Huyu shekhe anahitaji kupewa ushauri nasaha kwa upole. Lakini, niseme tu kwamba, manung'uniko yake ni kama ya kina Hellen Kijo Bisimba kuhusu ubaguzi wa kijinsia katika teuzi za JPM. Kina Hellen wanataka nafasi za uteuzi zigawiwe pasu kwa pasu kati ya wanawake na wanaume. Sasa shekhe anataka nafasi zigawiwe kwa kuzingatia uwiano fulani kati ya makundi mbalimbali ya kidini na kikanda. Naona auanongelea Ukristo dhidi ya Uislam, Umashariki dhidi ya Umagharibi. Amesahau kuongelea ujana dhidi ya uzee, Ukulima dhidi ya Ufanyabiashara, Usomi dhidi ya Kutosoma, na migawanyiko kama hiyo.
Yeye pamoja na kina Bisimba ni watu wa kuelimishwa hivi: Vyeo havigawiwi kwa kuangalia vigezo vinavyohusiana na migawanyiko ambayo haina tija katika ofisi. Kwa mfano, mwalimu wa hesanu anaweza kuwa mwanamke au mwanamume, mkristo au muislamu, mmashariki au mmagharibu, kijana au mzee. Lakini hawezi kuwa mkulima wala mfanya biashara kama ambavyo hawezi kuwa asiye na kisomo. Vigezo vya ujuzi, ustadi, uzoefu na utayari vinahusika. Hivi hoja hii ni ngumu?
Kuna performance indicators in good governance wanatuletea hawa development partners kama vile gender equity, denominational equity, geographical equity, inter generational equity, n.k. Haya mambo tuyakatae kwa hoja kwa kuwa hayana tija. Tukikubali kila kitu tutakuwa kama madodoki.