Sheikh Yahya Hussein afariki Dunia

Sheikh Yahya Hussein afariki Dunia

Pumzika kwa amani Mnajimu Sheikh Yahya Hussein.
Ni majonzi kuwa hutakuwepo kushuhudia na kuthibitisha utabiri wako kuwa kipindi hiki, wanasiasa wakubwa au watu maarufu watafikwa na masaibu ya watoto wao, jamaa zao wa karibu au wao wenyewe, kutekwa au kuchukuliwa mateka kati ya Aprili na Julai 2011.

Utakumbukwa na wengi kwa mema na mabaya, ila Mwenyezi Mungu ndiye pekee mwenye uamuzi wa mwisho juu ya nafasi yako huko ahera.
 
Salam zangu za rambirambi zimfikie rais Kikwete;

kwa kumpoteza huyu jemadari, muona mbali, mlinzi wa wakubwa wengi nchini, simba wa vita, mfasaha wa kujieleza hata kama wa kumsikiliza hawapo na mtaalam wa kimataifa wa tiba za sili.

Vile vile salam hizi ziendee Mufti wa Tanzazania Sheikh Simba bin Jumaa na baraza zima la ma-Ulama kwa kumpoteza muumini wao na mpigania haki na mali za Waislam nchini.


Mungu aweke roho ya Marehemu Sheikh Yahya Hussein mahala pema peponi.


Huyu hadi azikwe ndio tutaamini habari hii, aliwahi kum-bipu Mungu mwaka jana baadae tukaambiwa yu hai!

R.I.P. Sheikh Yahya.
 
Maskini mkweere wa watu sasa atafanyeje na suala la usalama wake kama mlinzi mkuu amefariki! Kizunguzungu kitazuiliwaje?
 
Kifo chake kimeacha pengo kubwa sana katika medani ya siasa za Tanzania hasa hasa kipindi hiki ambacho Nchi yetu inapita katika mitihani migumu sana kisiasa.

Mungu ailaze mahala pema peponi roho ya marehemu Sheikh yahya Hussein, kazi aliyotumwa imekwisha

Kazi ipi aliyotumwa! Ya kumlinda nanii jukwani!?
 
The Following User Says Thank You to Kinyambiss For This Useful Post:
Shkh Yahya (Today)
 
kweli alikua mtu wa system.. naona polisi wanalinda usalama hapo nyumbani kwake na barabara ya kuingilia hapo mwembechai imefungwa
 
RIP sheikh

Nnakumbuka one day niliona kipindi chake kwenye TV akitaja sababbu ya zilizofanya Senegal kuwafunga France kwenye lile kombe la dunia mwaka gani sijui.............. Then akaendelea kuwa kama Taifa star itataka kushnidha mechi yao dhidi ya senegal ilitakiwa wafanye hivyo hivyo........
siku hiyo alikuwa na mabaki na mifupa ya viumbe fulani vya baharini kama baadhi ya dawa za ushindi michezoni...

Anyway wote ni binadamu hatuna uwezo wa kumuhukumu binadamu mwenzetu mungu ndo anajua

 
Pole sana familia ya Mzee Yahya na CCM wote mtoa taswira wenu kaondoka na nyie hamfanyi hadi kwa njia ya madogoli sasa wakati huu ni mgumu sana kwenu. Mungu msamehe makosa yake mpokee Mzee huyu
 
Kikwete shukuru uchaguzi wa kipindi cha pili umepita kwa kulindwa na huyu mganga wako.

Lakini usijali mtu wangu, pole sana.
 
Watanzania mna roho mbaya sana, mabaya ya wenzenu ndio mnayaona yenu hamyaoni, "wacheni mwenyezi mungu ahukumu kiumbe chake, sisi wote bainadamu hatujui hukumu yetu vipi tuanza kumuhukumu shehe Yahya.?
 
Bwana alitoa na Bwana Ametwaa, Jina lake liimidiwe Amina. RIP Mtabiri.
 
Haya tuanze upya habari zake zimeisha labda atajitokeza mtabiri mwingine wa kumlinda mkulu wa nchi

RIP sheikh Yahya
 
He died this morning at his Magomeni home.
Kwa mujibu wa mwanawe aitwaye Hassan, Sheikh yahya amefariki kutokana na heart failure. Aliamka asubuhi ya leo akiwa buheri wa afya, akaanza kazi yake ya kuona wenye matatizo wanaokuja kwake.

Kama kwenye saa tatu hivi, akaanza kujisikia vibaya, akapewa glasi ya juisi lakini hali haikutulia. wakaamua kumkimbiza katika hospitali moja maeneo ya Morocco na alipofikishwa hapo madaktari wakasema tayari ameshafariki dunia.

Mipango ya mazishi inafanywa nyumbani kwake na atazikwa kesho jijini Dar.

Ameimaliza safari yake. Mungu aiweke roho yake mahali pema peponi, Amina

Alikuwa anachangamsha sana taifa wakati mwingine kwa utabiri wake uliokuwa unaenda kombo kila mara.......
Sasa sijui yale majini yamsindikiza ahrea au??? dah! nimuulize nani swali hili?
Then kuna Mchungaji alikuwa shehe tena alikuwa mwanafunzi wa shehe Yahya anaitwa Mchungaji Rashidi Peter Abubakari alikuwa shehe msikiti ulioko mtaa wa mwanza ilala alimtabiria kuokoka au .......
 
Kwa mujibu wa mwanawe aitwaye Hassan, Sheikh yahya amefariki kutokana na heart failure. Aliamka asubuhi ya leo akiwa buheri wa afya, akaanza kazi yake ya kuona wenye matatizo wanaokuja kwake.

Ameimaliza safari yake. Mungu aiweke roho yake mahali pema peponi, Amina

Kudadadeki!!!! Yale majini aliyomtumia Kikwete yamlinde yataenda wapi sasa!!??? Nakuomba mleta taarifa usimfundishe Mungu kazi ya wapi awahifadhi wafu....
 
Katika utabiri wake wakati wa uchaguzi alisema mgombea mmoja wa urais atakufa na iwapo hatokufa basi atakufa yeye binafsi..kwa hili alipatia kujitabiria kifo. Hoja hapa ni nani atakuwa akiwapa amri walinzi wasioonekana aliompatia mkuu wa nchi ?

Inalillahi Waiyna Illayhi Rajuuna

Hujaongezea kachumvi kweli, alitabiri kwa mmoja wa wagombea wenye mvuto, lkn hili la atakufa yeye!!
Mwanafunzi wake mmoja kawa mchungaji.....
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom