Sasa hivi inatosha tu kwa Waislamu kutangaza kuandamana na serikali itatuma Polisi, FFU, Mgambo au hata JWTZ! kwa wasioona mbali wanaona kuwa hili ni suluhisho sahihi.
Wasichokijua hapa ni kuwa kama Waislamu wataamua kucheza gemu la kutangaza maandamano kila ijumaa na serikali kupeleka vyombo vya usalama misikitini kila ijumaa ukijumlisha na upelekaji wa hivi vyombo kwenye kesi za kina Sheikh Ponda basi ni gharama kubwa sana kiuchumi ambayo serikali inaingia kila Ijumaa.
Vilevile bajeti ya ulinzi nayo inaongezeka, kwa nchi changa kama Tanzania serikali haitaweza kufanya hivi kila ijumaa bila ya nchi kuyumba kiuchumi.
Tathmini yangu inanionyesha na nadhani kuna watakaokubaliana nami kuwa Waislamu wa Tanzania sasa wana uwezo wa kuifyonza nchi kiuchumi! matokeao yake ni kuwa kama yale ya baada ya vita na Uganda, hata Wakristo wanaochekelea kupigwa kwa Waislamu sasa wajue kuwa hizo hela za MoU zitapungua sana kwenda kwao.
Tunachodai Waislamu si Serikali kutuletea jua au mwezi mkononi! ni madai ya haki na ya kimsingi ambayo yanatekelezeka na yoyote yule anayependa uadilifu, vinginevyo subirini nchi kufilisika kabla ya kwenda hatua nyingine.