Serikali yakana hukumu ya kuilipa ESCROW dola Mil 185. Dk. Abbasi asema Serikali haidaiwi

Aiseee siasa bana ni ushenzi ushenzi fulani.
Huoni kwanini elimu haichukuliwi kwa uzito mkubwa ni sababu watu wakielimika huwezi msumbua unless aamue tu yeye kujitoa ufahamu, ndio mana illiteracy rate ndio kundi kubwa la wanaokua manipulated haswa na hizi fafanuzi
 
IMG_1243.JPG
IMG_1244.JPG
 
Serkali hawahusiki hapo ufafanuzi mzuri sana


Yalipe yale mafisadi yaliyojificha nyuma ya IPTL
Akili za kuambiwa changanya na za kwako,IPTL walipo enda kukopa Malaysia mdhamini wao aLlikuwa serikali ya Tanzania , Benk ya standard charter asingetoa pesa Kama hakuna mdhamini, IPTL iko chali kwa Hiyo mdhamini lazima aingizwe kwenye deni .Mwansheria mkuu usitufanye wote wajinga
 
  • Thanks
Reactions: MTK
Tusiumize vichwa hapo, Mdhamini WA Haya makampuni ya IPTL yalikopa standard chartered bank ni serikali ya Tanzania , Kama mdaiwa halipi deni unamkunja mdhamini, hapo ndio serikali ya Tanzania inapoingia , Tujiandae tena Ndege yetu kukamatwa
 
Yu
Akizungumzia hukumu hiyo iliyotolewa Oktoba 9, mwaka huu, Dk. Abbasi amesema ameulizwa kuhusu hukumu hiyo, na hivyo amelazimika kutoa ufafanuzi.

“Msingi wa kesi zote mdaiwa siyo serikali wala Tanesco, ni deni la benki dhidi ya IPTL (kampuni ya kufua umeme ya Independent Power Tanzania Limited) walilorithi miaka mingi kutoka kwa wakopeshaji wa Malaysia.

Kwa muktadha huo na kisheria, serikali na Tanesco ziliunganishwa tu kama kanuni za kisheria zinavyomruhusu mdai kuwaunganisha wahusika wengine kwenye kesi ili kupata uhakika kuwa analipwa madai yake," amesema Dk. Abbasi.

“Kwa muktadha huo, natumia fursa hii kuwatoa wasiwasi Watanzania, serikali haidawi, haijawahi kukopa Standard Chartered ya Hong Kong, ila kama Baraza la Usuluhishi lilivyoamua, tutahakikisha tunasimamia utawala wa sheria kwa kuona IPTL wanalipa deni lao,” amesema Dk. Abbasi.

Katika kesi hiyo ya ICSID yenye namba ARB/15/41, benki hiyo ilifungua kesi dhidi ya serikali ikidai kiasi hicho cha fedha kwa kile ilichodai ni kutokana na kukiukwa kwa mkataba wa manunuzi ya umeme uliokuwa umetiwa saini baina yao na pande tatu za mkataba huo.

Benki hiyo ilikuwa ikiwakilishwa na Matthew Weiniger wa QC Linklaters LLP One, Iain Maxwell, Aaron McDonald, Elizabeth Kantor, Harry Ormsby, Gavin Creelman na Herbert Smith wa Freehills LLP, wote kutoka Uingereza.

Hukumu hiyo inaonyesha Serikali ya Tanzania iliwakilishwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Dk. Adelardus Kilangi, Wakili Mkuu wa Serikali, Dk. Clement Mashamba, Beredy Malegesi wa Crax Law Partners, Richard Karumuna Rweyongeza wa R. K. Rweyongeza & Co. Advocates, Galileo Pozzoli, Mark Handley, Profesa Tullio Treves, Luciana Ricart, Irene Petrelli, Renato Treves na Valerio Salvatori Curtis wa Mallet-Prevost, Colt & Mosle LLP.

Chanzo: Nipashe

Mwanasheria Mkuu wa Serikali leo katika mahojiano maalum na TBC amesisitiza kauli ya jana ya Serikali kupitia kwa
Msemaji Mkuu wa Serikali kuwa Serikali haidaiwi na katika uhusiano wa kibiashara kati ya IPTL na Benki ya SCB Hong Kong.

Serikali kama msimamizi wa utekelezaji itaibana kampuni ya IPTL ambayo bado ipo hapa nchini ikiwa na mitambo na raslimali nyingine, ikamilishe deni wanalodaiwa.


Hukumu kwa Kwa kifupi imesema;-
V. The Government of United Republic of Tanzania shall;-
Pay to climant the sum of USD 185,449,440.04 together with interest thereonat the rate of LIBOR (6-Months) +2% from the 1 September 2018until the date of full and final payment and
VI. Bear its own legal costs and expenses

Pia soma
Yu wapi Praise singer "extraordinary and plenipotentiary" Paskali Mayallah aunge mkono hoja hii mujarabu kwamba serikali haidaiwi hata kidogo na hukumu hii ya ICSID ni ya kutungwa na mabeberu wakiongozwa na Tundu Lissu???!!!
 
Akili za kuambiwa changanya na za kwako,IPTL walipo enda kukopa Malaysia mdhamini wao aLlikuwa serikali ya Tanzania , Benk ya standard charter asingetoa pesa Kama hakuna mdhamini, IPTL iko chali kwa Hiyo mdhamini lazima aingizwe kwenye deni .Mwansheria mkuu usitufanye wote wajinga
Abbas kasahau doctrine isemayo kwamba "Unaweza kuwahadaa baadhi ta watu kwa muda lakini huwezi kuwadanganya watu wote kwa wakati wote"!!; sooner rather than later the devil aka (pepo la udanganyifu) will catch up with you, big time!
 
Akizungumzia hukumu hiyo iliyotolewa Oktoba 9, mwaka huu, Dk. Abbasi amesema ameulizwa kuhusu hukumu hiyo, na hivyo amelazimika kutoa ufafanuzi.

“Msingi wa kesi zote mdaiwa siyo serikali wala Tanesco, ni deni la benki dhidi ya IPTL (kampuni ya kufua umeme ya Independent Power Tanzania Limited) walilorithi miaka mingi kutoka kwa wakopeshaji wa Malaysia.

Kwa muktadha huo na kisheria, serikali na Tanesco ziliunganishwa tu kama kanuni za kisheria zinavyomruhusu mdai kuwaunganisha wahusika wengine kwenye kesi ili kupata uhakika kuwa analipwa madai yake," amesema Dk. Abbasi.

“Kwa muktadha huo, natumia fursa hii kuwatoa wasiwasi Watanzania, serikali haidawi, haijawahi kukopa Standard Chartered ya Hong Kong, ila kama Baraza la Usuluhishi lilivyoamua, tutahakikisha tunasimamia utawala wa sheria kwa kuona IPTL wanalipa deni lao,” amesema Dk. Abbasi.

Katika kesi hiyo ya ICSID yenye namba ARB/15/41, benki hiyo ilifungua kesi dhidi ya serikali ikidai kiasi hicho cha fedha kwa kile ilichodai ni kutokana na kukiukwa kwa mkataba wa manunuzi ya umeme uliokuwa umetiwa saini baina yao na pande tatu za mkataba huo.

Benki hiyo ilikuwa ikiwakilishwa na Matthew Weiniger wa QC Linklaters LLP One, Iain Maxwell, Aaron McDonald, Elizabeth Kantor, Harry Ormsby, Gavin Creelman na Herbert Smith wa Freehills LLP, wote kutoka Uingereza.

Hukumu hiyo inaonyesha Serikali ya Tanzania iliwakilishwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Dk. Adelardus Kilangi, Wakili Mkuu wa Serikali, Dk. Clement Mashamba, Beredy Malegesi wa Crax Law Partners, Richard Karumuna Rweyongeza wa R. K. Rweyongeza & Co. Advocates, Galileo Pozzoli, Mark Handley, Profesa Tullio Treves, Luciana Ricart, Irene Petrelli, Renato Treves na Valerio Salvatori Curtis wa Mallet-Prevost, Colt & Mosle LLP.

Chanzo: Nipashe

Mwanasheria Mkuu wa Serikali leo katika mahojiano maalum na TBC amesisitiza kauli ya jana ya Serikali kupitia kwa
Msemaji Mkuu wa Serikali kuwa Serikali haidaiwi na katika uhusiano wa kibiashara kati ya IPTL na Benki ya SCB Hong Kong.

Serikali kama msimamizi wa utekelezaji itaibana kampuni ya IPTL ambayo bado ipo hapa nchini ikiwa na mitambo na raslimali nyingine, ikamilishe deni wanalodaiwa.


Hukumu kwa Kwa kifupi imesema;-
V. The Government of United Republic of Tanzania shall;-
Pay to climant the sum of USD 185,449,440.04 together with interest thereonat the rate of LIBOR (6-Months) +2% from the 1 September 2018until the date of full and final payment and
VI. Bear its own legal costs and expenses

Pia soma
Acheni uzwazwa. Nini maana ya kudhamini?
1. Mdhaminiwa asipotimiza matakwa ya makubaliano kati pande mbili za mkataba, mdhamini anawajibika, na
2. Serikali ya JMT haijabadilika. Viongozi wa kitaifa (marais) ndio wamekuwa wakipokezana nafasi.
Elewewaeni hilo. Madeni yaliyokopwa tangu enzi za Mwl Ñyerere ambayo bado kulipwa ni ya Tanzania. Rejeeni sakata la kushikiliwa ndege Afrika Kusini kufuatia Settler mdai kukazia hukumu mahakamani.
 
Waandishi wa habari wa Tanzania ni makanjanja kweli na ndio chanzo cha kupotosha jamii wakati kila kitu kimewekwa wazi au labda lugha shida.

Hakuna mahala serikari ilitoa udhamini kwa IPTL kukopa

1571405484431.png


Kwenye harakati za kukopa IPTL wali sign 'security deed' maana yake nini wakishindwa kulipa mdai anaweza kuchukua umiliki ya mali zao.

1571405548245.png


Mali walizokuwa tayari kutoa kwa security agent, wamiliki wa IPTL kwa mujibu wa mdeni ni share zote wanazomiliki kwenye kampuni.

1571405731187.png


Baada ya kupata mkopo wa kujenga na kununua mtambo wa kuzalishia umeme IPTL wakaingia mkataba wa kuuzia umeme TANESCO

1571405805852.png


Serikari ya Tanzania ichoahidi TANESCO wakishindwa kulipa hela za kununua umeme kutoka IPTL wao watalipa kwa ivyo waliidhamini TANESCO kulipia umeme kutoka IPTL iwapo watashindwa na sio udhamini wa deni la IPTL kwa bank walizokopa.

1571405905148.png


IPTL walidhamini share zao kwenye mabenki wakishindwa kulipa kampuni ichukiliwena kuendeshwa na mkopaji kama mali yao (this has nothing to do with the government) wao awajali nani mmiliki ilimradi wanauziwa umeme na kulipia.

1571406046724.png


Msisitizo ya kuwa wamiliki wa IPTL waliahidi kutoa shares zao wakishindwa kulipa deni kama makubaliano yao ya kukopa

1571406135282.png


Wakopeshaji ambae IPTL walitakiwa kuwalipa wanatajwa hapo juu na wakishindwa kampuni ni halali yao

1571406217479.png


Mwaka 2005 SCHK walipata umiliki wa hilo deni la IPTL kutoka kwa wakopeshaji na wanadai walivunja makubaliano ya malipo ivyo kwa mujibu security deed waliosaini iwapo watashindwa lipa mdeni atachukua shirika.
....................................................................................................................................................................................................

Ndio msingi wa kesi ya SCHK wao wamefungua kesi kama wamiliki wa IPTL kwa sababu wameshindwa lipa deni na wanadai serikari malipo kwa kutumia umeme wao kama walimiliki ya kampuni.

Upuuzu ni serikari kuwasikiliza badala ya kutaka kuona wanamalizana na shareholders wao waliokopa bank kwa sababu serikari aijui haswa masharti waliyokopea na watu waliokopa awajaenda mahakamani kujibizana na madai ya SCHK juu ya madai yao ya umiliki.
 
Escrow ni aina tu ya akaunti ya benki. Hata mimi ningeulizwa unadaiwa na Escrow ningekataa kama naisemea Serikali.

Deni ni la IPTL kusema ni la Escrow haileti maana yoyote.

Waandishi wengi wa Tanzania ni makanjanja sana na hawana ueledi.

Mazao ya shule za kusomea ujinga yametamalaki kila pembe.
Umeisoma hukumu? Kama hujasoma nikusamehe, kama umesoma na kuandika haya unakoelekea siko wahi mapema matibabu ya...
 
Serkali hawahusiki hapo ufafanuzi mzuri sana


Yalipe yale mafisadi yaliyojificha nyuma ya IPTL
V. ◇The Government of United Republic of Tanzania◇shall;-
Pay to climant the sum of USD 185,449,440.04 together with interest thereonat the rate of LIBOR (6-Months) +2% from the 1 September 2018until the date of full and final payment....

Kuna sehemu imetaja IPTL hapo?

Huu uzuzu wa kuona watanzania mazuzu ukome!!!
 
Aisee hili swala angelizungumzia Mwanasheria Mkuu wa Serikali maana hawa baadae watakuja kuruka hukumu inasema wewe unadaiwa unaleta viswahili vya tuliunganishwa tuu kwenye kesi...
 
Kule Afrika Kusini ndege haiendi tena.
London ndege haiendi tena.

Bado wale jamaa wa Bagamoyo
Bado Symbion mmmmmh
Kweli Mabeberu si mchezo
IHiyo ya ndege na vijikesi vidogp vidogo ilikuwa rasha rasha cinema kamili ingekuja anageendelea na ujinga wake. Tuliyaona wakati wa Nyerere, mpaka sabuni ya kuongea tulikosa.

Tuwaone na Wazimbabwe walifanywa nini wakati wa Mugabe?

Hii mijitu mingine ni baraka ya kujua kufunga tai tu shingoni lakini vichwani ni zero kabisa. Tulifanya makosa makubwa sana CCM kuchagua mtu ambae hana asili ya uongozi.
 
IHiyo ya ndege na vijikesi vidogp vidogo ilikuwa rasha rasha cinema kamili ingekuja anageendelea na ujinga wake. Tuliyaona wakati wa Nyerere, mpaka sabuni ya kuongea tulikosa.

Tuwaone na Wazimbabwe walifanywa nini wakati wa Mugabe?

Hii mijitu mingine ni baraka ya kujua kufunga tai tu shingoni lakini vichwani ni zero kabisa. Tulifanya makosa makubwa sana CCM kuchagua mtu ambae hana asili ya uongozi.
pole bi faiza si ndo mnapenda hayamambo... mnasema kazi iendelee etiee 😂 😂
 
Back
Top Bottom