! Kufanyakazi wanataka which is good thing but kuwajibika kutunza familia ni Big No!
Wajibu wa mwanaume sio mwanamke!!

Haki bila wajibu ni tamu Sana!
 
Mkuu Kuna dini pia, sheria ya dini moja inataka mwanaume ndio amuhudimie mwanamke hata Kama mwanamke huyo ni billionaire na mwanaume ni kapuku!!

Na Kama wote mnafanyakazi sawa, Basi mshahara wa mwanaume pekee ndio utakao tumika nyumbani. Na Kama mwanamke akitoa Basi lazima arejeshewe fedha zame, labda mwanamke atoe mwenyewe tu kwakupenda kutokurudishiwa!

Sasa hapo huo usawa sijui utakuwaje?! Kufanyakazi wanataka which is good thing but kuwajibika kutunza familia ni Big No!
Wajibu wa mwanaume sio mwanamke!!

Haki bila wajibu ni tamu Sana!
Sheria za dini na dunia zinakinzana, dunia imempa mwanamke fursa na haki sawa, dini bado inamkandamiza mwanamke na kumuona second class.
 
Tumefikia huku , ni rahisi tu unataka mtoto basi uwe tayari kuhudumia huwezi acha kuongeza street children na waliokosa malezi ya baba, wanaume tusifike huku mambo ya kutafuta usawa, hizi zilikua ni ishu za wakinamama zamani
 
SHERIA YA KUMHUDUMIA MWANAMKE IFUTWE, KWA SASA AJIRA ZINATOLEWA KWA WOTE BILA UPENDELEO.

Anàandika, Robert Heriel
Mtibeli.

Sheria ya Mwanaume kumhudumia Mwanamke ifutwe. Sheria ya mke kuchukua mkopo kwa Jina la mumewe nayo ifutwe. Ni sheria zilizopitwa na wakati na zisizoendana na ulimwengu wa sasa.

Ni sheria kandamizi, zinazomkandamiza Mwanaume.
Kwa zamani zilikuwa sheria nzuri lakini sio sasa. Zilikuwa nzuri kwa sababu Wanaume walipewa fursa zaidi kuliko wanawake.
Wanaume walipewa fursa ya kumiliki Mali huku wanawake walikatazwa.

Wanaume walipewa fursa ya kusoma na kutafuta elimu huku wanawake wakiachwa nyuma.
Wanaume walipewa fursa ya kutafuta kazi na kufanya shughuli za uzalishaji huku wanawake wakibaguliwa.

Ndio maana sheria ya kumhudumia Mwanamke ilikuwa ya maana na tunaweza kuiita sheria ya haki kama Watibeli tupendavyo Haki

Lakini siku hizi Kila mtu anahaki. Haki sawa baina ya jinsia zimeboreshwa na kulinganishwa.
Ikiwa ni hivyo basi na wajibu lazima uboreshwe.

Isiwe wajibu kwa mwanaume kumhudumia Mwanamke katika ulimwengu wa haki Sawa.

Vijana, sio wajibu wako kumhudumia Mwanamke katika ulimwengu huu wa haki sawa. Ndio maana dunia ya sasa imetoa usawa wa kifursa.

Mwanamke afanye kazi na wewe ufanye kazi. Wote mlete mezani. Hiyo ni Haki.

Mwanamke akifanya kazi alafu anataka kuhudumiwa tuu yaani hela yako anaikodolea macho fukuza. Usiwe mjinga. Huo ni ubinafsi.

Mwanamke ambaye atakuambia pesa ya Mwanamke hailiwi wakati unamuita sijui mpenzi, sijui mkeo, huyo ni tapeli, nyonyaji. Huyo hakufai. Piga chini wala usisite mara mbili mbili.

Ndoa za kitapeli, mahusiano ya kibeberu na kikoloni. Unakuta mwanaume mzima kumbe ni koloni la mtu. Unanyonywa kama mwendawazimu. Alafu miaka 45 hii hapa kisukari, presha, mara Stroke unaacha mke Watu tunapiga. Shauri yako. Usijesema sijakuambia.

Alafu kwa ujinga wenu mnauliza maswali ya kijinga, ooh! Mbona wanaume wanawajibika kufa mapema kabla ya Wake zao. Hivi utaachaje kufa mapema ikiwa wewe umegeuzwa kisukule, kuzuka. Mbona kwetu Babu zetu wamepiga age ya kutosha. Tumieni akili. Jinga kabisa.

Usiendekeza ujinga. Mimi nimemaliza. Mwenye hasira za karibu aje tupigane.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Upo sahihi mkuu ila kuna wadangaji na wajinga waliolishwa limbwata watakuja hapa kukuponda
 
Back
Top Bottom