Serikali iunganishe Dar na Pwani uwe mkoa mmoja uitwe Dar ili watu wazidi kusogea nje ya mji

Hakuna sehemu nimesema Dar imejaa hoja yangu ya kuongeza ukubwa siyo kwa sababu eti Dar imejaa, Dar bado haijajaa hoja yangu ni Dar ndio mkoa mdogo kuliko yote, yet ndio mkoa wenye idadi kubwa ya watu kuliko yote hii sidhani kama ni sawa
Mkuu mimi nimekuelewa vizuri sana,hoja yangu iko na mashiko sana.
Ikifanyika hivyo maendeleo yatagawanyika kwa usawa kuliko hali ya sasa ya watu kurundikana na kufanya maendeleo sehemu moja na sehemu zingine zinabaki mapori miaka na miaka.
Ukitembelea hata hapo Kenya kuna utofauti unaona kwenye mikoa yao yote ina mgawanyo sawa wa kimaendeleo na watu hawarundikani sehemu moja.
 
Heri ya mwaka mpya wakuu

Hivi kwanini serikali isiunganishe mikoa ya Dar na Pwani kisha huo mkoa uitwe Dar na tubaki na mikoa 30 tu, hakuna haja ya kuwa na mikoa mingi huku maendeleo yakiwa ni madogo na idadi ya watu ikilundikana kwenye vimiji vichache tu, kusema kwamba tutamaliza mapori na kuharibu mazingira kwa vizazi vijavyo ni upotoshaji kwa sababu Tanzania bado hakuna population ya kumaliza mapori yote tuliyonayo

Ni ajabu kwamba mkoa mdogo kijiografia kuliko yote nchini ndio mkoa mkubwa kidemografia kuliko yote nchini, ukiuliza sababu hakuna sababu ya maana utapewa zaidi ya watu wengi hasa vijana, kutaka waonekane wanaishi Dar hata kama maisha yao hayaeleweki na huko mikoani wameona fursa

Juzi nilikuwa nasikiliza interview ya Mwijaku alipokuwa anawajibu watu wanaosema kwamba kajenga ghorofa lake kwenye kaeneo kadogo, akasema alikuwa na eneo karibu ekari mbili huko Bagamoyo, ila hakutaka kujenga huko sababu hati ya nyumba yake ingesoma Pwani na yeye anataka isome Dar

Sasa nimemtolea mfano huyo sababu ni maarufu lakini kiuhalisia hizi ndio akili za vijana wengi walioko kwenye hili jiji, wapo wengi sana ninaowafahamu ambao nao wana mawazo kama haya ya kutaka kuonekana wanaishi Dar tu na si sehemu nyingine, sasa tukumbuke idadi ya watu Dar inazidi kuongezeka siku hadi siku ila ukubwa wa mkoa hauongezeki

Kwa mtazamo wangu naona suluhisho pekee ni kuunganisha hii mikoa miwili Pwani yote nayo iitwe Dar, kuhusu wilaya kuwa nyingi sioni kama ni tatizo maana hata mkoa wa Tanga una wilaya nyingi kulinganisha na idadi ya wakazi wake so sioni kama ni tatizo kufanya hivyo hata kwa Dar, ambao ndio mkoa wenye idadi kubwa ya wakazi na kama wakiona utakuwa na wilaya nyingi basi wanaweza waka merge baadhi ya wilaya

Sasa hivi miji inakuwa kuelekea Bagamoyo, Kisarawe, Chalinze na Mkuranga kwa maana kwamba watu wameanza kuchangamkia ardhi huko na wengine wameanza kujenga, lakini ukuaji wake bado hauna kasi kulinganisha na idadi ya watu wanaohamia Dar kila siku, hakuna haja ya kuwa na mkoa specific unaoitwa Pwani wakati hata Dar, Tanga, Lindi na Mtwara nayo ni mikoa ya Pwani

Hapa simaanishi miji ikuwe makazi ya watu tu bali hata huduma za kijamii kama ni ofisi, masoko, shule, hospitali, hoteli, malls, bars, restaurants na huduma nyinginezo, lakini hizo asilimia kubwa hufuata makazi ya watu mtu hawezi kufungua tu biashara yake sehemu ambayo hana uhakika wa wateja wa kutosha, kwahiyo ni lazima watu waanze kwanza kuhamia ndipo huduma zitafuata, sasa kwa akili hizi za watu kutaka kuonekana wanaishi Dar tusitegemee Pwani itakuwa haraka

Kama ni ushamba wa bahari mbona hata Bagamoyo na Mkuranga bahari ipo ila bado kuna mapori, nashangaa baadhi ya watu wanataka mikoa izidi kugawanywa wakati hii iliyopo tu maendeleo yametushinda, haya ya kusema eti kawilaya kakishakuwa na tuhuduma fulani twa kijamii hata kama ni tubovu basi kanafaa kuwa mkoa unaojitegemea sioni kama yanasaidia

Kuna mahali nilisoma eti na wakazi wa Masasi nao wanataka hiyo wilaya iwe mkoa eti kisa tu biashara ya korosho yani kuna mambo yanachekesha kwa kweli, huo mkoa wa Mtwara tu bado hamjamalizana nao mnataka muanzishe mkoa wa Masasi tena, halafu hata kijiografia Mtwara siyo mkoa mkubwa kihivyo wa kuhitaji kugawanywa kuna mikoa mikubwa kama Morogoro, Tabora, Lindi nk ambayo ndio inastahili kugawanywa

Hata hivyo hii gawanya gawanya ya mikoa na wilaya inazidi kuongeza idadi ya makabila tu maana nimekuja kugundua hii nchi ina makabila zaidi ya haya tunayoyajua, mengine unakuta ni mtu tu na mkewe na wanaye walihamia pori fulani wakakuta hapana watu wakaanzisha kijiji na kikabila chao hatimaye kikakuwa na kupata watu basi nao wanataka watambulike, mara makabila mengine unasikia eti ni muunganiko wa kabila fulani na kabila fulani sasa hayo yote ya nini ikiwa vitu muhimu kama maji, umeme, afya, elimu, uchumi na teknolojia vinatushinda na ndio maana Nyerere alipiga marufuku mambo ya kuendekeza makabila

Kwahiyo maoni yangu ni kwamba badala ya kuendelea kugawanya mikoa tuangalie kama kuna mikoa ambayo inaweza kuunganishwa iunganishwe, na kwa sasa nilikuwa napendekeza tuanze na Dar na Pwani tubaki na mikoa 30 tu tupambane kuiendeleza kwanza hiyo, na siyo kuwa na mikoa mingi ambayo imejaa mapori tu na huduma mbovu za kijamii pamoja na maendeleo duni
Ndivyo ilikuwa hapo swali kabla ya kugawanywa.

Naunga mkono hoja.Hata hivyo eneo linapokuwa kubwa ndio maendeleo yanachelewa tofauti na eneo la Utawala likiwa dogo.
 
Mawazo kama haya wangekuwa nayo wabunge wetu tungewaona wa maana lakini wao kazi yao ni kugonga meza na kuitikia tu ndiyooooo..!!
 
Heri ya mwaka mpya wakuu

Hivi kwanini serikali isiunganishe mikoa ya Dar na Pwani kisha huo mkoa uitwe Dar na tubaki na mikoa 30 tu, hakuna haja ya kuwa na mikoa mingi huku maendeleo yakiwa ni madogo na idadi ya watu ikilundikana kwenye vimiji vichache tu, kusema kwamba tutamaliza mapori na kuharibu mazingira kwa vizazi vijavyo ni upotoshaji kwa sababu Tanzania bado hakuna population ya kumaliza mapori yote tuliyonayo

Ni ajabu kwamba mkoa mdogo kijiografia kuliko yote nchini ndio mkoa mkubwa kidemografia kuliko yote nchini, ukiuliza sababu hakuna sababu ya maana utapewa zaidi ya watu wengi hasa vijana, kutaka waonekane wanaishi Dar hata kama maisha yao hayaeleweki na huko mikoani wameona fursa

Juzi nilikuwa nasikiliza interview ya Mwijaku alipokuwa anawajibu watu wanaosema kwamba kajenga ghorofa lake kwenye kaeneo kadogo, akasema alikuwa na eneo karibu ekari mbili huko Bagamoyo, ila hakutaka kujenga huko sababu hati ya nyumba yake ingesoma Pwani na yeye anataka isome Dar

Sasa nimemtolea mfano huyo sababu ni maarufu lakini kiuhalisia hizi ndio akili za vijana wengi walioko kwenye hili jiji, wapo wengi sana ninaowafahamu ambao nao wana mawazo kama haya ya kutaka kuonekana wanaishi Dar tu na si sehemu nyingine, sasa tukumbuke idadi ya watu Dar inazidi kuongezeka siku hadi siku ila ukubwa wa mkoa hauongezeki

Kwa mtazamo wangu naona suluhisho pekee ni kuunganisha hii mikoa miwili Pwani yote nayo iitwe Dar, kuhusu wilaya kuwa nyingi sioni kama ni tatizo maana hata mkoa wa Tanga una wilaya nyingi kulinganisha na idadi ya wakazi wake so sioni kama ni tatizo kufanya hivyo hata kwa Dar, ambao ndio mkoa wenye idadi kubwa ya wakazi na kama wakiona utakuwa na wilaya nyingi basi wanaweza waka merge baadhi ya wilaya

Sasa hivi miji inakuwa kuelekea Bagamoyo, Kisarawe, Chalinze na Mkuranga kwa maana kwamba watu wameanza kuchangamkia ardhi huko na wengine wameanza kujenga, lakini ukuaji wake bado hauna kasi kulinganisha na idadi ya watu wanaohamia Dar kila siku, hakuna haja ya kuwa na mkoa specific unaoitwa Pwani wakati hata Dar, Tanga, Lindi na Mtwara nayo ni mikoa ya Pwani

Hapa simaanishi miji ikuwe makazi ya watu tu bali hata huduma za kijamii kama ni ofisi, masoko, shule, hospitali, hoteli, malls, bars, restaurants na huduma nyinginezo, lakini hizo asilimia kubwa hufuata makazi ya watu mtu hawezi kufungua tu biashara yake sehemu ambayo hana uhakika wa wateja wa kutosha, kwahiyo ni lazima watu waanze kwanza kuhamia ndipo huduma zitafuata, sasa kwa akili hizi za watu kutaka kuonekana wanaishi Dar tusitegemee Pwani itakuwa haraka

Kama ni ushamba wa bahari mbona hata Bagamoyo na Mkuranga bahari ipo ila bado kuna mapori, nashangaa baadhi ya watu wanataka mikoa izidi kugawanywa wakati hii iliyopo tu maendeleo yametushinda, haya ya kusema eti kawilaya kakishakuwa na tuhuduma fulani twa kijamii hata kama ni tubovu basi kanafaa kuwa mkoa unaojitegemea sioni kama yanasaidia

Kuna mahali nilisoma eti na wakazi wa Masasi nao wanataka hiyo wilaya iwe mkoa eti kisa tu biashara ya korosho yani kuna mambo yanachekesha kwa kweli, huo mkoa wa Mtwara tu bado hamjamalizana nao mnataka muanzishe mkoa wa Masasi tena, halafu hata kijiografia Mtwara siyo mkoa mkubwa kihivyo wa kuhitaji kugawanywa kuna mikoa mikubwa kama Morogoro, Tabora, Lindi nk ambayo ndio inastahili kugawanywa

Hata hivyo hii gawanya gawanya ya mikoa na wilaya inazidi kuongeza idadi ya makabila tu maana nimekuja kugundua hii nchi ina makabila zaidi ya haya tunayoyajua, mengine unakuta ni mtu tu na mkewe na wanaye walihamia pori fulani wakakuta hapana watu wakaanzisha kijiji na kikabila chao hatimaye kikakuwa na kupata watu basi nao wanataka watambulike, mara makabila mengine unasikia eti ni muunganiko wa kabila fulani na kabila fulani sasa hayo yote ya nini ikiwa vitu muhimu kama maji, umeme, afya, elimu, uchumi na teknolojia vinatushinda na ndio maana Nyerere alipiga marufuku mambo ya kuendekeza makabila

Kwahiyo maoni yangu ni kwamba badala ya kuendelea kugawanya mikoa tuangalie kama kuna mikoa ambayo inaweza kuunganishwa iunganishwe, na kwa sasa nilikuwa napendekeza tuanze na Dar na Pwani tubaki na mikoa 30 tu tupambane kuiendeleza kwanza hiyo, na siyo kuwa na mikoa mingi ambayo imejaa mapori tu na huduma mbovu za kijamii pamoja na maendeleo duni
Wazo la kijinga sana

Baada ya miaka 100 utaunganisha Morogoro na Tanga iwe tena Dar es Salaam maana kote pakua pamejaa?

Solution hapa ni kuendeleza miji mingine nayo iwe mizuri kama Dar watu wahamie au kubaki huko wasilazimike kuja Dar ili Dar isijae ipumue

Cha msingi ndio hicho,lazima kuwe na miji mizuri pembeni across ya country ili kupunguza traffic ya watu kuja Dar
 
H
Kwani ilivyo hivi sasa inakuzuwia nini kuishi Pwani ukafanya kazi Dar au Kuishi Dar ukafanya kazi Pwani?

Mbona wapo wengi sana wanafanya hivyo?


Dar yote ilikuwa Mkoa wa Pwani mpaka ilivyokatwa na kuwa mkoa wa pekee.
Huyo aliyekata ali angalia mahitaji na huduma kwa kipindi hiko, watu walikuwa wachache dar, sasa watu ni wengi ila jiji liko pale pale halija tanuka, ofisi zote yaani kila kitu ni dar, sasa imefika muda serikali kutanua hili jiji kwa maana ya kwamba Kupeleka miundombinu nje ya dar, mfano hii barabara ya njia 4 kutoka kibaha mpaka chalinze, ilitakiwa kila sehemu ijengwe barabara ndefu kama hiyo, mfano kule tegeta piga barabara njia nne mpaka bagamoyo huko mbele kabisa, hivyo hivyo gongolamboto iwe barabara ndefu mpaka kibiti mbele huko... Basi hapo kutakuwa na mwamko mkubwa sana wa watu wataenda kuishi huko
 
Ukifanya hivi huo mkoa wa pwani utakufa sasa, maana pwani yenyewe ina tegemea mapato toka kwenye hizo sehemu maana tayari zime changamka.
Uko sahihi, ila kwa upande wangu naona ni bora kuchukua maeneo kadhaa ya mkoa wa Pwani kama vile Bagamoyo, Kibaha, Chalinze, kisarawe na kibiti hayo maeneo ndio yawe sehemu ya Dar mana mkoa wa pwani ni mkubwa sana (hvy kwa kufanya hvy itakuwa ni sawa na kugawa mkoa wa pwani kupata mikoa miwili)
 
H

Huyo aliyekata ali angalia mahitaji na huduma kwa kipindi hiko, watu walikuwa wachache dar, sasa watu ni wengi ila jiji liko pale pale halija tanuka, ofisi zote yaani kila kitu ni dar, sasa imefika muda serikali kutanua hili jiji kwa maana ya kwamba Kupeleka miundombinu nje ya dar, mfano hii barabara ya njia 4 kutoka kibaha mpaka chalinze, ilitakiwa kila sehemu ijengwe barabara ndefu kama hiyo, mfano kule tegeta piga barabara njia nne mpaka bagamoyo huko mbele kabisa, hivyo hivyo gongolamboto iwe barabara ndefu mpaka kibiti mbele huko... Basi hapo kutakuwa na mwamko mkubwa sana wa watu wataenda kuishi huko
Sifahamu hayo unayoyasema yanahusiana nini na kufanywa mkoa mmoja.

Kuwa mkoa zaidi ya mmoja ni kugawa madaraka ya utawala.

Hata Dar yenyewe kuna baadhi ya idara za serikali zimeugawa mkoa kuwa mikoa maalum kiutawala.
 
Wazo la kijinga sana

Baada ya miaka 100 utaunganisha Morogoro na Tanga iwe tena Dar es Salaam maana kote pakua pamejaa?

Solution hapa ni kuendeleza miji mingine nayo iwe mizuri kama Dar watu wahamie au kubaki huko wasilazimike kuja Dar ili Dar isijae ipumue

Cha msingi ndio hicho,lazima kuwe na miji mizuri pembeni across ya country ili kupunguza traffic ya watu kuja Dar
Kuhusu hiyo aya yako ya mwanzo nilishatoa ufafanuzi kuunganisha Dar na Pwani hakuhusiani na maendeleo ya miji mingine hiyo ni mada nyingine, hoja yangu ni kwamba Dar ndio mkoa mdogo kuliko yote kijiografia ila ndio mkoa mkubwa kuliko yote kidemografia, hivyo kuuunganisha na Pwani kuna afadhali kuliko kuuacha hivi ulivyo
 
Back
Top Bottom