Anna Nkya
Member
- Oct 21, 2021
- 69
- 341
Rais Samia amerudi leo kutoka Scotland na ameingia kazini moja kwa moja.
Alipotoka kukagua ujenzi wa Daraja la Tanzanite (Lile la juu ya Bahari pale Salenda) alienda kuongea na wananchi wanaofanya biashara pale Coco Beach.
Akiwa hapo ameeleza nia njema ya Serikali katika zoezi la kuwapanga wamachinga akieleza kwamba nia ni kufanya majiji yetu yawe katika usafi na mpango mzuri.
Hapo pia amesema kwamba tayari ameagiza watendaji husika kuanza mara moja ujenzi wa majengo mapya kwenye soko la Kariakoo, ambapo ujenzi huo utawezesha machinga zaidi ya 2,300 kupata nafasi nzuri ya kufanya biashara zao.
Amesema pia kuna mpango wa kujenga soko kubwa katika eneo la Jangwani.
Rais Samia amedhamiria kutekeleza zoezi la kuwapanga vizuri machinga katika namna yenye tija pana kwa nchi yetu.
Alipotoka kukagua ujenzi wa Daraja la Tanzanite (Lile la juu ya Bahari pale Salenda) alienda kuongea na wananchi wanaofanya biashara pale Coco Beach.
Akiwa hapo ameeleza nia njema ya Serikali katika zoezi la kuwapanga wamachinga akieleza kwamba nia ni kufanya majiji yetu yawe katika usafi na mpango mzuri.
Hapo pia amesema kwamba tayari ameagiza watendaji husika kuanza mara moja ujenzi wa majengo mapya kwenye soko la Kariakoo, ambapo ujenzi huo utawezesha machinga zaidi ya 2,300 kupata nafasi nzuri ya kufanya biashara zao.
Amesema pia kuna mpango wa kujenga soko kubwa katika eneo la Jangwani.
Rais Samia amedhamiria kutekeleza zoezi la kuwapanga vizuri machinga katika namna yenye tija pana kwa nchi yetu.