Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,378
- 39,319
Nabisha hodi watani, mjuao Kiswahili,
Nimetingwa mawazoni, sasa nauliza swali,
Jibu niandikieni, moyo wangu ukubali,
Kula tunda kwa kuiba, kwanini huko kutamu?
Ni tunda naulizia, lile lililonawiri,
Si langu nawaambia, la kwake bwana Bushiri,
Miye nimetamania, njama nikatafakuri,
Kula tunda kwa kuiba, kwanini huko kutamu?
Mwenyewe yuko kazini, shamba liliko ni mbali,
Zamu yake ni jioni, asubuhi yangu mali,
Nalila kiulani, pasipo ya mushkeli,
Kula tunda kwa kuiba, kwanini huko kutamu?
Tunda silili kwa pupa, na silili kibahili,
Siling'ati kwa kuepa, kama vile mbilikili,
Mbegu yake sitotupa, namung'unya kimahili,
Kula tunda kwa kuiba, kwanini huko kutamu?
Utamu wake adimu, unaizidi asali
Tunda hili siyo ndimu, na wala siyo figili,
Ninaling'ata kwa zamu, unasisimka mwili,
Kula tunda kwa kuiba, kwanini huko kutamu?
Siogopi kuja bambwa, na yeye bwana Bushiri,
Ni fumbo lilifumbwa, tunda sitalighairi,
Hata akileta Mbwa, nalifunguia safari,
Kula tunda kwa kuiba, kwa nini huko kutamu?
Beti zangu nazifunga, jibu lenu nasubiri,
Mlo mabingwa kutunga, mnijibu kishairi,
Na hata mso malenga, nijibuni bila shari,
Kula tunda kwa kuiba, kwanini huko kutamu?
Na. M.M.Mwanakijiji (Sauti ya Shamba)
Nimetingwa mawazoni, sasa nauliza swali,
Jibu niandikieni, moyo wangu ukubali,
Kula tunda kwa kuiba, kwanini huko kutamu?
Ni tunda naulizia, lile lililonawiri,
Si langu nawaambia, la kwake bwana Bushiri,
Miye nimetamania, njama nikatafakuri,
Kula tunda kwa kuiba, kwanini huko kutamu?
Mwenyewe yuko kazini, shamba liliko ni mbali,
Zamu yake ni jioni, asubuhi yangu mali,
Nalila kiulani, pasipo ya mushkeli,
Kula tunda kwa kuiba, kwanini huko kutamu?
Tunda silili kwa pupa, na silili kibahili,
Siling'ati kwa kuepa, kama vile mbilikili,
Mbegu yake sitotupa, namung'unya kimahili,
Kula tunda kwa kuiba, kwanini huko kutamu?
Utamu wake adimu, unaizidi asali
Tunda hili siyo ndimu, na wala siyo figili,
Ninaling'ata kwa zamu, unasisimka mwili,
Kula tunda kwa kuiba, kwanini huko kutamu?
Siogopi kuja bambwa, na yeye bwana Bushiri,
Ni fumbo lilifumbwa, tunda sitalighairi,
Hata akileta Mbwa, nalifunguia safari,
Kula tunda kwa kuiba, kwa nini huko kutamu?
Beti zangu nazifunga, jibu lenu nasubiri,
Mlo mabingwa kutunga, mnijibu kishairi,
Na hata mso malenga, nijibuni bila shari,
Kula tunda kwa kuiba, kwanini huko kutamu?
Na. M.M.Mwanakijiji (Sauti ya Shamba)