Serikali kununua ndege nyingine ya Boeing 787

Serikali kununua ndege nyingine ya Boeing 787

Sasa nini kinaweza rekebisha uchumi uliokufa..?
Matrekta, planter na mbolea zinazowafikia wakulima kwa wakati. Kilimo kinachangia pato la taifa kwa 60%+, wala sio bombadier. Kila alie hai anahitaji chakula, sio kupaa hewani
 
Hii Habari asiisikie Tundu Lissu vinginevyo watamrudisha ICU, kwa chuki aliyonayo dhidi ya nchi yetu!
Mkuu naona unatekeleza kwa vitendo mafunzo yako ya ujasusi, mmeshindwa physical elimination Sasa ni character killing, sawa bhana, haishangazi maana tawala zote korofi watu Kama wewe wanakuepo huitwa henchmen
 
Wanasahau kilimo wako busy kununua ndege wanasahau hiyo ni biashara kama biashara zingine hivyo inapaswa kwenda nayo taratibu na kwa uangalifu.

Hizi Bomberdier mbili zilizopo hata hatujui perfomance ikoje maana hata utoaji wa taarifa zake haueleweki.
Zinafanya vizuri kiasi zimeisha ingiza zaidi ya 20b bila kuondoa gharama.
 
Jambo jema sana, ila naiomba serikali isilipe cash hata kama fedha inazo

Serikali iwalipe watengenezaji mara tu zitakapo wasili Tanzania

Huwa nina hisia kuwa malipo ya cash kwa ndege zilizopita nayo yamechangia kukamatwa kwa moja ya Bombadier yetu


Niko tayari kurekebishwa kama ninakosea
Hii Sasa tuombe Sana isikamatwe maana ikiwa hivyo lazima tu mzalendo mmojawapo atalifahamisha taifa, ataitwa msaliti na atatumiwa Nissan nyeupe hakuna uhakika wa kupona Kama yule wa mwanzo. Mimi naona Bora madege yenu yaacheni hukohuko sisi tubaki salama, kwani thamani ya ndege Ina zidi uhai wa mtu
 
Hili ni jambo zuri kwa serikali kwenye dhamira yake ya kufufua shirika letu la ndege, lakini vilevile lazima ijitahidi kugusa sehemu kubwa ya uchumi ambao unagusa(unamilikiwa) wengi hasa kwenye sekta ya kilimo na viwanda ingependeza sana kama serikali ingejikita intensively kusaidia kuinua kilimo hasa wakulima wadogowado na kuwatafutia masoko ndani na nje ya nchi.

Japo hili linalofanywa na serikali nalo lina mchango wake kwenye ufufuaji Wa uchumi hongera mh.raisi kwa kufufua hili shirika ambalo lilishafariki.
Kupanga ni kuchagua toka uhuru unazungumzia kilimo,kilimo kipi,nchi inahitaji kuangalia fursa zingine makosa yalishafanyika kwa kukaribisha wageni ambao walikuja kwa mgongo wa kufanya tafiti na matokeo yake unayajua!tanzania kama tanzania haina tena ardhi bora ya kilimo.
 
Aisee hii wakiidaka tena,mzee lazima asogeze vifaru boda aisee
 
Ukitoa kununua ndege na wapinzani, CCM haina cha kujigamba zaidi ushetani wanaoufanya
 

Lisu na Zito Kabwe hawapendi kusikia nchi ikipiga hatua, wao hupenda kusikia ikishindwa ili wapate kukosoa
kwako unaona kununua ndege ni hatua za ki maendeleo lakini vp wananchi kukosa pesa kutokana na kuwa biashara hazifanyiki ni hatua gani hiyo ? Au hizo ndege unataka ufanye biashara na watu wa kutoka wapi wakati watu wako una zidi kuwa nyang"anya uwezo wa kujitegemea kiuchumi. Au labda huo ndio uchumi wa viwanda ambao sasa hata wimbo wake hausikiki tena hata kwa hao viongozi, kama tume potea njia sio vibaya tukarudi nyuma ili tupate muelekeo ulio sahihi tupate kusonga mbele, na njia sahihi ni kuwekeza kwenye kilimo. Ondoa kwanza njaa ndio utapata uwezo wa kujiamiani.
 
Kabla ya Magufuli waliotangulia hawakununua ndege kilimo kilikuwaje?

Chifu, kama umesoma nilichosema mwanzo, utaona kwamba anachokifanya Magufuli kwenye kilimo ni muendelezo wa sekta hiyo kutelekezwa, at least kutokea mwaka 2003, ambapo Tanzania ilikubali uamuzi (wa Maputo Declaration) kwamba ili kuinua kilimo na kuondoa umaskini wa wakulima Afrika, kila nchi itenge asilimia 10 ya national budget kwenye kilimo.

Na ukitumia a broader picture, tokea Tanzania imekubali sera na miongozi ya kiuchumi ya IMF/Benki ya Dunia miaka ya 1980, kilimo ndipo kilipoanza rasmi kutelekezwa. Sera na miongozo hiyo ililazimisha serikali kupunguza uwekezaji kwenye kilimo (pembejeo na mafunzo na ajira kwa agro extension officers).

Sasa kwa mtu anayejiita ni ‘Rais wa wanyonge’, nilitarajia angefanya kinyume na Mwinyi, Mkapa na Kikwete, kwa kuwekeza kweli kwenye kilimo. Kama taifa litatengenezwa na takribani asilimia 70 ya watu walio subsistence farmers (peasants), haingii akilini kutenga TZS 500B kununua ndege, huku ukiweka TZS 24B kwenye kilimo (15B zikiwa ni fedha za nje).
 
Back
Top Bottom