Serikali kununua ndege nyingine ya Boeing 787

Serikali kununua ndege nyingine ya Boeing 787

Serikali ya Tanzania ipo katika hatua za mwisho kununua ndege nyingine ya Boeing 787.

Itakumbukwa ya kwamba serikali washa-order ndege nne, ambazo ni Boeing787, CS300 na Bombardier q400, ndege zote Zitawasili July mwaka huu.

Source: Aviation Tanzania
Inayonunua ni Seikali ya Tanzania au ni Tanganyika?
 
Serikali ya Tanzania ipo katika hatua za mwisho kununua ndege nyingine ya Boeing 787.

Itakumbukwa ya kwamba serikali washa-order ndege nne, ambazo ni Boeing787, CS300 na Bombardier q400, ndege zote Zitawasili July mwaka huu.

Source: Aviation Tanzania
ilikuwa july 17 sasa 18....????sawa
 
Safi sana,naziona hizi Bombadier zinavyotesa,itafikia mahali hata wazungu watatuamkia..
 
ana chuki dhidi ya makafiri wa ccm
watekaji na wapiga risasi..
walafi wanaoishi ikulu tangu uhuru..
wanaogeuza vyombo vya ulinzi na usalama sehemu ya chama.
Hiyo chuki ina gharama though, hope umeviona na vile viguu!
 
Hii Habari asiisikie Tundu Lissu vinginevyo watamrudisha ICU, kwa chuki aliyonayo dhidi ya nchi yetu!
BWANA YULE HANA HATA CHEMBE YA UZALENDO KWA NCHI YAKE. MBAYA ZAIDI HATA ADABU KWA VIONGOZI HANA KABISA!
 
Ukiangalia comments nyingi humu jamiiforum siku hizi unagundua wale wajinga wa instagram na facebook ndo wamevamia ila the great thinkers hawamo tena.
Kumbe na wewe ni Mjinga mojawapo? Maana haya maoni hujayatolea Mbinguni bali JF. Basi jitambue na ondoa ujinga
 
Serikali iweke vipaombele, sekta kubwa inayoingizia taifa mapato mengi na kuajiri watu wengi ni kilimo, fedha zote hizo za hizo ndege kama Mungu angewafungulia fikira hawa viongozi wetu wakawekeza kwny kilimo hasa pembejeo na umwagiliaji, leo hii wanyonge wengi sana wangepata neema kubwa na uhitaji wa viwanda ungekua kwa kasi ya ajabu. Lakini wapi bhana, mtu mweusi hata asome vp fahari yake ipo kwny vitu, yaani magari, nguo, majumba nk.
Nchi hii hv sasa hatujui hasa dira yetu ni ipi kwny uchumi, Rwanda nawaelewa sana wamejikita kwenye ICT na conference facilities kutokana na mazingira ya nchi yao ndogo, na wanayo haki ya kukuza shirika lao la ndege kutokana na hiyo dira ya pili kuwa centre ya mikutano mikubwa Africa mashariki na kati. Sasa hapa kwetu safari tunayo, huyu akiondoka yule atakaye kuja ataturudisha pia sehemu tofauti na hayo mandege yaani hakuna muendelezo. Aliyetoka alisema Kilimo kwanza, huyu kaja anasema kazi tu, ipi hasa haijulikani ni fully mseto
 
Umeongea logic na point Sana mkuu.Ila tambua pia ya kwamba serikali haifanyi kwa mtu mmoja mmoja ila majority.Unapowekeza kwenye airline sio mbaya at all coz inaboost sekta ya utalii Sana kwasababu huwezi kufanikiwa kwenye utalii without a stable airline company ambayo itaitangaza nchi ughaibuni.Mind you utalii utaongeza fedha za
kigeni ambazo Zita boost
uchumi pia in one way or
another.So kenya,Rwanda
Ethiopia sio wajinga kuinvest
kwenye airlines companies
mkuu.

Utalii ni biashara nzuri lakini sisi tumechelewa sana! Ni kujidanganya nchi nchi inapoamua kutumia rasilimali zake nyingi kununua Madege ya kubeba watalii wakati ULAYA NA SEHEMU NYINGINE DUNIANI KUMEJAA MA ZOO NA WANYAMA WOTE TULIISHASAFIRISHA WAKIWA HAI. HEBU PELEKENI PESA KWENYE KILIMO JAMANI!
 
Ukiangalia comments nyingi humu jamiiforum siku hizi unagundua wale wajinga wa instagram na facebook ndo wamevamia ila the great thinkers hawamo tena.
Kumbe na wewe ni mmojawapo uliyetoka Instagram na facebook. Jitambue na Uache ujinga ili na wengine waache ujinga, maana haya maoni yako hajatumia mbingu kufikisha hapa
 
Utalii ni biashara nzuri lakini sisi tumechelewa sana! Ni kujidanganya nchi nchi inapoamua kutumia rasilimali zake nyingi kununua Madege ya kubeba watalii wakati ULAYA NA SEHEMU NYINGINE DUNIANI KUMEJAA MA ZOO NA WANYAMA WOTE TULIISHASAFIRISHA WAKIWA HAI. HEBU PELEKENI PESA KWENYE KILIMO JAMANI!
Tumechelewa kila kitu mkuu..Ndio tunaanza upya sasa..Awamu iliyopita ilikua kilimo kwanza lakini bado ili fail sio mbaya tukijaribu na huku.
 
Sasa nini kinaweza rekebisha uchumi uliokufa..?
Wekeza kwenye kilimo. Asilimia karibu 70 ya watanzania ni peasants. Tanzania inatengenezwa na agrarian societies. Ni mjinga ama mpumbavu tu anayefikiri nchi hii itaendelea na watu wake kutokuwa maskini kwa kuitekeleza sekta ya kilimo. Serikali ilikubali kutenga asilimia 10 ya bajeti yake kwenye kilimo toka mwaka 2003, lakini hadi leo haijawahi hata kutenga asilimia 5!

Kilimo na wakulima wakifanikiwa, kunakuwa na multiplier effects kwenye sekta zingine kama vile viwanda, uhifadhi wa mazingira, na hata ongezeko la purchasing power ya wananchi.

Yaani hii ni basic economics! Lakini clueless Magufuli haelewi hili!
 
Wekeza kwenye kilimo. Asilimia karibu 70 ya watanzania ni peasants. Tanzania inatengenezwa na agrarian societies. Ni mjinga ama mpumbavu tu anayefikiri nchi hii itaendelea na watu wake kutokuwa maskini kwa kuitekeleza sekta ya kilimo. Serikali ilikubali kutenga asilimia 10 ya bajeti yake kwenye kilimo toka mwaka 2003, lakini hadi leo haijawahi hata kutenga asilimia 5!

Kilimo na wakulima wakifanikiwa, kunakuwa na multiplier effects kwenye sekta zingine kama vile viwanda, uhifadhi wa mazingira, na hata ongezeko la purchasing power ya wananchi.

Yaani hii ni basic economics! Lakini clueless Magufuli haelewi hili!
Sawa nakubaliana na wewe chief ila awamu iliyopita c iliweka mkazo kwenye kilimo kwa kauli mbiu ya kilimo kwanza?lakini what happened?hebu tujaribu na huku kdgo mkuu tuone.
 
Kwan mwezi wa saba mbalii??
 
Back
Top Bottom