Seif al Islam
JF-Expert Member
- Nov 14, 2011
- 2,156
- 640
Tuhuma hizo ziangaliwe maana sheikh amekuja na mahesabu kabisa
we ni miongoni , na nyie ndo mlokuwa mkimlalamikia jk alipokuwa anajitahidi kubalance! hoja ya kuwa waislam hawajasoma ni ya kijinga sana, pita collages na universities uone takwimu!Hiyo si kweli kwamba kuna ubaguzi wa kikanda na kidini. Rais alipotangaza kuwa Mfalme wa Morroco amekubali kuwajengea waislamu Msikiti mkubwa sana Dar. Si waislamu walifurahi sana? Na wakristo walishangazwa sana na wakanyamza?
Na kama ingekuwa ni wakristo wanajengewa Kanisa KUBWA si kelele ingekuwa kibao?
Sasa basi ni lazima tujue TAKWIMU za DINI hizi mbili zilivyo nchini mwetu:
WAKRISTO ni 61.4%
WAISLAMU 35.2%
Kati ya hawa WAISLAMU 35.2% Wengi walienda Madrassa zaidi kuliko masomo ya elimu ya kawaida kabla ya serikali kuhimiza umuhimu wa elimu!
Wazazi wa watoto wa Kiislamu waliojua UMUHIMU wa ELIMU waliwapeleka watoto wao shule za dini ya Kikristo wakasomehuko nao hawakuwa wengi walikuwa ni WACHACHE.
Hivyo basi kati ya WAKRISTO 61.4% wengi waliosoma ni wale waliotoka mahali WAMISIONARY WALIKUBALIKA na kuanza kujenga shule.Hivyo wengi WAKABAHATIKA kusoma zaidi.
Na Sehemu zilizokuwa hazikufikiwa na wamisionari zilibaki nyuma kimasomo bila KUJALI DINI ama UKANDA. Hivyo wengi HAWAKUSOMA!
Hiyo ndio hali halisi iliyoleyeleza UWIANO kuwa hivyo MPAKA LEO!
SIDHANI kama rais Magufuli ANABAGUA.Ila anaangalia Qualifications na si UDINI! ama UKANDA.
Watanzania wote wanapewa haki sawa.
Kusema kanda ya ziwa inapendelewa si kweli Ukanda wa KUSINI una MAWAZIRI wengi zaidi. Hii ikiwa ni pamoja na WAZIRI wetu MKUU Kassimu Majaliwa ambaye ni MWISLAMU na mke wake Mary ambaye ni Mkristo.
Hizi kelele za Sheikh Khalifa HAZINA msingi wowote!
Aliyeuanzisha humuoni na wewe kwa maneno na matendo yake bado unamwamini...?Kila kiongozi amechaguliwa kwa elimu yake na Si dini .
Mnaotaka kuanzisha ugomvi huu wa kidini hauta ka uishe.
Mtu anakaa anaanza kuhesabu watu wa dini yake wapo wangapi serikalini??
Ni mawazo ya kipumbavu..............
mwenzio katoa data .....we unaishia kusema muongo bila ushahidiKwa masiku kadhaa Sheikh Khalifa amekuwa akisikika na kauli yake ya kumtuhumu Rais Magufuli kuwajaza Wakristo wengi kwenye nafasi zake za uteuzi.
Aidha Sheikh huyo aliongezea kwa kusema kuwa licha ya uwepo wa suala hili la udini Rais Magufuli ameweka wazi upendeleo wake wa kikanda ambapo watu wa kanda ya Ziwa wameonekana kung’ara kwa kuteuliwa katika nafasi za uongozi kwa wingi zaidi kuliko watu wa kanda yoyote hapa nchini.
Akizungumzia suala hilo na waandishi wa gazeti la Mizani la November 11, 2016 Sheikh Khalifa Khamis alieleza kuwa katika nafasi 10 walizotumbuliwa Waislam ni nafasi 1 tu ndiyo aliyopewa Muislam.
Sheikh Khalifa alizidi kufafanua kuwa Wenyeviti wa bodi mbalimbali walioteuliwa na Rais Magufuli 18 ni Wakristo na 1 tu ndiyo Muislam.
Makatibu Tawala wa Wilaya Wakristo ni 81% huku Waislam wakiambulia 19% tu. Wakuu wa wilaya Wakristo ni 71% na Waislam ni 21%.
Makatibu Tawala wa mikoa 137 ni Wakristo na 16 tu ndiyo Waislam. Wakurugenzi wa Halmashauri za wilaya na majiji Wakristo ni 185 na Waislam ni 36 tu.
Kitu pekee anachopaswa kutambua Sheikh Khalifa Khamis ni kwamba Rais Magufuli hateui mtu kwa kuangalia dini bali anaangalia taaluma na uwezo wa kuongoza.
Kukiwa na kitengo kinachohitaji uwakilishi wa dini hapo ndo tunapaswa kuangalia usawa wa uwakilishi wa kidini. Pia anapaswa kutambua kuwa Tanzania haina Wakristo na Waislam tu, kuna watu wa dini tofauti tofauti na wasio na dini pia, je hao amewaweka kwenye kipengele gani?
Hizi ni njama tu za kutaka kumrudisha nyuma Rais wetu kipenzi cha Watanzania wengi. Watanzania tunahitaji MAENDELEO na AMANI tu, mambo ya dini tunayaacha kwenye nyumba za ibada. Tunapofika kwenye sekta za umma hatusemi tena mambo ya dini zetu, bali kauli yetu huwa ni moja tu nayo ni HAPA KAZI TU.
Ni jambo la kusikitisha sana kuona kiongozi mkubwa wa dini akitoa tuhuma za uongo na uzushi kwa Kiongozi Mkuu wa wa nchi yetu.
Sheikh Khalifa anakiuka misingi ya imara ya taifa letu iliyowekwa na baba wa Taifa Mwl Julius Nyerere ya kupiga vita udini na ukabila.
Udini na ukabila ni mbegu mbaya sana ambayo siyo tu haifai kupandwa kwenye ardhi yetu bali haipaswi hata kutunzwa majumbani mwetu, isije mea hata kwa bahati mbaya.
Mataifa mengi yameshuhudia machafuko na mauaji ya kutisha kwa udini na ukabila. Hakuna hata Mtanzania mmoja anayetamani kuona mfano wa mauaji ya Kimbari ya Rwanda au vita ya Biafra Nigeria ikitokea hapa kwetu.
Mpangawangu,Muhimu ni Rais kufanyia kazi haya malalamiko,taifa hili ni la watu wa dini zote
Hii sensa imefanyika lini?! "Wasomi" nyinyi utawasikia "huwa tunapitisha sensa makanisani!" Kama nawe hili ndo jibu lako; basi naomba unisaidie yafuatayo!ilivyo nchini mwetu:
WAKRISTO ni 61.4%
WAISLAMU 35.2%
Kati ya hawa WAISLAMU 35.2% Wengi walienda Madrassa zaidi kuliko masomo ya elimu ya kawaida kabla ya serikali kuhimiza umuhimu wa elimu!
sasa huo msikiti wataingia waislam wotehata mimi sikubaliani na suala kuwa utawala wa JPM unawapendelea wakiristo sababu kuna maswala matatu mazuri rais aliwafanyia waislamu, ambaye wakiristu haja wafanyia:
1) kwanza kashiriki Baraza la IID, na kuwaahidi mali zote za waislam zilizo porwa, watarejeshewa.
2 )waislam waliahidiwa kuwa BAKWATA, wajengewe OFISI mpya.
3) rais aliwaobea kwa Mfalme wa Morocco awajegee MSIKITI MKUUUBWA..
sasa wakiristu hakuna hata jambo moja walio fanyiwa
Toka tupate uhuru haijawahi kutokea waislamu kuwazidi wakristo kwenye teuzi serekalini.Angefanya ulinganisho na Awamu iliyopita ningemuelewa.
Kwamba awamu iliyopita ambayo Rais alikuwa muislam teuzi zilikuwa hivi na hivi sasa ni hivi.
Pamoja na hayo pale hawaendi kuhubiri dini wanaenda kuwatumikia watanzania wote yoyote anafiti kama anakizi vigezo.
Waanze na kukataa kujengewa mjengo na serikali kwanza.
argument kuwa waislam hawajasoma ni argument ya kipumbavu kuwahi kutokea! anyway endeleeni ni dhulma jehanam inawasubiria, thus y kuna siku ya hukumuKuteuliwa kazi serikalini sio bakwata wala tec. Hatuangalii elimu ya madrasa wala teolojia ya dini bali vigezo vingine. Wewe shehe wawapi. i
kwa hiyo ili wawe serikalini waislamuu wamtafute asiyesoma mwenzao ndio wampigie kura?Nilivyokuwa Sekondari shule ya serikali
Waisilamu 150
Wakristo 650
Kwa hiyo wanaofaa ni wakristo tuu?Mtoa mada ukimaliza hili utaanza kuleta hoja zingine za kibaguzi kwa maslahi ya nani. Hii inchi ni yetu wote kwa nini mnaleta hoja za kipuuzi mala udini, mala ukanda, mala mtakuja na mambo mengine. Hivi tutafika kweli kwa ujinga kama huu. Hivi mtu asipewe nafasi kama anafaa kisa dini yake na kabila yake. Acheni hizo ni akili za kipumbavu hizo.
Mngekuwa na elimu hiyo mnayodai tungeona maendeleo kwa jinsi mlivyojazana serekalini.Facts zipi unaongelea? Kwani kigezo cha uteuzi ni dini ya mtu? Tafuteni elimu kabla ya kuanza kupayuka ovyo ovyo.