Kama Eva asingekula tunda la mti wa kati

Mshana Jr

Platinum Member
Aug 19, 2012
269,634
697,845
Ijumaa Khareem....!

Naandika haya Leo hii kwakuwa kwakuwa Eva alikula tunda la mti wa kati mti wa UJUZI wa MEMA na MABAYA.

Eva hakujilia tu hilo tunda bali ni kwa ushawishi wa nyoka.... Na kamwe hakuwahi kuhangaika nalo kwa kuwa Mungu mwenyenzi yote alikuwa keshakataza kabisa matumizi ya matunda ya huo mti wa kati mti wa Ujuzi wa mema na mabaya. Haya ndio maelezo ya kidini katika ukristo.

Kuna maswali mubashara ya kujiuliza hapa;

- Kwanini kiumbe nyoka? Na si kingine chochote?
- Kwanini kiumbe nyoka hakumfuata Adam?
- Kwanini Eva baada ya kula na kuliona lile tunda linafaa kwa chakula hakuhisi tofauti yoyote mpaka alipompa Adam akala ndio wakajihisi wako uchi?
- Ni nani aliwafunulia siri ya wao kuwa uchi?

Haya maswali yatachukua Karne nyingi kuja kupata majibu mubashara, lakini dunia ipo hapa ilipo Leo! Ipo hivi ilivyo leo kutokana na kile kilichotokea Eden. Nje ya hapo mambo yangekuwa tofauti kabisa.

Inawezekana kabisa Adam na Eva wangeishi pale milele na pengine RACE ya Africa na waafrika tusingekuwepo? Kutokana na picha za wazungu Adam na Eva hawakuwa weusi... Na dunia isingekuwa hivi ilivyo leo.

Kuna dhana zinazopingwa sana na hii pengine ni kutokana na kukosekana kwa ithibati japo za kimaandishi kwamba nje ya Eden huko mbali duniani kulikuwa na viumbe wengine waliofanana na wale wa Eden. Lakini hili linapingwa kwa nguvu na yale maneno ya kwenye Bible kuwa Mungu ndie aliyeumba dunia hii na vingine vyote vilivyomo.

Tunaitwa kizazi cha nyoka je ni sisi wote ama ni wale tu waliokuwa Eden na vizazi vyake? Lakini Kwanini kizazi cha nyoka?..

Ni mkanganyiko tupu lakini bado nazidi kujiuliza kama Eva kwa ushawishi wa nyoka asingekula lile tunda ingekuwaje! Leo hii??? Ama kama angekula peke yake bila kumgaia Adam ingekuwaje? Je story ya Lilieth ingejirudia?

Kuna mengi bado hatuyajui.

Sent from my INFINIX-X551 using JamiiForums mobile app
 
I think we are living in the new chapter baada ya uasi uliotokea pale eden na ilikupata jibu lazima turudi kuishi kwenye ile chapter means turudishe miaka nyuma halafu tuwe pale eden.Kitu ambacho ni mathematically impossible
 
Tukianza kutafuta hayo majibu tutajaza millions of pages na bado hatuta pata jibu sahihi mana ni vitu vya kufikirika sana.
Cha msingi life goes on
Ni kweli lakini bado yataendelea tu kutafutwa
Kwa mfano dhana ya tunda! Kwanini maranyingi tufaa ndio litumike?
Kitendo cha kula hilo tunda kilijumuisha viungo vitatu macho mdomo na mkono na miguu pia.. Lakini baada tu ya kula wanahisi aibu na kuziziba sehemu zao za siri kwa majani! Kwanini? Kwanini in the first place hawakuziba mdomo uliokula?
7867f28db74476846565fd17120d433b.jpg
 
MUNGU hakuumba Wazungu .
MUNGU aliumba MTU mweusi.
Malaika walipo ona binti black zina shape Kali, sura na rangi wakavutiwa.
Wakaja duniani na kuzaa na binadamu, ndio wakapatikana Wazungu.
Ngorongoro creator ndio ilikuwa Eden.
Habari ndio hiyo mshana jr The king of JF.
 
Ni kweli lakini bado yataendelea tu kutafutwa
Kwa mfano dhana ya tunda! Kwanini maranyingi tufaa ndio litumike?
Kitendo cha kula hilo tunda kilijumuisha viungo vitatu macho mdomo na mkono na miguu pia.. Lakini baada tu ya kula wanahisi aibu na kuziziba sehemu zao za siri kwa majani! Kwanini? Kwanini in the first place hawakuziba mdomo uliokula?
7867f28db74476846565fd17120d433b.jpg
Jr hebu fafanua miguu imetumikaje kula lile tunda especially pale alipokula eva
 
WaAfrica tusingekuwepo vipi wakati ni old vai IPO tens kwetu tena Tanzania mkuu? Rejea notes za darasa la tano mkuu
 
MUNGU hakuumba Wazungu .
MUNGU aliumba MTU mweusi.
Malaika walipo ona binti black zina shape Kali, sura na rangi wakavutiwa.
Wakaja duniani na kuzaa na binadamu, ndio wakapatikana Wazungu.
Ngorongoro creator ndio ilikuwa Eden.
Habari ndio hiyo mshana jr The king of JF.
Aisee
Hapo umeongelea historia ya kawaida,hebu tupeleke kwenye maandiko ya Mungu halafu utwambie huyo mtu mweusi ametokeaje
 
MUNGU hakuumba Wazungu .
MUNGU aliumba MTU mweusi.
Malaika walipo ona binti black zina shape Kali, sura na rangi wakavutiwa.
Wakaja duniani na kuzaa na binadamu, ndio wakapatikana Wazungu.
Ngorongoro creator ndio ilikuwa Eden.
Habari ndio hiyo mshana jr The king of JF.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom