Shabiby line tuoneeni huruma abiria....!!!

Shabiby line tuoneeni huruma abiria....!!!

Padle your own canoe, beba donut zako 2 weka kwa mfuko. Nunua soda/juice njiani huko ule inatosha.
Tatizo Watz, mnaendekeza wali, ugali, ndizi nyama........yaani mbongo bila kula ubwabwa hajala bado.
Acha kabisa, ubwabwa kambale?
 
Duuh bora ununue biskuti na soda yako..dar sio mbali mpk ule mi wali au michips mchemsho
Kuna siku niko kwenye dar express tukapelekwa pale mombo. Binafsi safarini nakula vyakula vikavu tu (nyama choma, chips au ndizi za kukaanga) nje ya hapo ni bites tu.

Nikawa na mzungu flani klwa rangi ya ngozi yake ) kwenye seat ya pembeni. Kufika pale jamaa akanunua wali maharage, wakamjazia na kisanvu mchuzi mwingi, akachukua na sharubati ya parachichi (imewekewa kwenye chupa ya maji) Akaja kula ndani ya gari daaah siku ile ndio niligundua kuna watu wana roho ngumu.
 
Wana "succession plans"!!??
Maana biashara nyingi mzee yupo hoi lakini ndiye kashikilia usukani,na ana watoto watu wazima wengi ambao wangeweza kuendeleza biashara kama wangekuwa wameandaliwa vyema.
Nafikir ni wakati muafaka wakae pembeni na kuachia watoto waendeshe biashara kama mabvyo Azim Dewji kamuachia Mohamed Dewji
 
Acha tabia za kula hovyo, Dar Dodoma eti unakula njiani mwanaume mzima! Ubidhoo unakusumbua ndiyo maana mnalishwa vibudu visivyoivishwa vizuri, nunua ndizimbivu mbili au ndizi choma na soda au juisi, usiguse mishikaki hata ukipewa bure.
Eti ubishoo , kweli this is Jf
 
mimi wale huwa nawafananisha na wachinja kuku wa sokoni, anakulipisha 1000 anakuchinjia na kunyonyoa manyoya, ila kichwa na miguu hakupi, ukifanya mchezo hata filigisi anaweza kuchukua, jioni vimejaa vindoo anauza kwa mamantilie kwa pesa ndefu tu, vya kukaangia na pilipili then wanauza kwa wanywa chibuku na mnazi huko uswahilini.
Huu ni ushuzi mzito kabisa. Yani anakuchinjia kuku kwa buku kisha anabaki na mazaga?
 
Hawezi kusimama kwa mshindani wake wa Biashara.
Ila waluguru na Wagogo sasa muiteni Mzee Mremi au Sawaya wa Kilimanjaro truck hiyo barabara atawawekea hoteli na mabasi ya kistaarabu.
Kilimanjaro ana hotel yake mbona haina maaju yoyote zaidi ya bei kubwa na msosi uliolala, pili kuhusu mabasi ya klm itakuwa ulipanda zamani wewe
 
Kilimanjaro ana hotel yake mbona haina maaju yoyote zaidi ya bei kubwa na msosi uliolala, pili kuhusu mabasi ya klm itakuwa ulipanda zamani wewe
Of Course , way back 2009 ndio mara ya mwisho kupanda public transport.
 
Tatizo wabongo pia tunapenda sana kupoteza muda na kulakula hovyo. Safari ya Dodoma ilipaswa iwe kushusha tu abiria na kupakia na sio kusimama kula. Hata safari ya Arusha ilipaswa kuwa hivyo. Angalau Dar - Mwanza, Dar - Sumbawanga, Dar - Kigoma, Dar - Songea, Dar - Bukoba ndo kuna ulazima wa watu kusimama kula.
 
Back
Top Bottom