Influenza
JF-Expert Member
- Jul 1, 2018
- 1,445
- 3,403
Serikali ya Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam imetoa saa 72 kwa Bodi ya Mikopo (HESLB) kutekeleza maagizo 4 likiwamo kuwaingizia fedha wanafunzi ambao hawajapewa tangu chuo hicho kifunguliwe, yasema isipotekeleza watakusanyika nje za ofisi ya HESLB.
Taarifa iliyotolewa na Waziri wa Habari na Mawasiliano wa Daruso, Judith Mariki ilisema wamefikia uamuzi huo baada ya changamoto ya kukosekana kwa mikopo kwa wanafunzi wengi wa mwaka wa kwanza tangu chuo kifunguliwe huku baadhi ya wanafunzi wanaoendelea wakikatwa fedha zao.
DARUSO wamesema kuwa baada ya muda huo wanafunzi wote ambao hawajilipwa mikopo , wamekatwa mikopo yao, wamepewa mikopo kwa waliokata rufaa na kubadili Ofisa mikopo wa chuo hicho wataandamana nje ya ofisi za bodi hiyo
“Wanafunzi wamevumilia vya kutosha na mazungumzio yamefanyika vya kutosha, ahadi za uongo tumepewa za kutosha, hivyo endapo saa 72 zitaisha bila mambo hayo yote kutekelezwa kwa pamoja, Daruso tukutane nje ya ofisi ya ofisa mikopo ili kwa umoja wetu tuelekee HESLB.” imenukuliwa Taarifa hiyo
Zaidi, soma:
Taarifa iliyotolewa na Waziri wa Habari na Mawasiliano wa Daruso, Judith Mariki ilisema wamefikia uamuzi huo baada ya changamoto ya kukosekana kwa mikopo kwa wanafunzi wengi wa mwaka wa kwanza tangu chuo kifunguliwe huku baadhi ya wanafunzi wanaoendelea wakikatwa fedha zao.
DARUSO wamesema kuwa baada ya muda huo wanafunzi wote ambao hawajilipwa mikopo , wamekatwa mikopo yao, wamepewa mikopo kwa waliokata rufaa na kubadili Ofisa mikopo wa chuo hicho wataandamana nje ya ofisi za bodi hiyo
“Wanafunzi wamevumilia vya kutosha na mazungumzio yamefanyika vya kutosha, ahadi za uongo tumepewa za kutosha, hivyo endapo saa 72 zitaisha bila mambo hayo yote kutekelezwa kwa pamoja, Daruso tukutane nje ya ofisi ya ofisa mikopo ili kwa umoja wetu tuelekee HESLB.” imenukuliwa Taarifa hiyo
Zaidi, soma:
Mkuu wa Serikali ya wanafunzi (DARUSO) na wenzake, wasimamishwa masomo kwa muda usiojulikana
Habari za muda huu! Kiongozi wetu mkuu wa serikali ya wanafunzi DARUSO ndugu Hamis Musa Hamis amekabidhiwa barua ya kuondoka chuoni kwa muda usiojulikana muda si mrefu kutokea sasa. MWENDELEZO: Viongozi wengine wa DARUSO waliosimamishwa masomo UDSM ni pamoja na Kasim Ititi-Mwenyekiti wa Bunge...
www.jamiiforums.com