Sheria na taratibu za kuasili (Adopt) mtoto Tanzania

Helooo wapendwa.....
Mimi ni mzima wa afya, hofu na mashaka ni juu yenu nyie mlio mbali na upeo wa macho yangu....lakini natumai salam zangu zimewafikia popote pale mlipo....na poleni na harakati za kutafuta grisi....
Moja kati ya malengo niliyojiwekea mwaka huu ni kuweza kuwa na mtoto wangu....sio wa kuzaa.....ila nataka nipate mtoto kwa njia ya kuasili (adoption)....japo ni njia ambayo kwa hapa kwetu sijaiona sana watu wakiitumia ila mie nina sababu zangu za msingi.....hivyo ningependa kujuzwa sheria...taratibu.....na taasisi zinazohusika na hili swala.....asanteni
 
Tafuta ofisi za ustawi wa jamii popote ulipo au wakili anayejuwa sheria ya kifamilia. Vile vile unaweza kwenda wilayani watakusaidia.
 
nenda kwenye kituo cha kulelea watoto yatima ama kama tayari umempata sehemu .nenda ofisi za kata ambazo siku hizi kuna ustawi wa jamii. hawa watakuhoji maswali kadha na watakupa form maalum baada ya kujaza na kurudisha wao watafanya uchunguzi wao.then ukikizi vigezo na masharti utapewa mtoto. wataangalia uwezo wa kumlea,mazingira ya kumlelea,capital nk nk
 
nenda kwenye kituo cha kulelea watoto yatima ama kama tayari umempata sehemu .nenda ofisi za kata ambazo siku hizi kuna ustawi wa jamii. hawa watakuhoji maswali kadha na watakupa form maalum baada ya kujaza na kurudisha wao watafanya uchunguzi wao.then ukikizi vigezo na masharti utapewa mtoto. wataangalia uwezo wa kumlea,mazingira ya kumlelea,capital nk nk
Asante mkuu....
Naomba nikuulize japo kidogo tu japo hili swali naweza kuuliza huko uliponielekeza.....ni lazima niwe nimeoa?
 
Asante mkuu....
Naomba nikuulize japo kidogo tu japo hili swali naweza kuuliza huko uliponielekeza.....ni lazima niwe nimeoa?
ni rahisi zaidi ukiwa umeoa lkn hata kama hujao bado una nafasi ya kupata kuna vitu vingi wanaangalia back ground history,criminal history ,nk nk
 
Helooo wapendwa.....
Mimi ni mzima wa afya, hofu na mashaka ni juu yenu nyie mlio mbali na upeo wa macho yangu....lakini natumai salam zangu zimewafikia popote pale mlipo....na poleni na harakati za kutafuta grisi....
Moja kati ya malengo niliyojiwekea mwaka huu ni kuweza kuwa na mtoto wangu....sio wa kuzaa.....ila nataka nipate mtoto kwa njia ya kuasili (adoption)....japo ni njia ambayo kwa hapa kwetu sijaiona sana watu wakiitumia ila mie nina sababu zangu za msingi.....hivyo ningependa kujuzwa sheria...taratibu.....na taasisi zinazohusika na hili swala.....asanteni
EM hawezi kuzaa na wewe?
 
Taratibu za ku asili mtoto Tanzania zikoje?Hakuna kiasi cha pesa unatakiwa kulipa? Kama ukiasili mtoto kutoka kituo cha yatima baadae wakajitokeza ndugu (kama hana wazazi) wakadai wanaweza kumtumia sheria inasemaje?

Mwanamke aki asili mtoto mchango chini ya mwaka je anaruhusiwa kuchukua likizo ya maternity?
Kama kuna taarifa zaidi juu ya kuasili mtoto naomba kujulishwa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wakuu habari za asubuhi, naomba kwa wanaojua mnisaidie.

Je, ni taratibu gani zinapaswa kufuatwa ili mtu aweze kuasili(adopt) mtoto?

Ni umri gani unaruhusiwa na kwa mazingira gani?

Na ni Nani amayeruhusiwa kuasili?

Karibuni wadau, shukrani sana.

Nani anaweza kuasili mtoto

Ndugu au mtu yeyote anayeishi Tanzania mwenye umri wa miaka 25 na angalau mwenye miaka 21 zaidi ya mtoto anayeasiliwa; mwanamke asiyeolewa aliye raia wa Tanzania au wenza –mke na mume– waliokubaliana kumwasili mtoto kwa maslahi ya mtoto. Mahakama itabidi ijiridhishe kwamba wenzi hao wamekubaliana kumuasili mtoto.

Sheria hii inamruhusu mwanamume kutuma maombi ya kumwasili mtoto ikiwa mahakama itajiridhisha kwamba yapo mazingira maalumu yanayohalalisha utaratibu huo. Wenzi wanaoishi bila kuwa na ndoa inayotambulika kisheria hawawezi kukubaliwa kuendelea na utaratibu wa kumuasili mtoto. Ndio kusema watu wanaoishi kinyumba bila kuwa na ndoa hawawezi kuasili mtoto.

Hata hivyo, ili maombi yoyote ya kumuasili mtoto yakubalike, lazime mwombaji awe ameishi na mtoto husika kwa angalau miezi sita mfululizo kabla ya tarehe ya maombi husika.

Mwombaji asiye raia wa Tanzania anaweza kuasili mtoto ikiwa ameishi Tanzania kwa angalau miaka mitatu mfululizo; amemlea mtoto kwa angalau miezi mitatu chini ya uangalizi wa afisa ustawi wa jamii; hajawahi kutiwa hatiani kwa kosa la jinai na mahakama ya nchini kwake inaheshimu na kutambua maombi yake.

Utaratibu wa kufuata

Sheria ya Mtoto inaelekeza kwamba maombi ya kuasili mtoto yatatumwa Mahakama Kuu baada ya kupata ridhaa ya mlezi au mzazi wa kumzaa mtoto. Mahakama itajiridhisha ikiwa mlezi au mzazi wa mtoto husika anaelewa matokeo ya mwanawe kuasiliwa na ikiwa kweli ameshindwa kumtunza mtoto au amekuwa na tabia ya kumnyanyasa mtoto.

Katika mazingira ambayo mzazi au mlezi hana uwezo wa kutoa ridhaa mahakama lazima ijiridhirishe kuwa utaratibu wa kumuasili mtoto unazingatia maslahi ya mtoto na kwamba matakwa ya mtoto yamezingatiwa. Kwa mtoto mwenye umri wa angalau miaka 14 lazima ridhaa yake izingatiwe isipokuwa kama mtoto hana uwezo wa kujieleza.

Katika maombi ya kuasili mtoto, taarifa zifuatazo zitahitajika. Tarehe na mahali alikozaliwa mtoto; jina, jinsia na jina la ukoo la mtoto kabla na baada ya kuasiliwa; jina, jina la ukoo, anuani, mahali pa kuzaliwa, mahali anapoishi, uraia na kazi ya mzazi anayemuasili mtoto.

Wakati utaratibu wa kuasiliwa mtoto ukiendelea kufanyiwa kazi, mtoto atakuwa chini ya uangalizi wa afisa ustawi wa jamii na hatasafirishwa nje ya nchi bila ruhusa ya mahakama.
 
Back
Top Bottom