Serikali na jamii kwa ujumla tuwasaidie bodaboda Arusha kutoka kwenye mtazamo usiofaa

Matongee

JF-Expert Member
Jun 17, 2023
253
629
WanaJF ninaandika nikiwa na hasira zilizochanganyikana na huzuni kuhusu kinachoendelea huko Arusha. Kwanza kabisa niseme mimi ni mzaliwa wa Arusha na nimekulia huko. Kilichonitoa Arusha ni elimu ngazi ya chuo kikuu. Nitakachoandika hapa sio stori za kuhadithiwa au kuona kwenye media.

Kwa miaka ya karibuni hasa mwaka huu kumeripotiwa ajali nyingi za pikipiki zilizoondoa maisha ya vijana wengi na kuwaachia wengine ulemavu. Tofauti na sehemu zingine kwa Arusha imeonekana hii misiba ni kawaida hali inayopelekea kuwepo na masikhara mengi sana misibani. Vyombo vya habari hasa vya mitandaoni vimekuwa mstari wa mbele kuripoti masikhara yanayofanyika misibani huku msiba wenyewe ukipewa uzito mdogo. Mkipita kwa Millard Ayo na online media zingine mtaona vijana wa Arusha maarufu kama machii wa R wakifukia makaburi kwa mikono kama kuonyesha heshima kwa mwenzao. Ule ni upuuzi unaopelekea kuonekana kama ajali iliyotoa uhai ni jambo dogo.

Pamoja na ajali za pikipiki pia kuna tabia ya vijana wengi wa Arusha kufanya bidii waonekane wao ni wahuni kuanzia mavazi hadi kuongea. Wazazi na walezi wengi wanaugulia ndani kwa ndani hakuna namna. Mimi ninakataa kabisa huu USELA MAVI wa hawa vijana. Vijana wengi wameacha kusoma na kukimbilia bangi, pombe na mambo mengine ya kijinga. Media pia zimekuwa na ujinga wa kupromoti huu upuuzi wa Machalii wa R.

Pichani dada maarufu mitaa ya Kijenge aliyefariki kwa ajali ya pikipiki mwaka jana. Alijulikana kwa jina maarufu LA MAMA. Huu msiba uliniuma sana. Ndoto zangu nyingi kwa huyu hayati "La mama" zilizimika.
FB_IMG_1668892460839.jpg
 
Huwa inaumiza pale ambapo matendo yao yanaumiza wasiohusika. Ila kama tabia zao za kipumbavu ni kwa maangamizi yao wenyewe sioni kama ni tatizo. Ardhi ya kuzika ipo ya kutosha; ondoa shaka.

Uhai ni kitu cha kutunza mno; ukishatoka haurudi. Kama kuna wajinga wameamua kuchezea uhai wao wenyewe tena wakijua matokeo yake nani apoteze muda kuwasaidia wajinga wa calibre hiyo?

Je, haikunenwa, kuvuja kwa pakacha nafuu ya mchukuzi? Na liendelee kuvuja wapo watakaojifunza kwa hiari bila kutumia gharama kubwa kumfunza mjinga.
 
MIMI SIONI TATIZO MTU AKIFA KWASABAB YA UPUMBAV WAKE MWENYEW NA ANAJUA NI HATARI...
Acha wafe tu maana wanajiona wao ndio wamezaliwa kuchezea pikipik wao ndio masela w taifa...
Police wenyew wamewachoka... By the way kama taifa tuna vijana wengi ambao hawajitambui acha wasio jutambua wafe
 
WanaJF ninaandika nikiwa na hasira zilizochanganyikana na huzuni kuhusu kinachoendelea huko Arusha. Kwanza kabisa niseme mimi ni mzaliwa wa Arusha na nimekulia huko. Kilichonitoa Arusha ni elimu ngazi ya chuo kikuu. Nitakachoandika hapa sio stori za kuhadithiwa au kuona kwenye media.

Kwa miaka ya karibuni hasa mwaka huu kumeripotiwa ajali nyingi za pikipiki zilizoondoa maisha ya vijana wengi na kuwaachia wengine ulemavu. Tofauti na sehemu zingine kwa Arusha imeonekana hii misiba ni kawaida hali inayopelekea kuwepo na masikhara mengi sana misibani. Vyombo vya habari hasa vya mitandaoni vimekuwa mstari wa mbele kuripoti masikhara yanayofanyika misibani huku msiba wenyewe ukipewa uzito mdogo. Mkipita kwa Millard Ayo na online media zingine mtaona vijana wa Arusha maarufu kama machii wa R wakifukia makaburi kwa mikono kama kuonyesha heshima kwa mwenzao. Ule ni upuuzi unaopelekea kuonekana kama ajali iliyotoa uhai ni jambo dogo.

Pamoja na ajali za pikipiki pia kuna tabia ya vijana wengi wa Arusha kufanya bidii waonekane wao ni wahuni kuanzia mavazi hadi kuongea. Wazazi na walezi wengi wanaugulia ndani kwa ndani hakuna namna. Mimi ninakataa kabisa huu USELA MAVI wa hawa vijana. Vijana wengi wameacha kusoma na kukimbilia bangi, pombe na mambo mengine ya kijinga. Media pia zimekuwa na ujinga wa kupromoti huu upuuzi wa Machalii wa R.

Pichani dada maarufu mitaa ya Kijenge aliyefariki kwa ajali ya pikipiki mwaka jana. Alijulikana kwa jina maarufu LA MAMA. Huu msiba uliniuma sana. Ndoto zangu nyingi kwa huyu hayati "La mama" zilizimika.
View attachment 2703417
Mimi naona ingewezekana vijana wa Mwanza wangekusanywa ingalau waende wakawatie adabu
 
Huu utamaduni unashamiri kwa kasi Arusha, na usipodhibitiwa mapema itakuwa janga kubwa.

YAFANYIKE YAFUATAYO:

(1). Online media zipigwe marufuku kuripoti matukio ya hawa machalii/ wadudu.

(2). Vijiwe vyote vya bodaboda vilivyosajiliwa vipewe ruhusa ya kumkamata yeyote anayeendesha pikipiki kwa mbwembwe na kutoa taarifa polisi. Adhabu iwe Kali kwa atakayekutwa na kosa.

(3). Mashindano ya pikipiki aina ya bodaboda yapigwe marufuku.
 
Umeongea ukweli Arusha kimsingi wengi hasa vijana ni washamba na hawajielewi, hakuna mtu mwenye akili akaona kufanya usela mavi ni ujanja, bangi, pombe, mrungi ndio sifa yao kuu lakini hua nawaonea huruma wakifika Dar na usela mavi wao wanakua wadogo kama karanga na hawana swaga wanaishia kuonekana mandina tu
 
Kumepambazuka masela mavi wa R waje kushambulia mtoa hoja na kuona chugs ni Jiji kuu kuliko mwanza.
Bahati nzuri na mimi ni wa Chuga 100%. Hakuna kitu wataongea nisijue. Tunataka Arusha yenye vijana wanaowaza maendeleo na kujituma sio kutokea kwenye media kama wavuta bangi na walevi.
 
Huu utamaduni unashamiri kwa kasi Arusha, na usipodhibitiwa mapema itakuwa janga kubwa.

YAFANYIKE YAFUATAYO:

(1). Online media zipigwe marufuku kuripoti matukio ya hawa machalii/ wadudu.

(2). Vijiwe vyote vya bodaboda vilivyosajiliwa vipewe ruhusa ya kumkamata yeyote anayeendesha pikipiki kwa mbwembwe na kutoa taarifa polisi. Adhabu iwe Kali kwa atakayekutwa na kosa.

(3). Mashindano ya pikipiki aina ya bodaboda yapigwe marufuku.
Hakika umenena
 
Vijana wa Arusha ni vijana wa hovyo sana nchi hii. Wana usela mavi sana hata huku dar nawaona kwenye vijiwe vya boda boda matendo Yao ni tofauti kabisa na wenzao wa mikoa mingine.

Arusha wasipokua makini miaka ijayo watakuwa na uhaba mkubwa sana wa vijana wanaojitambua.

Serikali piga marufuku vipombe vya buku buku vinaua vijana
 
Vijana wa Arusha ni vijana wa hovyo sana nchi hii. Wana usela mavi sana hata huku dar nawaona kwenye vijiwe vya boda boda matendo Yao ni tofauti kabisa na wenzao wa mikoa mingine.

Arusha wasipokua makini miaka ijayo watakuwa na uhaba mkubwa sana wa vijana wanaojitambua.

Serikali piga marufuku vipombe vya buku buku vinaua vijana
Tumeshaliona tatizo tunapambana nalo
 
Hawa jamaa wa chuga R Huwa wananifurahishaga sana kwa namna wanavyojichukulia hasa katika mavazi na life style kwa ujumla..

Wanajiona wao ndiyo wajaaaanja kumbe tunawachora tu na kuwaona kama mandezi fulani hivi!!!
 
Back
Top Bottom