Shabiby line tuoneeni huruma abiria....!!!

Shabiby line tuoneeni huruma abiria....!!!

Shida yenu mnakula kama wajawazito...huwezi kubeba snacks zako na maji siku ikapita??Mimi nilishaacha kula njiani kitambo sana
 
Kamanda kwa safari za Dom-Dar kama wataka usipate tabu ya chakula panda private tu zimejaa kibao hapo bungeni/CBE.
Unasafiri kwa raha kabisa.
 
Wakuu, narudi Dodoma. Kama kawaida wametushusha hapa, Leo nimechukua machungwa na maji
PXL_20240225_123641705.jpg
PXL_20240225_123645229.jpg
PXL_20240225_123555612.jpg
 
Kila mwenye hela na mamlaka ni kambale, na akiwa kada ndio anakuwa nyangumi kabisa. No one cares!
 
kuna mgahawa mmoja wa ajabu upo pale morogoro msamvu aisee, chakula kichafu, wanauza chakula cha 1500 kwa shs.8000, hata chakula cha mamantilie ni kuzuri afu wana customer care mbovu, ajabu sana. bora hata pale pa zamani.
Upo sahihi alichoandika mleta mada ni tofauti na uhalisia.

Shabiby ni gari yenye standard fulani hivi ya juu ila pale wanaposimama Morogoro karibu na Midland Hotel ni pa kichovu sana. Sina uhakika kama Management ya Shabiby huwa wanasimamia kila kitu ninahisi hili wamewaachia madereva na mautingo ambao wao hawawezi kujali sana.

Pale vyoo ni vibovu, vichafu na vinanuka. Chakula ni kibaya na bei ya ghali! Hao wanaouza ukiwasemesha mara mbili hawakujibu na wanabetua midomo na wengi wao ni mabinti ambao hawajui a wala b. Sasa njoo kwenye bei ya huo ubwabwa wa kiporo unaouziwa na uliopoa
 
Ni afadhali wapaki sehemu ya bei ya juu ila huduma ziwe zinaendana na wanachotoa. Utatumia hela nyingi ila utakula vizuri. Ila pia mabarabarani tunaposafiri chakula ni kati ya Sh. 5,000 hadi 10,000 sasa haya ndio mambo ya kulalamika kwamba bei ni juu kweli???

Naona bundles zimekuwa bei rahisi sana hadi vijana wa shule wanatulalamikia kwa mada potoshi. Tulalamikie huduma mbovu ila sio kuogopa kupelekwa sehemu za bei kubwa! Sasa mnataka kutuua kwa kipindupindu kwa mama ntulie kwa ugali na wali wa elfu mbili??? Yaani kabisa magari yakapaki kwa vibanda vya kuuza chakula cha elfu mbili na elfu tatu!!? Tutafuteni hela ndugu zangu.
 
Safari ni ya masaa mangapi mkuu?

Unaweza ukajibebea biskuti na soda au juisi kidogo kwa safari za ndani...
kaka ukiwa na hela huwezi kuchaguliwa cha kutumia na watu kama wewe, ila kama ndio hivyo tena ndio utakuwa unawaza ukae njaa hata kama inauma.
 
Basi kusimama hoteli au mgahawa fulani huwa ni mapatano ya madereva na wenye hoteli...

Madereva hupata kamisheni...

Upo sahihi alichoandika mleta mada ni tofauti na uhalisia.

Shabiby ni gari yenye standard fulani hivi ya juu ila pale wanaposimama Morogoro karibu na Midland Hotel ni pa kichovu sana. Sina uhakika kama Management ya Shabiby huwa wanasimamia kila kitu ninahisi hili wamewaachia madereva na mautingo ambao wao hawawezi kujali sana.

Pale vyoo ni vibovu, vichafu na vinanuka. Chakula ni kibaya na bei ya ghali! Hao wanaouza ukiwasemesha mara mbili hawakujibu na wanabetua midomo na wengi wao ni mabinti ambao hawajui a wala b. Sasa njoo kwenye bei ya huo ubwabwa wa kiporo unaouziwa na uliopoa
 
shida ni pale upo safarini(dharula)hii unataka uishi kama uko home,ule milo yote tena kwa kiwango kile kile😀😀,ndio sababu hamuishi kuomba kuchimba dawa.

unajua una safari,itoe zadaka tu siku hiyo kwamba ni ya kuteseka,ni korosho na maji au juice na soda,msosi unaoeleweka mpaka ufike.

ila hakikisha korosho au karanga hazina kawaida ya kukuviriga tumbo,usijeharibu safari zaidi.
 
Back
Top Bottom