Ajali za bodaboda ni sawa na ugaidi au mauji ya risasi Marekani

Nyamesocho

JF-Expert Member
May 5, 2023
476
1,244
Ingekuwa ni kikundi cha ugaidi kinaua Watanzania basi serikali ingetoa kila aina ya silaha kupambana nacho au angekuwa ni mtu anawapiga risasi raia wasio na hatia basi jeshi la polisi lingekuwa na operation za hatari.

Ajali zinazosababishwa na bodaboda ni zaidi ya ugaidi au mauaji ya kuwafyatulia risasi raia mtaani huku serikali ikiwa kimya kuhusu haya mauaji yanayoondoa watanzania kwa kila saa.

Binafsi ndani ya miaka 2 tu nimeshuhudia watu 6 tuliokuwa tunafahamiana wamekufa kwa sababu ya ajali za bodaboda kwa muda tofauti tofauti kwa nini huu usiwe ugaidi?

Serikali imekaa kimya huku jamii za kitanzania kila kukicha wanazika wenzao kwa sababu ya bodaboda na wengine wakiachiwa na ulemavu wa kudumu, kwa mfano kila familia ya Kitanzania imezika ndugu jamaa au rafiki kwa sababu ya bodaboda.

Hatukatai bodaboda imerahisisha usafiri na ajira kwa vijana lakini tunapoteza watu wengi sana kwa sababu ya bodaboda.

Serikali iandae utaratibu mpya wa bodaboda kudhibiti ajali, na waendesha bodaboda wapimwe akili, haiwezekani mwendesha bodaboda aondoke kwa speed 120 umbali wa mita 100.

Serikali ije na mpango mkakati kupunguza au kuondoa ajali za bodaboda, huu ni zaidi ya ugaidi tofauti yake ni ndogo tu, ugaidi watu wengi wanauawa kwa muda mfupi lakini huu watu wachache wanakufa kwa saa na serikali ipo tu.

Na serikali ianzishe kitengo cha kutoa takwimu za ajali za bodaboda kila mwezi ili jamii ichukue tahadhari.
 
Lema aliwaambia kuendesha bodaboda ni umaskini mkabisha, dunia ya kwanza hakuna huu ujinga.
 
Boda boda ni janga mazee, hapo kwenye speed 120 ndani ya Mita 100 ni kisanga Sana, Dar er Salaam ni too dangerous kupanda boda, mara mia Kodi bajaji lakini sio Bodaboda panda akutoe home akusogeze njia kuu.

Ila kupanda boda highway au any congested main road ni death sentence, mbali na hvyo ajali za barabarani zimekuwa too much, ukiachana na hili kundi la boda.

Serikali ifanye mkakati wa kupiga 4 lanes kwa njia zifuatazo, Dar-Arusha, Dar-Mwanza, Dar-Mbeya, hizo njia ajali za kugongana uso kwa uso ni nyingi sana na nyingi huwa haziripotiwi.
 
Boda boda ni janga mazee , hapo kwenye speed 120 ndani ya Mita 100 ni kisanga Sana , Dar er salaam ni too dangerous kupanda boda ,
Nakuunga mkono, ajali zinazosababishwa na bodaboda nyingi haziripotiwi ndo maana hata jamii wanaona siyo janga lakin hili ni janga la kitaifa, watu wanaokufa kwa sababu ya bodaboda ni wengi mnoo
 
Bodaboda wenyewe wanasikia
Mshaambiwa sana hamsiki,mmeachwa sasa yanayowakuta mamlaka hata haijali

Ova
 
Kuna bodaboda na bajaji Hawa jamaa wakiwa barabani akili zao huwa wanazijua wenyewe,,
 
Watu wawili Kijiji cha Soroneta na Nyamwigura Wilaya ya Tarime wamefariki baada ya kugongwa na bodaboda aliyekuwa amelewa
 
Kwa dar ni safe zaidi ukipanda daladala kuliko boda boda. Nafikiri tukiweza ku control fujo zao wanapokua kwenye makutano ya barabara itasaidia.

Pia kwa nature ya ujenzi wa barabara za dar haziachi nafasi kwa ajiliya waendesha baiskel na boda boda
 
Jana tumemzika jamaa hapa Mpwapwa mjini , ambaye ni bodaboda.. amefariki kwa kugongana na bodaboda mwenzake.
 
Bodaboda unakuta yuko speed rough road halafu anapokea simu anabaki anaendesha kwa mkono mmoja. Hawa jamaa ni walishajikatia tamaa wenyewe.
 
Back
Top Bottom