Hili swali ukimwuliza Nape au Chiligati utapata majibu.Mimi natamani kujua
alizaa na wanawake wangapi??????
Hao ni ambao wamejitokeza kwa leo, subir na wale wa Mombasa wafike ndo utajua.hao ni rasmi au wote?
RIP Shekh Yahaya Poleni CCM
Wewe wasema, no comprimise na wachawi na washirikina wanaojaza hofu wananchi. kifo cha huyu pepo mchafu ni GREAT RELIEF kwa Taifa.
Duh! Poleni Watanzania wote Mpendao Amani, Mshikamano na Umoja. Sheikh Yahya atakumbukwa sana kwa kutokuwa muumini wa UDINI.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete ametuma salamu za rambirambi kwa familia ya Sheikh Yahya Hussein kufuatia kifo cha Mnajimu Mkuu huyo kilichotokea asubuhi ya leo tarehe 20 Mei, 2011, katika Hospitali ya Mount Ukombozi iliyoko Morocco Jijini Dar es Salaam.TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
SALAMU ZA RAMBIRAMBI ZA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA MHESHIMIWA DKT. JAKAYA MRISHO KIKWETE KUFUATIA KIFO CHA SHEIKH YAHYA HUSSEIN
Nimepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za kifo cha Sheikh Yahya Hussein ambaye enzi za uhai wake alijipatia umaarufu mkubwa ndani na nje ya nchi kutokana na kipaji chake katika masuala ya unajimu wa nyota ambao ulimpatia sifa kubwa, amesema Rais Kikwete katika rambirambi zake.
Ameongeza: Naomba, kama familia, mpokee salamu zangu za pole kwa kuondokewa na kiongozi muhimu na tegemeo kubwa la familia. Namuomba Mwenyezi Mungu aiweke mahali pema peponi roho ya Marehemu. Amina.
Amesema Rais Kikwete katika salamu zake: Naelewa fika machungu mliyonayo katika kipindi hiki kigumu cha kuondokewa na mpendwa wenu. Najua alikuwa mzazi, alikuwa baba, alikuwa babu, alikuwa mlezi na tegemeo kubwa la familia. Najua ameacha pengo kubwa ambalo litakuwa gumu kuzibika. Najua mko katika kipindi kigumu na cha majaribio. Hivyo nawaombeni muwe na moyo wa uvumilivu na subira. Yote ni mapenzi ya Mola. Napenda kuwahakikishieni kuwa niko nanyi katika kipindi hiki cha maombolezo ya msiba wa mpendwa wenu.
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.
20 Mei, 2011