Shabiby line tuoneeni huruma abiria....!!!

Shabiby line tuoneeni huruma abiria....!!!

Mtu unakula 15k ukishuka tu pale kwenye gari.

Hiyo hela si unaweza kununua kuku wako, ndizi mzuzu, chipsi, viazi au hata mihogo. Juice yako ya matunda umeihifadhi kwa chupa itunzayo baridi.
Njiani unakula saaafi kabisa.

Nakumbuka ant yangu alikua anasoma Mwanza, enzi hizo tupo kusini huko. Ilikua kama kesho ana safari basi leo bibi ataanza kumpikia kuku, chipsi, maandazi(vile vidogo vitamu kweli)

Safarini anajinoma tu, sanasana yeye ni kununua juice/soda.
Anasafiri na kiporo?
 
safari ya masaa 8 unataka kula njiani huo ni ulafi, mimi nilikuwa natoka dar to mwanza bila kula njiani na nikirudi mwanza to dar sili
njiani
Tunajuaje wewe una ubahili au hauna pesa pia. Inawezekana msamaria mwema akikunulia chakula kwenye safari hiyo ya masaa 8 au ya Dar to Mwanza utakula vizuri tu.
 
Tunajuaje wewe una ubahili au hauna pesa pia. Inawezekana msamaria mwema akikunulia chakula kwenye safari hiyo ya masaa 8 au ya Dar to Mwanza utakula vizuri tu.
Kwa vile wao vinara wa kushinda njaa basi wanataka kila mtu ashinde na njaa.
Pesa yake mwenyewe,mtu anashindaje njaa?
 
Mnatuleta kwenye migahawa ya ghali sana kwa huduma za chakula, au mnataka turudi kwenye Zama za kusafiri huku tumebeba mikate na soda?

Mnatuleta kwenye migahawa ya ghali sana kwa huduma za chakula, au mnataka turudi kwenye Zama za kusafiri huku tumebeba mikate na soda?
Kwa kweli mimi nikipanda ABC waga naiona thamani ya pesa niliyotoa. Jamaa wana very hygiene toilets na hygiene food pale Cathe hotel japokuwa naishia kula wali maharage wa elfu 3. Ila kwa usafi ABC ni namba moja
 
Siku ukipelekwa Muhimbili hospital, siku bibie amekupa mzigo mashine haifanyi kazi, Kisukari kimepanda unatamani uikamate uingize kwa mkono utam'kumbuka Dokta Janabi.

#Mark my words.
Acha kumuambudu mwanadamu mwenzako
Janabi anaweza zuiai mtu asipate type 1 diabetic?
Kuna vitu ni kuomba mungu tu visikutokee ila hakuna uhodari wa kuvizuia , tembelea muhimbili siku moja uone watoto wadogo wakisubiri dialysis! hadi huruma maana hujui walikosea wapi mpaka figo zinafeli
 
Sawa, nikujuze tu, vyakula vya njiani huwa wengi wanawalisha viporo na ndio maana abiria wengi hukamatwa na matumbo ya kuhara.
Vyakula vinabaki, wanaweka kwenye freezer kesho yake unapashiwa.
vyakula vya njiani vyafaa mtu ambaye hajiwezi kabisa lakini ili kuondoa huo ukiritimba ni kuhama kabisa kwenye hayo mabasi maana hasikilizi kilio chenu.
Tatizo watanzania wewe wanaushamba wa kula hovyo wawapo safarini
 
Back
Top Bottom