Ni afadhali wapaki sehemu ya bei ya juu ila huduma ziwe zinaendana na wanachotoa. Utatumia hela nyingi ila utakula vizuri. Ila pia mabarabarani tunaposafiri chakula ni kati ya Sh. 5,000 hadi 10,000 sasa haya ndio mambo ya kulalamika kwamba bei ni juu kweli???
Naona bundles zimekuwa bei rahisi sana hadi vijana wa shule wanatulalamikia kwa mada potoshi. Tulalamikie huduma mbovu ila sio kuogopa kupelekwa sehemu za bei kubwa! Sasa mnataka kutuua kwa kipindupindu kwa mama ntulie kwa ugali na wali wa elfu mbili??? Yaani kabisa magari yakapaki kwa vibanda vya kuuza chakula cha elfu mbili na elfu tatu!!? Tutafuteni hela ndugu zangu.