Mwana Mtoka Pabaya
JF-Expert Member
- Apr 22, 2012
- 15,117
- 16,500
Sheikh Ponda amefanya kosa gani?..tujue kwanza kisha tutajadili kitu kinachoeleweka haya ya kudandia treni tu kusema kweli wengine hatuwezi.. Tuambieni kafanya nini kufikia kukamatwa..
Siku zote nitalaani unafiki.
Mkuu Mkandara, sisi wote ni Watanzania, lkn sasa imefikia sehemu tutambuane kwa hulka zetu. Nyinyi wenzetu mmekuwa MIZIGO. Mmekuwa mizigo kwa namna mnavyojiweka na kwa kudhania mnatetea kile mnachokiamini ilhali hamjui u wapi msingi wa imani yenu.
Hili swali lako kwa kifupi ni la kipumbavu.
Upumbavu wa swali lako unaambatana na unafiki wa wengi wenu. Naomba unisome kwa makini kabla hujakurupuka kusema umetukanwa au umeonewa. Mmekuwa na tabia ya kudumu ya unafiki ambao sielewi mmepofuka kiasi hamuoni au mnafanya makusudi mkidhania watu wengine ni wajinga.
Imekuwa kawaida yenu sasa kutokuwa na msimamo imani yenu inapoingia majaribuni kiasi mnakuwa na matamko mawili yanayopingana. Tukio la Mbagala mmelilaani na wengi wenu mkasema kuwa UISLAMU HAUFUNDISHI VILE. Haikuishia hapo, mkadai vile vile kuwa, tukio lile haliwezi kamwe kufanywa na Muislamu kwa kuwa ni kinyume cha mafundisho ya Marehemu Mohammad. Mkasema kuwa mambo yale machafu yamefanywa na watu wenye nia ya kuuchafua Uislamu. Mimi naamini hayo yote yamesemwa ili tu kutuaminisha kuwa Uislamu hauungi mkono vurugu.
Cha kushangaza (unafiki mbaya), unapofikia wakati wa sheria kuchukua mkondo wake dhidi ya watu ambao mwanzo mmewakana kuwa si Waislamu ila wana nia tu ya kuuchafua Uislamu, basi mnageuka. Hapo kauli yenu ni UISLAMU UNAANDAMWA.
Ina maana wahalifu wana uhusiano na Uislamu kiasi wakikamatwa mseme uislamu unahujumiwa?
Jana Channel Ten imemnukuu Sheikh Ponda akisema amesikitishwa na tukio lile na analilaani. Lakini alichotaka yeye ni kusikia serikali ikilaani kitendo cha mtoto kukojolea quran. Serikali haijalaani, bali imechukua hatua za kisheria kumfikisha mtoto yule mahakamani, vivyo hivyo kwa wezi wale na wavunjifu wa amani. Lakini Ponda anahoji kwa nini wamekamatwa.
Ujinga na unafiki wa Ponda, wewe unaurudia hapa. Hii tabia yenu si nzuri kwa kweli. Ikiwa tunataka tuonekane wengi, JUMA ni MUISLAMU, lakini JUMA akiiba KANISANI, JUMA sio Muislamu.
Kwa kweli mnachosha, tukiacha masihara, mmekuwa mzigo. Ndio hizi tabia zinafanya tunarudi nyuma hata katika mambo ya msingi. Wakati watu wanakazana kuibana serikali kudai mambo ya msingi kwenye katiba mpya, wenzetu mnadai haki ya kufuga ndevu na polisi kuvaa hijabu. Hii maana yake ni kwamba, mambo ya elimu, afya na ulinzi wa nchi yetu nyie kama kundi hamna maoni, mnaji- isolate na kuwa na maoni yenu kwa faida yenu na hayo mengine mnawaachia waliopewa jukumu la kuibeba nchi, au nisemeje?
Laana huonekana kwa matendo ya mwanadamu, na unafiki ni sehemu ya laana hiyo.