Sheria inasemaje kuhusu kuzaa na mke wa mtu?

dungune

Member
Nov 10, 2021
70
157
Habari Wakuu,

Ninaomba kufahamishwa sheria ya ndoa Tanzania inasemaje ikiwa umezaa na mke wa mtu? nataka kujua kama unaweza endelea kutoa matunzo ya mtoto akiwa kwenye familia nyingine. Na unatakiwa kufata utaratibu gani kumchukua mtoto anapo fikisha umri wa kulelewa na baba.

Hii imenitokea kwa mwanamke ambae nilizaa nae mwaka 2017 kwa kipindi cha miaka minne nimekuwa nikitoa matunzo yote kama mzazi mpaka mwaka jana nilipo pokea simu kwa mtu ambae alijitambulisha kama mume halali wa mama mtoto.

Nilishangaa sababu mwanamke alinitambulisha kuwa yeye ni single mama nilipo muuliza jamaa alikuwa wapi kwa kipindi chote anasema alikuwa safarini. Na mwanamke anakiri kweli ni mume wake na waliishi pamoja ila mwanaume alimtelekeza akaenda kuishi na mwanamke mwingine.

Sasa baada ya malumbano ya muda mwanaume akachukua simu ya mama huyo akaiharibu ili nipoteze mawasiliano na mimi nikaamua kukaa kimya ili kuona nini huyo dada atafanya nini.

Baada ya miezi miwili nikapokea simu kutoka kwa jirani wa mama wa mtoto huyo akinijulisha hali ya mtoto sio nzuri hakuna uangalizi tena maana nyumba imekuwa uwanja wa vita. Nikajiskia vibaya sana mana kweli ni damu yangu ila watuwazima na makosa yetu ndio tunapelekea watoto kuwa na mazingira magumu.

Lengo la kuja hapa ni kutaka kujua uhalali wangu kwa mtoto huyo na si mwanamke ili tu mtoto apate haki yake ya malezi.
 
Hiyo ni sababu ya kuvunjika kwa ndoa ya mtu endapo mmoja wapo atafanya kitendo cha uzinzi na ikathibitika. Na pia wewe unaweza kulipa fidia endapo mwenye mke ataamua kukushitaki.

Lakini pia kwenye hali ya kawaida ikitokea kwa upande wako mkeo azalishwe na mwanaume mwingine kwako utajiskiaje au kwenye hii dunia unajiona kidume ni wewe tu au unadhani utayemuoa ni mwanamke wa tofauti sana.
 
Daah kweli kila tukio Lina mfano wake.

Wewe kama Mimi tofauti yetu Mimi sijazaa na yule single mother. Mimi kanipotezea Mali zangu nyingi tu kwa uzembe wake na nilimchukulia poa kwa sababu ya mahusiano yetu ya karibu sana kama Mume na mke,na kama si kutumia uzazi wa mpango ningembebesha mimba.

Funzo:-
Wanaume tuacheni ujing haiwezekani demu humlishi,humvishi wala hamlipii pango ata simu humpigii afu useme mkeo kisa umemtolea mahari au mmezaa nae, huu ni ujinga×1000

Mwanamke matunzo, ndio waislamu wanaambiwa kijana mwenye uwezo aoe kama huna kausha,na uwezo unaozungumziwa ni wa kitandani,matunzo na kumjali ata kwa pipi na peremende.
 
Hiyo ni sababu ya kuvunjika kwa ndoa ya mtu endapo mmoja wapo atafanya kitendo cha uzinzi na ikathibitika na pia wewe unaweza kulipa fidia endapo mwenye mke ataamua kukushitaki kakini...
Mkuu tambua ni vigumu kutambua ukweli ikiwa umekutana na mwanamke na akakwambia yeye ni mama tu alisha tengana na mwanaume aliye zaa nae.

Na hata kwa kujiridhisha kweny mawasiliano ya miaka 3 hakukua na madai yoyote ya mtu kunishutumu natembea na mke wake mpaka mtoto anafikisha miaka 4 ndipo mtu anajitokeza.

Mawasiliano ni pamoja na kupiga simu muda wowote uhuru wa mwanamke kuja kwangu kushinda hata kulala..
 
Daah kweli kila tukio Lina mfano wake...

Wewe kama Mimi tofauti ytu Mimi sjazaa na yule single mother....Mimi kanipotezea Mali zangu nyingi tu kwa uzembe wake na nilimchukulia poa kwassbu ya mahusiano ytu ya karbu sana kama Mme na mke,na kama si kutumia uzazi wa mpango ningembebesha mimba...
wazo la kuiba linanijia akilini ila nimekuja hapa ili kujua uhalali wa kisheria mana kweli anasema ni mke wake ila swali alikuwa wapi kwa miaka mnne?

mpaka nimegharamika kwa kiasi hiki tambua nilikuwa natoa pesa zote kwajili ya matunzo.
 
wazo la kuiba linanijia akilini ila nimekuja hapa ili kujua uhalali wa kisheria mana kweli anasema ni mke wake ila swali alikuwa wapi kwa miaka mnne..?
mpaka nimegharamika kwa kiasi hiki tambua nilikuwa natoa pesa zote kwajili ya matunzo.
Sema wanawake huwa hawajitambui... mwanamke ndo angetakiwa kwenda dawati la kijinsia akupatie huyo mtoto mambo yaende na sio wewe...

Au mwanamke ndo amtoroshe huyo mtoto...
 
Daah kweli kila tukio Lina mfano wake...

Wewe kama Mimi tofauti ytu Mimi sjazaa na yule single mother....Mimi kanipotezea Mali zangu nyingi tu kwa uzembe wake na nilimchukulia poa kwassbu ya mahusiano ytu ya karbu sana kama Mme na mke,na kama si kutumia uzazi wa mpango ningembebesha mimba...
Teh teh teh teh teh 😂😂😂😂😂 we jamaa umenivunja mbavu haa haaaa 😂😂 😂
 
Inawezekana mwanaume wenzio alimtelekeza mkewe.

Si mnajua mkishikwa na micheps mkashikika mnavyokuwa?

Sasa ndio kakumbuka ana mke, au kaona mke anaendelea na maisha yake bila yeye karudi kumvurugia.(ni tabia yenu wanaume)

Hebu mtafute mama mtoto kwanza mzungumze ujue situation ya mtoto kabla hujafanya maamuzi mengine.
mkuu tambua ni vigumu kutambua ukweli ikiwa umekutana na mwanamke na akakwambia yeye ni mama tu alisha tengana na mwanaume aliye zaa nae. Na hata kwa kujiridhisha kweny mawasiliano ya miaka 3 hakukua na madai yoyote ya mtu kunishutumu natembea na mke wake mpaka mtoto anafikisha miaka 4 ndipo mtu anajitokeza...
Mawasiliano ni pamoja na kupiga simu muda wowote uhuru wa mwanamke kuja kwangu kushinda hata kulala..
 
Nenda ustawi wa jamii ,maana ukiishi kinyumba na mwanamke kwa miezi mitatu mpaka sita sheria inatambua kuwa huyo ni mkeo,sasa ukiacha mke kwa kumtelekeza kwa muda wote huo naamini pia anakuwa huru kusaidiwa hasa upande wa kushiriki mapenzi.
 
Habari!
Ninaomba kufahamisha sheria ya ndoa Tanzania inasemaje ikiwa umezaa na mke wa mtu? nataka kujua kama unaweza endelea kutoa matunzo ya mtoto akiwa kwenye familia nyingine...
Tafuta wazee mkayamalize haya mambo. maadam mama wa mtoto yupo hiyo kesi inaisha asubuhi na mapema. Ukienda ustawi (kiserikali) ni sawa pia ila ndoa ya huyo ex wako ndo itakuwa ndo baibai tena.
 
Back
Top Bottom